Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Tofauti kati ya yai la kuku wa kienyeji na la kuku wa kisasa
Updated at: 2024-05-25 10:34:45 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Kilishe mayai yote ni sawa. Virutubishi vinavyopatikana kwenye yai la kuku wa kienyeji kama protini, vitamini A, madini ya chuma na virutubishi vya aina nyingine, ndivyo hivyo vinavyopatikana pia kwenye yai la kuku wa kisasa.
Tatizo linaweza kutokea pale ambapo wafugaji wa kuku wa kisasa hawafuati taratibu za ufugaji na pengine hawawapi kuku vyakula muhimu wanavyohitaji au wanawapa dawa na vyakula visivyo bora kiafya, hivyo wakati mwingine kiini cha yai la kuku wa kisasa huonekana kupungua rangi ya njano kuliko kiini cha yai la kuku wa kienyeji.
Mtu anashauriwa kula yai bila kujali ni la kuku gani, kwa kutegemea ni yai lipi linapatikana kwa urahisi. Lakini nivizuri kula mayai ambayo yapo salama.
Updated at: 2024-05-25 10:34:38 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Viazi - 3lb
Nyama - 1lb
Kitunguu - 1
Nyanya - 2
Kitunguu saumu(thomu/galic) - 1 kijiko cha chai
Manjano - ½ kijiko cha chai
Curry powder - ½ kijiko chai
Nyanya kopo - 1 kijiko cha chai
Pilipili ya unga - kiasi upendavyo
Chumvi - kiasi
Kidonge cha supu - 1
Tui la nazi - 1 kopoau zaidi
Mtindi ukipenda - 3 vijiko vya supu
Kotmiri - kiasi ya kupambia
Nazi ya unga - 4 vijiko vya supu
Mafuta - 2 vijiko vya supu
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Kata nyama vipande vipande kisha chemsha na chumvi mpaka iive. Menya maganda viazi na ukate slice kubwa weka pembeni Kata kata kitunguu kisha kaanga na mafuta mpaka vibadilike rangi Tia thomu, bizari ya manjano, pilipili ya unga, nyanya kopo Kata kata nyanya nzima vipande vidogo tia na kidonge cha supu. Kisha tia viazi, nyama na tui la nazi finika mpaka viazi viwive lakini visiwe vikavu. Tia mtindi na nazi ya unga kama vijiko 4 vya supu iache motoni kidogo kisha pakua, tupia kotmiri juu na itakuwa tayari kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:22:58 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Unga wa mchele (rice flour 2 vikombe vya chai) Sukari (sugar 3/4 ya kikombe cha chai) Hamira (dried yeast 3/4 kijiko cha chakula) Hiliki (cardamon powder 1/2 kijiko cha chai) Ute wa yai 1(egg white) Tui la nazi (coconut milk kikombe 1 na 1/2 cha chai) Mafuta (vegetable oil)
Matayarisho
Changanya unga wa mchele, hamira, hiliki na tui la nazi pamoja katika bakuli la plastic kisha koroga vizuri. Ufunike na uwache katika sehemu ya joto mpaka uumuke.(ambayo inaweza kuchukua kama dakika 30-45. Ukisha umuka tia sukari na ute wa yai kisha ukoroge vizuri. Baada ya hapo washa oven katika moto wa 200°C kisha chukua chombo cha kuokea na ukipake mafuta na umimine mchanganyiko. Kisha utie katika oven na uoke kwa muda wa dakika 40. Hakikisha unaiva na kuwa rangi yabrown juu na chini. Na hapo mkate utakuwa tayari.
Jinsi ya kuandaa Pilau ya sosi ya soya, nyama na mboga
Updated at: 2024-05-25 10:23:16 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Nyama isiyokuwa na mifupa - 1 ½ Lb(ratili) Mchele wa Basmati (rowanisha) - 3 Magi Vitunguu maji - 2 Mchanganyiko wa mboga za barafu - 1 Magi (karoti, mahindi, njegere) Pilipili Mbichi - 3 Pilipili mboga kijani na nyekundu - 1 Pilipili manga - ½ kijiko cha chai Chumvi - Kiasi Sosi ya soya (soy sauce) - 5 Vijiko vya supu Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa - 1 Kijiko cha supu Mchanganyiko wa bizari (garam masala) - 1 Kijiko cha supu Kotmiri iliyokatwa - ½ Kikombe Mafuta ya kukaangia - Kiasi
Namna Ya Kutaarisha
Ndani ya sufuria, tia mafuta yakipata moto kaanga vitunguu mpaka ziwe rangi ya hudhurungi. Kisha tia nyama iliyokatwa vipande vidogo vidogo pamoja na maji ya kiasi na viungo vyote isipokuwa mchele, mboga zote na kotmiri. chemsha mpaka nyama iwive na maji yakauke. Halafu changanya na mboga na iwache kwa muda wa dakika kumi kisha tia kotmiri na umimine kwenye bakuli au treya ya oveni na uweke kando. Chemsha mchele na chumvi uwive kama kawaida ya kupika wali wa kuchuja, kisha umwagie juu ya ile treya ya nyama. Nyunyizia mafuta na sosi ya soya na ipike katika oveni moto wa 350° kwa muda wa dakika 20 hivi. Ukishawiva, uchanganye ukiwa tayari kwa kuliwa
