Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Jinsi ya kuishi maisha marefu (Mambo ya kuzingatia ili uishi maisha marefu)
Updated at: 2024-05-25 10:34:45 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kuishi ukiwa na afya na kuishi maisha marefu kunawezekana kwa kubadili hali ya maisha unayoishi inayoharibu afya yako mfano uvutaji wa sigara, unywaji wa pombe kupita kiasi,kutokufanya mazoezi na kutokula matunda na mbogamboga.
Mambo yanayoweza kukusaidia kuishi maisha marefu ni kama yafuatayo
Kuuandaa mwili kwa maisha marefu kwa kufanya mazoezi
Kuwa makini kutambua na kutibu matatizo ya kiafya
Kuepuka mazingira na kufanya kazi kwa namna au kazi zinazoweza kudhuru maisha yako. Mfano kuendesha gari bila kufuata utaratibu, kutokuvaa vifaa vya kujikinga wakati wa kazi
Epuka vitu vyenye sumu vinavyoweza kudhuru afya yako na kukuletea matatizo ya kiafya kama dawa za mimea na mifugo, zitumie kama inavyotakiwa
Usinywe pombe, usivute sigara wala kutumia dawa za kulevya
Tofauti kati ya yai la kuku wa kienyeji na la kuku wa kisasa
Updated at: 2024-05-25 10:34:45 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kilishe mayai yote ni sawa. Virutubishi vinavyopatikana kwenye yai la kuku wa kienyeji kama protini, vitamini A, madini ya chuma na virutubishi vya aina nyingine, ndivyo hivyo vinavyopatikana pia kwenye yai la kuku wa kisasa.
Tatizo linaweza kutokea pale ambapo wafugaji wa kuku wa kisasa hawafuati taratibu za ufugaji na pengine hawawapi kuku vyakula muhimu wanavyohitaji au wanawapa dawa na vyakula visivyo bora kiafya, hivyo wakati mwingine kiini cha yai la kuku wa kisasa huonekana kupungua rangi ya njano kuliko kiini cha yai la kuku wa kienyeji.
Mtu anashauriwa kula yai bila kujali ni la kuku gani, kwa kutegemea ni yai lipi linapatikana kwa urahisi. Lakini nivizuri kula mayai ambayo yapo salama.
Updated at: 2024-05-25 10:37:47 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Dagaa wabichi (Fresh anchovies packet 1) Unga wa ugali (corn meal flour 1/4 kilo) (unaweza kutumia unga wa choice uipendayo) Matembele ya kukaushwa (dried sweet potato leaves, handful) Nyanya ya kopo (tin tomato 1) Kitunguu maji (onion 2) Limao (lemon 1/4) Pilipili mbuzi nzima bila kukata (scotch bonnet pepper1, do not chop) Chumvi (salt 1/2 ya kijiko cha chai) Mafuta (vegetable oil) Hoho (green pepper 1) Kitunguu swaum (garlic 5 cloves) Tangawizi (ginger 1 kijiko cha chai) Binzari ya curry (Curry powder 1/2 kijiko cha chai)
Matayarisho
Safisha dagaa kwa kutoa vichwa na utumbo kisha waoshe na uwakaushe na kitchen towel na uwaweke pembeni. Baada ya hapo katakata, vitunguu na hoho kisha weka pembeni. Baada ya hapo weka sufuria jikoni na utie mafuta yakisha pata moto tia dagaa na uwakaange mpaka wawe wa brown, kisha tia kitunguu swaum,curry powder na tangawizi, kaanga kidogo kisha malizia kwa kutia vitunguu maji, hoho,pilipili,chumvi na ukamulie limao. Kaanga kwa muda wa dakika 3-4 na hakikisha vitunguu na hoho haviivi sana na hapo dagaa watakuwa tayari.
Baada ya hapo yaoshe na uyaloweka matembele (kama ni makavu) kwa muda wa dakika 15, Kisha yatoe na uyaweke kwenye sufuria pamoja na kitunguu, nyanya, chumvi ,kamulia limao kidogo, pilipili na maji kiasi. acha matembele yachemke kwa muda wa dakika 20 na uhakikishe yameiva kwa kuwa laini. Baada ya hapo yapike mpaka maji yote yakauke na mafuta yatok na hapo matembele yatakuwa tayari.
Ukisha maliza kupika dagaa na matembele andaa chungu cha ugali. Kwanza unatakiwa kuchemsha maji ya moto, kisha koroga pembeni unga kiasi katika maji ya baridi na utie kwenye maji yanayochemka, Fanya kama unatengeneza uji, uji wa ugali ukishachemka tia unga na uanze kuusonga mpaka ugali uive. Ukisha iva pakua na usevu na mboga tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:34:41 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Tambi (vermiceli Roasted) Mifuko 2
Siagi - 4 Vijiko vya supu
Maziwa (condensed) 300Ml
Lozi zilizokatwakatwa - 1 kikombe
Zabibu kavu - 1 Kikombe
Arki (essence) - 1 Kijiko cha supu
MAPISHI
Weka karai kwenye moto kiasi Tia siagi Tia tambi uzikaange usiachie mkoni mpaka ziwe rangu ya dhahabu. Weka lozi na zabibu huku unakoroga Tia maziwa na huku unakoroga usiachie mkono. Tia arki Epua karai, tumia kijiko cha chai kwa kuchotea na utie kwenye kikombe cha kahawa nusu usikijaze. Kipindue kwenye sahani utoe kileja. Fanya hivyo mpaka umalize vyote.
