Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Mapishi ya Pilau Ya Adesi Za Brown Karoti Na Mchicha Kwa Samaki Wa Salmon
Updated at: 2024-05-25 10:37:37 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Mchele vikombe 3
Karoti 1 ikune (grate)
Mchicha katakata kiasi
Adesi za brown
Kitunguu katakata (chopped)
Supu ya kitoweo chochote upendayo au vidonge vya supu 2
Garama masala (bizari mchanganyiko) kijiko 1 cha kulia
Samli ¼ kikombe
Chumvi kiasi
Vipimo Vya Samaki Wa Salmon
Samaki wa Salmon vipande 4 vikubwa
Tangawizi mbichi ilosagwa kijiko 1 cha kulia
Thomu (garlic/saumu) kijiko 1 cha kulia
Chumvi kiasi
Bizari ya mchuzi kijiko 1 cha kulia
Ndimu 1 kamua
Nyanya 2 kata slice kubwa kubwa
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Samaki wa Salmon
Changanya viungo vyote upake katika samaki. Weka katika treya na panga slice za nyanya juu yake. Oka (grill/choma) katika oven umgeuze samaki upande wa pili. Akiwa tayari epua.
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Wali
Roweka mchele kiasi kutegemea aina ya mchele. Tumia basmati (pishori) Roweka adesi kisha zichemshe katika maji ya kiasi. Chuja maji adesi na maji yatakayobakia tumia katika kupikia pilau hii. Kaanga vitunguu katika samli iliyoshika moto kwenye sufuria ya kupikia. Vikianza kugeuka rangi tia karoti, mchicha, adesi, bizari mchanganyiko kisha kaanga kidogo. Tia mchele ukaange kidogo kisha tia supu au maji pamoja na kidonge cha supu. Tia chumvi ukoroge funika upike kama pilau. Epua upakue katika sahani utolee kwa samaki wa salmon
Updated at: 2024-05-25 10:34:40 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Ndizi mbichi - 10
Nyama - kilo 1
Nazi ya kopo - 1
Chumvi - 1 Kijiko cha chakula
Ndimu - 1
Bizari ya manjano - 1 Kijiko cha chai
Pili pili mbichi - 3
Nyanya (tomatoes) - 2
Kitunguu maji - 1
Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi iliyosagwa - 1 Kijiko cha chakula
Namna ya Kutayarisha Na Kupika
Kata nyama vipande vipande na uisafishe. Chemsha nyama weka chumvi, thomu, tangawizi na ndimu. Iache iwive. Kata kata nyanya na kitunguu, kisha mimina kwenye nyama inayochemka, weka na bizari nusu kijiko. Wacha supu iwive kisha weka pembeni. Ukumbusho: Hakikisha supu inakuwa kiasi na si nyingi. Menya maganda ndizi na uzikate vipande vipande vya kiasi. Zikoshe ndizi na uziweke ndani ya sufuria. Weka maji ndani ya sufuria kisha zichemshe ndizi mpaka ziwe laini kidogo. Zimwage maji ndizi kisha mimina supu na nyama ndani ya ndizi. Mimina nazi pili pili na bizari nusu kijiko ndani ya ndizi na uziweke kwenye jiko zichemke mpaka zibakie na urojo kiasi. Onja chumvi na uongeze kadri utakavyopenda. Weka pembeni zipoe. Pakua ndizi kwenye sahani au bakuli tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:38 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Mchele basmati, pishori - 3 vikombe
Vitunguu katakata - 2
Nyanya/tungule katakata - 5 takriban
Viazi/mbatata menya katakata - 3 kiasi
Thomu (saumu/garlic) ilosagwa - 1 kijiko cha supu
Bizari mchanganyiko - 1 kijiko cha kulia
Hiliki ya unga - ½ kijiko cha chai
Kidonge cha supu - 2
Chumvi - kisia
Mafuta - ½ kikombe
Maji ya moto au supu - 5 takriban
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha na roweka mchele Katika sufuria weka mafuta yashike moto, tia viazi, vitunguu ukaange. Vikianza tu kugeuka rangi tia thomu na bizari, hiliki, endelea kukaanga kidogo. Tia nyanya kaanga lakini usiache zikavurugika sana. Tia mchele ukaange chini ya dakika moja. Tia maji ya moto, na kidonge cha supu au supu yoyote kiasi cha kufunika mchele yazidi kidogo. Koroga vichanganyike vitu, kisha funika upike kama pilau. Pakua ikiwa tayari, tolea kwa samaki wa kukaanga au kitoweo chochote kile
Updated at: 2024-05-25 10:34:44 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Njia za kupima Afya
Njia mbalimbali hutumika kupima hali ya lishe, njia hizi ni;
1. Vipimo vya umbile la mwili
2. Vipimo vya maabara
3. Kuchukua historia ya ulaji na maradhi
Vipimo vya umbile la mwili
Baadhi ya vipimo ambavyo vinaweza kutumika kutoa tahadhari kuhusu magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza ni;
