Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-25 10:34:51 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Unga 1 Magi (vikombe vya chai)
Sukari ya browni ½ Magi
Siagi iliyoyayushwa 125 g
Nazi iliyokunwa ½ Magi
Mjazo wa karameli (Caramel filling)
Syrup 1/3 kikombe cha chai
Siagi iliyoyayushwa 125 g
Maziwa matamu ya mgando 2 vikopo (condensed milk)
Mjazo wa chokoleti (Chocolate filling)
Chokoleti 185 g (dark chocolate)
Mafuta 3 Vijiko vya chai
Jinsi ya kuandaa na kupika
1. Changanya unga, sukari, siagi na nazi iliyokunwa kwenye bakuli mpaka unga ushikamane.
2. Paka mafuta treya ya kuchomea kisha utandaze kwenye treya ya 20cm kwa 30 cm au (8 in kwa 12 in) unaweza kuweka karatasi ya kuchomea chini ukipenda.
3. Choma kwenye moto 325˚C kwa muda wa dakika 15 mpaka 18 au mpaka ibadilike kuwa rangi ya browni.
4. Kwenye sufuria ndogo tia syrup siagi na maziwa matamu ya mgando na changanya kwa moto mdogo mpaka uwe mzito kasha mimina juu ya keki uliyochoma na choma tena kwa muda wa dakika 20 mpaka karameli iwe rangi ya dhahabu.
5. Kwenye sufuria ndogo nyingine tia vipande vya chokoleti na mafuta na ukoroge kwa moto mdogo mpaka iyayuke kisha wacha ipoe kidogo mimina juu ya mjazo wa karameli kisha weka kwenye friji mpaka ishikamane.
6. Kata vipande weka kwenye sahani tiyari kwa kuliwa
Jinsi ya kutengeneza Slesi Za Chokoleti Na Karameli
Updated at: 2024-05-25 10:34:41 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga - 1 Magi (vikombe vya chai)
Sukari ya browni - ½ Magi
Siagi iliyoyayushwa - 125 g
Nazi iliyokunwa - ½ Magi
MJAZO WA KARMEL (Caramel filling)
Syrup - 1/3 kikombe cha chai
Siagi iliyoyayushwa - 125 g
Maziwa matamu ya mgando - 2 vikopo (condensed milk)
MJAZO WA CHOKOLETI (Chocolate filling)
Chokoleti - 185 g (dark chocolate)
Mafuta - 3 Vijiko vya chai
MAANDALIZI
Changanya unga, sukari, siagi na nazi iliyokunwa kwenye bakuli mpaka unga ushikamane. Paka mafuta treya ya kuchomea kisha utandaze kwenye treya ya 20cm kwa 30 cm au (8 in kwa 12 in) unaweza kuweka karatasi ya kuchomea chini ukipenda. Choma kwenye moto 325˚C kwa muda wa dakika 15 mpaka 18 au mpaka ibadilike kuwa rangi ya browni. Kwenye sufuria ndogo tia syrup siagi na maziwa matamu ya mgando na changanya kwa moto mdogo mpaka uwe mzito kasha mimina juu ya keki uliyochoma na choma tena kwa muda wa dakika 20 mpaka karameli iwe rangi ya dhahabu. Kwenye sufuria ndogo nyingine tia vipande vya chokoleti na mafuta na ukoroge kwa moto mdogo mpaka iyayuke kisha wacha ipoe kidogo mimina juu ya mjazo wa karameli kisha weka kwenye friji mpaka ishikamane. Kata vipande weka kwenye sahani tiyari kwa kuliwa
• Chambua mnavu, osha na katakata. • Menya, osha na katakata kitunguu. • Osha, menya na kwaruza karoti. • Kaanga karanga, ondoa maganda na saga zilainike. • Kaanga vitunguu na karoti mpaka zilainike ukikoroga. • Weka mnavu na chumvi koroga sawa sawa, funika kwa dakika 5-10 (kama ni kavu weak maji kidogo). • Changanya maziwa na karanga, ongeza kwenye mnavu ukikoroga kisha punguza moto kwa dakika 5. • Onja chumvi na pakua kama kitoweo. Uwezekano Weka nyanya kidogo. Tumia tui la nazi au krimu badala ya maziwa. Weka nyama au dagaa au Mayai badala ya Karanga.