Updated at: 2024-05-25 10:37:35 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele wa basmati - 3 vikombe
Kuku - ½
Viazi - 4
Vitunguu - 2
Kitunguu saumu(thomu/galic) iliyosagwa - 2 vijiko vya supu
Binzari ya pilau nzima - 1 Kijiko cha chakula
Binzari ya pilau - ½ kijiko cha chai
Pilipili manga nzima - ½ kijiko cha chai
Karafuu nzima - 8
Iliki nzima - 6
Mdalasini nzima - 5 vijiti
Pilipili mbichi iliyosagwa - 2
Chumvi - kiasi
Mafuta ya kupikia - ¼ kikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika:
Osha mchele na roweka kwa muda kutegemea na aina ya mchele. Kata kuku vipande upendavyo, safisha kisha mchemshe kwa chumvi, pilipili iliyosagwa, thomu na tangawizi. Akiwiva kuku, mtoe weka kando, bakisha supu katika sufuria. Katika sufuria, kaanga vitunguu hadi vigeuke rangu ya hudhurungi. Tia thomu na tangawizi na binzari zote kaanga kidogo Kisha tia viazi kanga kidogo kisha tia kisha tia vipande vyako vya kuku na supu acha ichemke kidogo kisha tia maji ukisie kutokana na mchele unaotumia. Mwisho tia mchele koroga uchanganye na vitu vyote acha ichemke kiasi kisha funika na punguza moto mpaka uive (huku ukiugeuzageuza) Ukishakuwa tayari pakua kwenye sahani tayari kwa kula na salad na pilipili.
Updated at: 2024-05-25 10:34:42 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Unga wa ngano - 2 - 2 ¼ Vikombe
Siagi - 1 ½ Kikombe
Sukari - 1 Kikombe
Yai - 1
Vanilla -Tone moja
Baking Powder -kijiko 1 cha chai
Chumvi - Kiasi kidogo (pinch)
Unga wa Kastadi - 2 Vijiko vya supu
MATAYARISHO
Changanya vitu vyote isipokuwa unga. Tia unga kidogo kidogo mpaka mchanganyiko uwe sawa. Kisha fanya duara ndogo ndogo uzipange kwenye treya na utie rangi katikati. Halafu zichome katika moto wa 300°F kwa muda wa dakika 20 - 25 na zisiwe browni . Kisha panga kwenye sahani tayari kuliwa na chai.
Updated at: 2024-05-25 10:37:48 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Bilinganya 2 za wastani Nyanya kubwa 1 Kitunguu maji 1 kikubwa Swaum 1/2 kijiko cha chai Limao 1/4 Pilipili ya unga 1/2 kijiko cha chai Parpika 1/4 kijiko cha chai Pilipili mtama 1/4 kijiko cha chai Curry powder1/4 kijiko cha chai Chumvi kiasi Coriander Olive oil
Matayarisho
Katakata bilinganya slice nyembamba kisha ziweke pembeni. Baada ya hapo kaanga kitunguu maji mpaka kiwe cha brown kisha tia swaum na spice zote, zikaange kidogo kisha tia nyanya na chumvi kiasi. Pika nyanya mpaka iive na itengane na mafuta. Baada ya hapo tia mabilinganya na ukamulie limao kisha punguza moto na uyafunike na mfuniko usioruhusu kutoa mvuke ili yaivie na huo mvuke. Baada ya hapo yaonje kama yameiva na malizia kwa kutia fresh coriander na baada ya hapo yatakuwa tayari kwa kuliwa. kwa kawaida mi hupendaga kuyalia na wali na maharage badala ya kachumari kwahiyo nakuwa naitumia hiyo kama kachumbari
Jinsi ya kupika Pilau ya Nyama ya Kusaga Na Mboga Mchanganyiko
Updated at: 2024-05-25 10:23:13 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele - 2 Mugs
Viazi - 3
Nyama ya Kusaga - 1 Pound
Mboga mchanganyiko za barafu - 1 Mug
(Frozen vegetable)
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi - 2 vijiko vya supu
Garam masala - 1 kijiko cha supu
Nyanya - 1
Kitungu maji - 1
Mdalasini nzima - 1 vijiti
Karafuu - 3 chembe
Pilipili mbichi - 1
Chumvi - kiasi
Maji - 2 ½ Mugs
Mafuta - 3 vijiko vya supu
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha mchele na uroweke kiasi kutegemea aina ya mchele. Katakata viazi kaanga katika mafuta, toa weka kando. Tia mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu maji mpaka kigeuke rangi ya hudhurungi (brown). Tia nyama ya kusaga, thomu na tangawizi, pilipili, bizari zote na chumvi. Kaanga hadi nyama iwive. Katakata nyanya uliyokatakata itie katika mchanganyiko wa nyama na endelea kukaanga kidogo tu. Tia mboga ya barafu (frozen vegetables) Tia maji, kidonge cha supu. Yatakapochemka tia mchele. Punguza moto uwe mdogo funika kwa muda wa ½ saa hadi wali ukauke na uwive. Utakuwa tayari kuliwa.