1. Uwiano wa uzito na urefu au Body Mass Index (BMI).
2. Mzunguko wa kiuno.
3. Uwiano wa mzunguko wa kiuno na nyonga.
4. Kulinganisha uzito na umri.
Uwiano wa uzito na urefu au Body Mass Index (BMI).
Hiki ni kipimo kinachotumika kuangalia uwiano wa urefu na uzito wa mtu, ni muhimu kuchukua vipimo kwa usahihi.Uwiano wa uzito katika Kilogramu na urefu katika mita hupatikana kwa kutumia kanuni ifuatayo:
BMI= uzito (Kg)/Urefu2 (m2)
BMI huwa na viwango mbalimbali vilivyowekwa na shirika la Afya duniani (WHO) kutafsiri hali ya lishe ya mtu ambavyo ni
1. BMI chini ya 18.5 = uzito pungufu.
2. BMI kati ya 18.5 mpaka 24.9= uzito unaofaa.
3. BMI kati ya 25.0 mpaka 29.9 = unene uliozidi.
4. BMI ya 30 au zaidi = unene uliokithiri au kiribatumbo.
Mahitaji ya chakula mwilini hutegemea umri, jinsi, hali ya kifiziolojia (kama ujauzito na kunyonyesha), hali ya kiafya, kazi na mtindo wa maisha. Uzito wa mwili hutegemea na chakula unachokula, pamoja na shughuli unazofanya, mara nyingi unene hutokana na kula chakula kwa wingi. Unene uliokithiri unachangia kwa kiwango kikubwa kupata magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza kama kisukari, magonjwa ya moyo, shinikizo kubwa la damu, na saratani. Uzito uliozidi unapaswa kupunguzwa ili kuepuka magonjwa sugu yasiyo ya kuambukiza
Jinsi ya kupunguza unene uliozidi
1. Tumia mafuta kwa kiasi kidogo kwenye chakula
2. Epuka kula vyakula vyenye mafuta mengi hususani vinavyopikwa kwa kudumbukizwa kwenye mafuta, au vinavyokaangwa kwa mafuta mengi.
3. Epuka matumizi ya vinywaji au vyakula venye sukari nyingi
4. Epuka asusa zenye mafuta mengi au sukari nyingi kati ya mlo na mlo.
5. Ongeza vyakula venye makapi- mlo kwa wingi kama matunda, mboga mboga na nafaka zisizokobolewa.
BMI haitumiki kwa wanawake wajawazito, BMI haitumiki kwa watoto na vijana walio na umri chini ya miaka 18, BMI haitumiki kwa watu wasioweza kusimama vyema, waliovimba miguu, na wanawake wanaonyonyesha katika miezi sita ya mwanzo baada ya kujifungua.