Updated at: 2024-05-25 10:37:44 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Pilipili hoho (Red pepper 3) Cougette 1 Kitunguu (onion 1) Uyoga (mashroom 1 kikombe cha chai) Carrot 1 Nyanya (fresh tomato 1) Nyanya ya kopo iliyosagwa (tomato paste 3 vijiko vya chai) Giligilani (fresh coriander) Binzari manjano (Turmaric 1/2 ya kijiko cha chai) Curry powder 1/2 ya kijiko cha chai Chumvi (salt) Mafuta (vegetable oil)
Matayarisho
Kata hoho kati na utoe moyo wake kisha ziweke pembeni, Kisha katakata cougette, kitunguu, uyoga, carrot, nyanya katika vipande vidogo vidogo, Weka sufuria jikoni na uanze kupika uyoga kwa muda wa dakika 5, kisha weka curry powder, turmaric na chumvi na kaanga kidogo kisha weka vegetable zilizobakia pamoja na nyanya ya kusaga pamoja na giligilani. Zikaange kwa muda wa dakika 5 kisha zitie kwenye hoho na kisha uzibake kwa muda wa dakika 20 na hapo zitakuwa tayari kuseviwa na wali. Wali: angalia katika recipe zilizopita
1) Weka karai kwenye moto kiasi
2) Tia siagi
3) Tia tambi uzikaange usiachie mkoni mpaka ziwe rangu ya dhahabu.
4) Weka lozi na zabibu huku unakoroga
5) Tia maziwa na huku unakoroga usiachie mkono.
6) Tia arki
7) Epua karai, tumia kijiko cha chai kwa kuchotea na utie kwenye kikombe cha kahawa nusu usikijaze.
8) Kipindue kwenye sahani utoe kileja.
9) Fanya hivyo mpaka umalize vyote.
Updated at: 2024-05-25 10:37:41 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Kambale 2 Nazi kopo 1 Nyanya kopo 1 Vitunguu 2 Curry powder 1 kijiko cha chai Turmaric 1/2 kijiko cha chai Binzari nyembamba ya unga 1/2 kijiko cha chai Swaum/ tangawizi 1 kijiko cha chakula Giligilani kiasi Limao 1/2 Chumvi Olive oil
Matayarisho
Loweka samaki katika maji ya moto kwa muda wa muda wa nusu saa.Baada ya hapo Saga pamoja nyanya, vitunguu, swaum na tangawizi kisha vibandike jikoni na uvipike mpaka maji yote yakauke kisha tia mafuta. Pika mpaka nyanya zitengane na mafuta kisha tia spice zote.Zipike kwa muda mdogo kisha tia tui la nazi, maji kiasi, samaki, pilipili nzima, chumvi na kamulia limao. Pika mpaka tui la nazi litakapoiva na samaki pia wawe wameiva na mchuzi ubakie kiasi. Baada ya hapo ipua kisha tia giligilani iliyokatwa na mchuzi utakuwa tayari kwa kuliwa. Unaweza kuulia kwa chochote kile upendacho. Mi hupendaga kuulia na ugali mlaiiini au na wali pia.
Updated at: 2024-05-25 10:23:12 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viambaupishi Vya Masala
Nyama vipande - 3 LB
Mtindi - ½ kopo
Kitunguu (thomu/galic) - 1½ kijiko cha supu
Tangawizi - 1½ kijiko cha supu
Nyanya - 2
Pilipili mbichi - kiasi
Nyanya kopo - 4 vijiko vya supu
Vidonge supu - 2
Pilipili nyekundu paprika - kiasi
Bizari zote saga - 2 vijiko vya supu
Viazi - 4
Mafuta - 2 mug
Samli - ½ kikombe
Vitungu - 6
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika masala
Kwenye sufuria tia nyama, saga nyanya na thomu, pilipili mbichi, tangawizi. Mimina kwenye nyama na mtindi, tia na nyanya kopo, bizari paprika, vidonge vya supu, chumvi kisha changanya vyote pamoja weka motoni. Katika sufuria nyengine tia mafuta na samli kaanga vitungu mpaka viwe rangi ya hudhurungi toa weka pembeni. Kanga viazi weka pembeni. Chukua mafuta kidogo uliyokangia tia kwenye nyama acha katika moto wa kiasi mpaka nyama iwive na maji ya punguke. Tia viazi na vitunguu vivunje vunje tia ndani ya nyama acha moto mdogo.
