MAHITAJI

Wafer Powder/gram wafer (unga wa biskuti uliosagwa wa tayari) - vikombe 2

Maziwa ya Mgando Matamu ya Kopo - 2 vikombe

Nazi iliyokunwa - ½ Kikombe

Chokoleti vipande vipande - 1 Kikombe

Njugu vipande vipande - ½ Kikombe

Siagi - 227 g

MAPISHI

Yeyusha siagi motoni kisha changanya na unga wa wafer acha kidogo motoni
Mimina katika treya unayochomea itandaze vizuri, kisha mimina maziwa juu yake pamoja na njugu vipande , nazi iliyokunwa na vipande vya chokoleti.
Choma (bake) kwenye oveni kwa moto wa 350ºC kwa dakika 20.
Katakata tayari kwa kuliwa