Updated at: 2024-05-25 10:37:37 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Boga la kiasi - nusu yake
Tui zito la nazi 1 ½ gilasi
Sukari ½ kikombe
Hiliki ½ kijiko cha chai
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Menya boga kisha katakata vipande vya kiasi. Weka katika sufuri tia maji kiasi ya kuchemshia na kuwiva bila ya kubakia maji mengi. Changanya tui na sukari na hiliki kisha mimina juu ya boga wacha katika moto dakika chache tu bila ya kufunika. Epua mimina katika chombo likiwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:22:58 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Unga wa ngano (plain flour 1/2 of kilo) Siagi (butter vijiko 2 vya chakula) Yai (egg 1) Chumvi (1/2 ya kijiko cha chai) Hiliki (ground cardamon 1/4 ya kijiko cha chai) Maji ya uvuguvugu (warm water) Mafuta (vegetable oil)
Matayarisho
Weka unga wa ngano katika bakuli la kukandia, kisha tia chumvi na hiliki na uchanganye kwanza, baada ya hapo tia siagi na uichanganye vizuri na unga mpaka ipotee. Baada ya hapo tia tena yai na uchanganye vizuri. Mchanganyiko ukishachanganyika vizuri sasa unaweza kutia maji ya uvuguvugu kidogo, kidogo huku ukiwa unauchanganya ili kupata donge. Baada ya hapo anza kukanda hilo donge mpaka mabuje yote yapotee na unga uwe mlaini, ambapo itakuchukua kama dakika 15. Baada ya hapo tawanyisha unga katika madonge ya wastani (yasiwe makubwa sana au madogo sana) Ukimaliza hapo, andaa kibao cha kusukumia chapati kwa kukitia unga kidogo ili chapati isinatie kwenye kibao. Sukuma donge moja la chapati mpaka liwe flat na kisha weka kijiko kimoja cha mafuta na usambaze. ukisha maliza ikunje (roll). Fanya hivyo kwa madonge yote yaliyobakia. Baada ya hapo andaa chuma cha kuchomea (fry-pan) katika moto wa wastani. Kisha anza kusukuma chapati (ni vizuri ukaanza na zile ulizozikunja mwanzo ili kuzipa nafasi zile za mwisho ziweze kulainika) ukiwa unasukuma hakikisha zinakuwa flat (na zisiwe nene sana au nyembamba sana) Ukishamaliza hapo tia kwenye chuma cha kuchomea. Acha iive upande mmoja then igeuze upande wa pili. Tia mafuta ama kijiko kimoja kikubwa upande wa chini wa chapati na uanze kuukandamiza kwa juu uku ukiwa unaizungusha. fanya hivyo uku ukiwa unaigeuza kuiangalia kwa chini ili isiungue. ikishakuwa ya brown, geuza upande wa pili na urudie hivyohiyvo mpaka chapati iive. Rudia hii process kwa chapati zote zilizobakia.
Siri ya chapati kuwa laini ni kutia siagi au mafuta ya kutosha kipindi unazikanda na pia kuzikanda mpaka unga uwe laini.
Updated at: 2024-05-25 10:34:41 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Tambi (vermiceli Roasted) Mifuko 2
Siagi - 4 Vijiko vya supu
Maziwa (condensed) 300Ml
Lozi zilizokatwakatwa - 1 kikombe
Zabibu kavu - 1 Kikombe
Arki (essence) - 1 Kijiko cha supu
MAPISHI
Weka karai kwenye moto kiasi Tia siagi Tia tambi uzikaange usiachie mkoni mpaka ziwe rangu ya dhahabu. Weka lozi na zabibu huku unakoroga Tia maziwa na huku unakoroga usiachie mkono. Tia arki Epua karai, tumia kijiko cha chai kwa kuchotea na utie kwenye kikombe cha kahawa nusu usikijaze. Kipindue kwenye sahani utoe kileja. Fanya hivyo mpaka umalize vyote.
