Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Jinsi ya kuandaa Biriani Na Sosi Ya Nyama Ya Mbuzi
Updated at: 2024-05-25 10:23:15 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Nyama Ya Mbuzi - 1 Kilo
Mchele - 4 Magi
Vitunguu - 3
Nyanya - 2
Nyanya kopo - 3 vijiko vya chai
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa - 2 vijiko vya supu
Pilipili mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha supu
Garam Masala (mchanganyiko wa bizari) - 2 vijiko vya supu
Hiliki - 1 kijiko cha chai
Chumvi - kiasi
Mafuta - ½ kikombe
Zaafarani au rangi za biriani za kijani na manjano/orenji
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Sosi Ya Nyama
Changanya nyama na thomu, pilipili, chumvi na nusu ya garam masala. Tia katika treya ya oveni uipike nyama (Bake) hadi iwive. Au iwivishe kwa kuichemsha. Katika kisufuria kingine, tia mafuta (bakisha kidogo ya wali) kaanga vitunguu hadi vigeuke rangi, kisha tia nyanya, nyanya kopo, bizari zote nyingine zilizobakia.
Namna Ya Kupika Wali
Mchele - 4 magi
Mdalasini - 1 kijiti
Hiliki - 3 chembe
Kidonge cha supu - 1
Chumvi
Osha na roweka mchele wa basmati. Tia maji katika sufuria uweke jikoni. Tia kidonge cha supu, mdalasini, hiliki na chumvi . Yakichemka maji tia mchele, funika upike hadi nusu kiini kisha uchuje kwa kumwaga maji. Tia mafuta kidogo katika mchele na zaafarani iliyorowekwa au rangi za biriani kisha rudisha mchele katika sufuria ufunike na upike hadi uwive. Pakua wali katika sahani kisha mwagia sosi ya nyama juu yake, pambia kwa kukatika nyanya, pilipili mboga na figili mwitu (Celery) au mboga yoyote upendayo.
Updated at: 2024-05-25 10:23:09 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Unga wa mchele - 500g
Samli - 250g
Sukari - 250g
Hiliki iliyosagwa - 1/2 kijiko cha chai
Arki (rose flavour) - 1/2 kijiko cha chai
Baking powder - 1 kijiko cha chai
Mayai - 4
Maji ya baridi - 1/2 kikombe cha chai
MAANDALIZI
Saga sukari iwe laini kiasi, changanya unga wa mchele, baking powder, hiliki na sukari. Pasha moto samli mpaka iwe nyepesi kama maji mimina kwenye ule mchanganyiko wa unga wa mchele, kisha uchanganye pamoja na arki. Ongeza mayai yaliopigwa endelea kuchanganya mpaka unga umeanza kuchanganyika vizuri. Ongeza maji ya baridi sana kama nusu kikombe tu ili uchanganyike vizuri. Kata kwa design unayotaka viwe vinene visiwe kama cookies za kawaida kama ilivyo kwenye picha na ukipenda utaweka kidoto kwa kutumia zaafarani katikati ya kileja kama inavyoonesha hapo juu. Choma kwa moto wa baina ya 300F na 350F kwa dakika 15 mpaka 20 visiwe vyekundu toa na tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:23:12 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Wali:
Mchele - 3 Vikombe
Kitunguu kiichokatwa - 1
Pilipili boga nyekundu iliyokatwa vipande - 1
Mafuta - ¼ Kikombe
Zaafarani - 1 kijiko cha chai tia kwenye kikombe na maji robo roweka
Chumvi - 1 kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Katika sufuria, tia mafuta, kaanga kitunguu mpaka kiwe kidogo rangu ya udongo (brown) Tia pili pili boga. Tia mchele, kaanga kwa muda wa dakika 3, tia zaafarani na chumvi. Tia supu uliyochemshia kuku iwe imoto. Pika wali katika moto mdogo hadi uwive.
Kuku
Kuku Mzima -1
Mayai ya kuchemsha - 6
Namna Ya Kupika Kuku
Mchemshe kuku mzima na chumvi mpaka uhakikishe ameiva vizuri. Mtowe na muweke pembeni. Supu yake tumia katika wali kama ilivyo hapo juuu. Chemsha mayai, menya na kata vipande viwili kila yai moja weka kando
Vipimo Vya Sosi Ya Kuku Ya Nazi
Kitunguu - 1
Nyanya iliyokatwa vipande - 1
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi - 1 kijiko cha supu
Garam Masala - ½ kijiko cha supu
Bizari ya manjano - ½ kijiko cha chai
Chumvi - kiasi
Pilipili masala ya unga - ½ kijiko cha chai
Nyanya ya kopo - 1 kijiko cha supu
Nazi ya unga - 1 kikombe
Maji ya ukwaju - ¼ kikombe cha chai
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Tia Mafuta vijiko 2 vya supu katika sufuria Kaanga kitunguu maji mpaka kiwe rangi ya udongo (brown). Tia thomu na tangawizi. Tia nyanya nzima iliyokatwa katwa. Tia garam masala, manjano, pilipili ya unga, nyanya ya kopo, kaanga vizuri. Changanya kwenye sufuria na ukwaju. Iache ichemke vizuri. Changanya nazi ya unga na maji vikombe viwili. Mtie kuku mpike vizuri na hilo tui. Mtie kwenye oveni kidogo.