Updated at: 2024-05-25 10:37:40 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Tambi (spaghetti 1/2 ya packet) Mafuta (vegetable oil) Sukari (sugar 1/2 kikombe cha chai) Hiliki (cardamon 1/2 kijiko cha chai) Chumvi (salt 1/2 kijiko cha chai) Tui la nazi (coconut oil 1 kikombe cha chai) Maji kiasi
Matayarisho
Tia mafuta kiasi kwenye sufuria kisha ibandike jikoni (katika moto wa wastani) yakisha pata moto kiasi tia tambi na uanze kuzikaanga kwa kuzigeuzageuza kila mara mpaka zitakapokuwa za yangi ya light brown. baada ya hapo ipua na umwage mafuta ya kwenye tambi (bakiza kidogo sana kwani usipofanya hivyo tambi zitakuwa na mafuta sana) Baada ya hapo zirudishe jikoni na kisha utie hiliki, chumvi, sukari, tui la nazi na maji kiasi. Zifunike kisha ziache zichemke mpaka maji yakauke. Baada ya hapo zigeuze na uzipike mpaka ziive. Nahapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:43 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele 2 vikombe vya chai Choroko kikombe 1 na 1/2 Nazi kopo 1 Swaum 1 kijiko cha chakula Kitunguu 1 kikubwa Binzari nyembamba 1 kijiko cha chai Chumvi Mafuta
Matayarisho
Loweka choroko usiku mzima, pindi ukianza kupika loweka mchele nusu saa kisha katika sufuria kubwa, kaanga vitunguu vikianza kuwa vya brown tia swaum na binzari nyembamba kisha tia choroko, mchele, chumvi,nazi na maji mengi kiasi yakuivisha choroko pamoja na mchele. Pika mpaka vitu vyote viive na viwe vilaini kisha upondeponde kiasi.Baada ya mseto wako kuiva utakuwa unaonekana kama uji wa mchele vile. Na Baada ya hapo mseto wako utakuwa tayari kwa kuliwa na mboga yoyote uipendayo.Inapendeza zaidi kuliwa vile tu ukishamalizwa kupikwa
Updated at: 2024-05-25 10:23:14 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo Vya Wali
Mchele wa Basmati/Pishori - 1 kilo moja
Vitunguu maji - 3
Karoti - 2
Siagi - 3 vijiko vya supu
Kidonge cha supu (stock) - 1 kimoja
Chumvi - kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Ósha mchele uroweke kama saa moja au mbili Katakata vitunguu vipande vidogodogo (chopped) weka kando. Kwaruza karoti (grate) weka kando. Tia siagi katika sufuria ya kupikia wali, weka katika moto iyayuke Kaanga vitunguu hadi vigeuke rangi kiasi tu. Tia maji kiasi ya kupikia wali, changanya na kidonge cha supu. Yakichemka tia mchele, koroga, funika uweke moto mdogo mdogo. Kabla ya maji kukauka tia karoti changanya wali kisha funika uive kama unavyopika pilau.
Vipimo Vya Kuku Wa Kukaanga
Kuku alokatwakatwa - 1
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi ilosagwa - 2 vijiko vya supu
Bizari ya mchanganyiko/garam masala - kijiko cha supu
Mtindi/Yoghurt - 1 kijiko cha supu
Ndimu - 1
Chumvi - kiasi
Mafuta ya kukaangia - kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Ukishamuosha kuku, mchuje atoke maji yote. Changanya viungo vyote katika kibakuli kidogo. Changanya pamoja na kuku kisha acha akolee viungo (marinate) kwa muda wa masaa mawili takriban. Weka mafuta katika karai na kaanga kuku, akiwiva yu tayari kuliwa na wali.
Updated at: 2024-05-25 10:23:11 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI VYA TUNA
Tuna (samaki/jodari) - 2 Vikopo
Vitunguu (kata kata) - 4
Nyanya zilizosagwa - 5
Nyanya kopo - 3 Vijiko vya supu
Viazi (vilivyokatwa vipande vidogo - cubes) - 4
Dengu (chick peas) - 1 kikombe
Kitunguu saumu(thomu/galic)&Tangawizi iliyosagwa 1 Kijiko cha supu
Hiliki - 1/4 kijiko cha chai
Mchanganyiko wa bizari - 1 kijiko cha supu
Chumvi - kiasi
Pilipili manga - 1 Kijiko cha chai
Vipande cha Maggi (Cube) - 2
VIAMBAUPISHI VYA WALI
Mchele - 3 Vikombe vikubwa (Mugs)
Mdalasini - 2 Vijiti
Karafuu - chembe 5
Zaafarani - kiasi Jirsh (Komamanga kavu au zabibu kavu -raisins) - 1/2 Kikombe
JINSI YA KUANDAA
Kosha Mchele na roweka. Kaanga vitunguu hadi viwe rangi ya hudhurungi (brown) chuja mafuta uweke kando. Kaanga viazi, epua Punguza mafuta, kaanga nyanya. Tia thomu/tangawizi, bizari zote, vipande vya Maggi, nyanya kopo, chumvi. Mwaga maji ya tuna iwe kavu, changanyisha kwenye sosi. Tia zaafarani kidogo katika sosi na bakisha ya wali. Chemsha mchele pamoja na mdalasini na karafuu. Karibu na kuwiva, chuja maji utie katika chombo cha kupikia katika jiko (oven) Nyunyizia zaafarani, mwagia vitunguu, viazi, na dengu juu ya wali. Mwagia sosi ya tuna na pambia jirshi (au zabibu). Funika wali na upike katika jiko moto wa 450º kwa muda wa kupikika wali. Epua upakue.