Updated at: 2024-05-25 10:23:12 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viambaupishi
Mchele wa basmati - 3 vikombe
Kuku - ½
Bilingani - 2 ya kiasi
Viazi - 4
Vitunguu - 2
Kitunguu (thomu/galic) iliyosagwa - 2 vijiko vya supu
Pilipili mbichi iliyosagwa - 2
Chumvi - kiasi
Garama masala (mchanganyiko wa bizari) - 1 kijiko cha chai
Hiliki ya unga - ¼ kijiko cha chai
Mafuta ya kupikia wali - ¼ kikombe
Mafuta ya kukaangia viazi na bilingani - kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika:
Osha mchele na roweka kwa muda kutegemea na aina ya mchele. Kata kuku vipande upendavyo safisha Kisha mchemshe kwa chumvi, pilipili iliyosagwa, thomu, na bizari mchanganyiko (garama masala). Akiwiva kuku, mtoe weka kando, bakisha supu katika sufuria. Menya na kata viazi kaanga weka kando. Kata kata bilingani slesi nene kaanga, chuja mafuta weka kando. Katika sufuria, kaanga vitunguu hadi vigeuke rangu ya hudhurungi. Tia vipande vya kuku, ukaange kidogo. Tia supu ya kuku, mchele, tia hiliki, ufunike hadi karibu na kuwiva kabisa. Tia viazi na bilingani uchanganye kidogo, kisha tia katika oven imalizike kupikika pilau humo au unaweza kuendelea kufunika juu ya jiko hadi pilau iwive. Pakua katika sahani ikiwa tayari kuliwa kwa saladi ya mtindi.
Updated at: 2024-05-25 10:37:41 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Kabichi 1/2 kilo Nyanya ya kopo 1/2 Kitunguu 1 Curry powder 1/2 kijiko cha chai Chumvi Olive oil
Matayarisho
Kwanza kabisa bandua magada ya juu ya kabichi, kisha ioshe na uikaushe maji baaba ya hapo katakata kabichi (inapendeza zaidi kama ikikatwa nyembamba) kisha saga pamoja nyanya na kitunguu. Baada yahapo tia katika sufuria ya kupikia, ipike mpaka maji yote yatakapokauka kisha tia chumvi, curry powder na mafuta pika kwa muda kiasi kisha tia kabichi na upunguze moto. Pika mpaka kabishi itakapoiva kisha ipua na itakuwa tayari kwa kuliwa. Unaweza kuila kwa wali au ugali.
Mapishi ya Pilau Ya Nyama ya Kusaga, Adesi Za Brauni Na Zabibu
Updated at: 2024-05-25 10:34:40 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele wa Par boiled au basmati - 5 vikombe
Nyama kondoo/mbuzi ya kusaga - 1 kikombe
Kitunguu - 2
Kitunguu saumu (thomu/galic) - 7 chembe
Adesi za brauni (brown lentils) - 1 kikombe
Zabibu - 1 kikombe
Baharaat/bizari mchanganyiko - 1 kijiko cha supu
Chumvi - kiasi
Pilipilii manga - ½ kijiko
Jiyra/bizari pilau/cummin - 1 kijiko cha chai
Supu ya nyama ng’ombe - Kiasi cha kufunikia mchele
Mafuta - ½ kikombe
Namna Ya Kutayarisha
Osha, roweka masaa 2 au zaidi.
Katakata (chopped)
Menya, saga, chuna
Osha, roweka, kisha chemsha ziive nusu kiini.
Osha, chuja maji
Namna Ya Kupika:
Tia mafuta katika sufuria, kaanga vitunguu hadi vianze kugeuka vyekundu. Tia kitunguu thomu, kaanga, tia baharati/bizari zote kaanga. Tia nyama uchanganye vizuri, ukaange iwive.. Tia mchele ukaange kidogo kisha tia supu, koroga kidogo, funika uivie mchele. Karibu na kuiva, tia adesi, zabibu, changanya, funika uendelee kuiva kama unavyopika pilau. Epua pakua katika chombo, ongezea zabibu kupambia ukipenda