Kupakuwa katika Sinia
Pakuwa wali kwanza katika sinia Muweke kuku juu ya wali. Pambia mayai
Updated at: 2024-05-25 10:34:47 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Wali wa hoho ni chakula maalum kinachotumika katika hafla au sherehe. Ni chakula chenye ladha nzuri na kina muonekano wa kuvutia kinapokuwa mezani tayari kwa kuliwa.
Mara nyingi huandaliwa kama zawadi katika harusi hususan kwa watu wa pwani. Kwa kuwa zawadi hiyo au maarufu kama kombe huwa kuna vyakula vingi, ikiwamo chakula hiki ambacho hufanya kombe kuwa na muonekano wa kupendeza.
Mbali na kuliwa kama kombe chakula hiki kinaweza kuandaliwa kama mlo wa usiku.
Mahitaji:
• Mchele ½ kg • Nyanya 3 • Mafuta ya kupika ¼ kikombe cha chai • Chumvi kiasi • Kitunguu swaumu kilichosagwa kijiko 1 cha mezani • Kitunguu maji kilichosagwa kijiko 1 cha mezani • Hoho 4 • Nyama ya kusaga ¼ • Tangawizi kijiko 1 cha chakula • Limao au ndimu kipande
Maadalizi:
• Chukua mchele uoshe vizuri kasha chuja maji • Chukua nyama ya kusaga na kamulia ndimu, weka chumvi na tangawizi, changanya vizuri na weka jikoni.iache ichemke hadi ikauke maji yote. • Chukua maji na kiasi cha robo tatu lita chemsha na weka pembeni • Chukua sufuria kavu yenye uwezo wa kupika kiasi cha kilo moja • Weka mafuta ya kupika kiasi cha vijiko vitatu na acha yapate moto • Weka vitunguu maji, menya nyanya na katakata halafu weeka katika sufuria hiyo. • Weka chumvi na kanga hadi vilainike kabisa • Baada ya kuiva weka vitunguu swaumu na baadaye mchele • Koroga hadi uchanganyike na weka nyama. Endelea kukoroga, baada ya hapo weka maji kiasi cha kuivisha mchele huo. Acha vichemke hadi vikaukie. • Palia mkaa juu yake au kama unatumia jiko la gesi au umeme weka kwenye oven hadi maji yakauke kabisa. • Baada ya hapo chukua hoho na kasha kata upande wa juu kama vifuniko. Kasha ondoa matunda ya ndani yake. Funika na kasha zipange kwenye sufuria yenye maji na chumvi na mafuta kidogo kiasi cha kijiko kimoja. Chemsha jikoni hadi ziive. • Baada ya kuiva, chukua hoho zako na kasha chota wali kw akutumia kijiko kasha jaza katika kila hoho na weka kwenye sahani tayari kwa kuliwa. • Unaweza kupamba na salad ukipenda.
Updated at: 2024-05-25 10:34:42 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Mayai 5
Sukari 450gm (1 lb)
Unga wa Ngano 1 kg
Siagi 450gm (1 lb)
Baking powder ½ Kijiko cha chai
Unga wa Custard Vijiko 2 vya chakula
Karanga za kusaga 250gm
Jam ½ kikombe
MAANDALIZI
Chukua bakuli la kiasi, weka sukari na siagi. Changanya sukari na siagi kwa kutumia mashine ya kukorogea keki (cakemixer), mpaka sukari ichanganyike na siagi. Vunja yai moja moja na weka kiini chake kwenye mchanganyiko wa sukari na siagi, endelea kuchanganya mpaka ichanganyike vizuri. Hifadhi ute wa mayai ndani ya kibakuli. Mimina unga wa ngano ndani ya mchanganyiko wako huku ukichanganya Changanya unga wa custard na baking powder. Tengeneza viduara vidogo vidogo. Vichovye viduara ndani ya ute wa yai kisha zimwagie unga wa karanga na kuzipanga kwenye tray ya kuchomea. Weka dole gumba kati kati ya kila kiduara na uweke jam. Washa jiko (oven) 350F na uchome vileja vyako kwa dakika 20. Toa vileja vyako vipoe na uviweke ndani ya sahani tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:23:14 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Ndizi - 15 takriiban
Nayma ya ng’ombe - 1 kilo
Kitunguu maji - 1
Nyanya - 3
Kitunguu saumu(thomu/galic) kilosagwa - 1 kijiko cha supu
Tangawizi mbichi ilosagwa - 1 kijiko cha supu
Pilipili mbichi ilopondwa - 2
Jira/cummin/bizari ya pilau ilosagwa - 1 kijiko cha chai
Ndimu - 1
Chumvi - kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Chemsha nyama kwa ndimu, chumvi na tangawizi mbichi na kitunguu thomu. Menya ndizi na zikatekate vipande kiasi, weka katika sufuria. Katakata kitunguu na nyanya utie katika ndizi. Tia jira na chumvi. Nyama ikiwiva mimina pamoja na supu yake ufunike ndizi ziwive na kuwa tayari kuliwa. Ukipenda tia pilipili mbuzi zichemke pamoja na ndizi.
Updated at: 2024-05-25 10:34:48 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Leo wapendwa nitaenda kuzungumzia mapishi ya mchuzi wa kuku (chicken curry).
Mahitaji
Kuku mzima Nyanya kubwa 3 Karoti mbili Pilipili hoho Kotmiri Tangawizi Kitunguu maji Kitunguu saumu kidogo Ndimu Mafuta ya kupikia Chumvi (pilipili ukipenda)
Matayarisho
1. Menya vitunguu saumu na tangawizi na uvitwange pamoja. 2. Katakata kuku vipande vidogo kisha ukamulie ndimu na kupaka mchanganyiko wa tangawizi na vitunguu saumu (kiasi tu). 3. Katakata vitunguu maji na pilipili hoho uweke pembeni. 4. Grind (Kwangua) kwenye grater nyanya na karoti pia uweke pembeni. 5.Katakata kotmiri vipande vidogo uweke pembeni. 6. Andaa kikaango na jiko.
Mapishi
1. Bandika kikaango jikoni na mafuta kiasi, yakishachemka weka vitunguu maji na kaanga hadi vimelainika na kuiva (hakikisha haviungui). 2. Weka pilipili hoho na karoti na endelea kukoroga hadi vyote viive na kulainika, Kisha weka chumvi. 3. Sasa weka vipande vya nyama koroga na funikia kwa dakika 3, kisha weka nyanya zako ulizo grind na koroga ili zichanganyike vizuri, vikishachanganyika weka kotmiri na pilipili kama utapenda. Acha vichemke kwa dakika 5. Hakikisha moto sio mkali sana. 4. Angalia kama nyama zimeiva vizuri kisha epua mchuzi wako. 5. Pakua kwenye bakuli na katakata kotmiri uweke kwa juu. Unaweza kula kwa ugali, wali, ndizi rost au chipsi.
Updated at: 2024-05-25 10:23:00 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Unga wa ngano (self risen flour) kikombe 1na 1/2 Sukari (sugar) 1/4 kikombe Barking powder 1/2 kijiko cha chai Magadi soda (bicarbonate soda) 1 kijiko cha chai Mafuta 2 vijiko vya chai Mafuta ya kukaangia Maji ya uvuguvugu kiasi
Matayarisho
Changanya unga na vitu vyote (kasoro mafuta ya kuchomea) kisha ukande (hakikisha unakuwa mgumu) Baada ya hapo sukuma na ukate shape uipendayo (hakikisha unakata vipande vinene kiasi na sio kama mandazi) Baada ya hapo ziweke sehemu yenye joto na uache ziumuke. Zikisha umuka zikaange katika moto mdogo ili ziive mpaka ndani. Zikisha iva zitoe na uziweke katika kitchen towel ili zichuje mafuta. Ziache zipoe na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.
Mapishi ya Wali Wa Tambi Na Kuku Wa Sosi Ya Mtindi
Updated at: 2024-05-25 10:23:13 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo Vya Wali
Mchele - 3 vikombe
Tambi - 2 vikombe
Mafuta - ¼ kikombe
Chumvi
Vipimo Vya Kuku
Kuku kidari (boneless) aliyekatwa katwa vipande - 1 Kilo
Kitunguu maji kilichokatwa katwa - 2
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa - 1 kijiko cha supu
Pilipili mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha chai
Chumvi - kiasi
Paprika - 1 kijiko cha supu
Masala ya kuku (tanduri au yoyote) - 1 kijiko cha supu
Ndimu - 2 vijiko vya supu
Mtindi (yoghurt) au malai (cream) - 1 kikombe
Mafuta - ¼ kikombe
Majani ya kotmiri (coriander) - ½ kikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Wali:
Osha Mchele, uroweke. Tia mafuta katika sufuria, kaanga tambi zilizokatwakatwa hadi zigeuke rangi kuwa nyekundu. Tia mchele endelea kukaanga kidogo. Tia maji kiasi cha wali kupikika kama unavyopika pilau. Kiasi cha maji kinategemea aina ya mchele Funika katika moto mdogo mdogo hadi uive ukiwa tayari.
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Kuku
Katika bakuli, changanya vitu vyote isipokuwa mtindi na kitunguu. Tia mafuta katika karai, kisha tia kitunguu ukaange muda mdogo tu, usikiache kugeuka rangi. Tia kuku na masala yake, endelea kukaanga, kisha tia mtindi au malai ufunike apikike na kuiva vizuri. Nyunyuzia kotmiri iliyokatwakatwa ikiwa tayari kuliwa na wali wa tambi.