Vipimo Vya Wali
Mchele - 5 mug
Maji - kiasi
Chumvi - kiasi
Mafuta uliyokaanga vitungu - kiasi
Rangi ya biriani - ¼ kijiko cha chai
*Zafarani - ½ kijiko cha chai
*roweka rangi na zafarani
Namna Ya Kutarisha Na Kupika Wali
Osha mchele roweka muda wa saa. Chemsha maji kama magi 10 hivi na chumvi tia mchele. Uache uchemke ukishaiva kiini nusu, mwaga maji chuja. Mimina juu ya nyama tia rangi na mafuta kwa juu funika. Aacha kidogo katika oveni kwa muda wa dakika 20 hivi kisha epua ikiwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:34:47 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Wali wa hoho ni chakula maalum kinachotumika katika hafla au sherehe. Ni chakula chenye ladha nzuri na kina muonekano wa kuvutia kinapokuwa mezani tayari kwa kuliwa.
Mara nyingi huandaliwa kama zawadi katika harusi hususan kwa watu wa pwani. Kwa kuwa zawadi hiyo au maarufu kama kombe huwa kuna vyakula vingi, ikiwamo chakula hiki ambacho hufanya kombe kuwa na muonekano wa kupendeza.
Mbali na kuliwa kama kombe chakula hiki kinaweza kuandaliwa kama mlo wa usiku.
Mahitaji:
• Mchele ½ kg • Nyanya 3 • Mafuta ya kupika ¼ kikombe cha chai • Chumvi kiasi • Kitunguu swaumu kilichosagwa kijiko 1 cha mezani • Kitunguu maji kilichosagwa kijiko 1 cha mezani • Hoho 4 • Nyama ya kusaga ¼ • Tangawizi kijiko 1 cha chakula • Limao au ndimu kipande
Maadalizi:
• Chukua mchele uoshe vizuri kasha chuja maji • Chukua nyama ya kusaga na kamulia ndimu, weka chumvi na tangawizi, changanya vizuri na weka jikoni.iache ichemke hadi ikauke maji yote. • Chukua maji na kiasi cha robo tatu lita chemsha na weka pembeni • Chukua sufuria kavu yenye uwezo wa kupika kiasi cha kilo moja • Weka mafuta ya kupika kiasi cha vijiko vitatu na acha yapate moto • Weka vitunguu maji, menya nyanya na katakata halafu weeka katika sufuria hiyo. • Weka chumvi na kanga hadi vilainike kabisa • Baada ya kuiva weka vitunguu swaumu na baadaye mchele • Koroga hadi uchanganyike na weka nyama. Endelea kukoroga, baada ya hapo weka maji kiasi cha kuivisha mchele huo. Acha vichemke hadi vikaukie. • Palia mkaa juu yake au kama unatumia jiko la gesi au umeme weka kwenye oven hadi maji yakauke kabisa. • Baada ya hapo chukua hoho na kasha kata upande wa juu kama vifuniko. Kasha ondoa matunda ya ndani yake. Funika na kasha zipange kwenye sufuria yenye maji na chumvi na mafuta kidogo kiasi cha kijiko kimoja. Chemsha jikoni hadi ziive. • Baada ya kuiva, chukua hoho zako na kasha chota wali kw akutumia kijiko kasha jaza katika kila hoho na weka kwenye sahani tayari kwa kuliwa. • Unaweza kupamba na salad ukipenda.
Updated at: 2024-05-25 10:37:40 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Viazi ulaya 4 vya wastani Hoho jekundu 1/2 Hoho la njano 1/2 Hoho la kiajani 1/2 Njegere 1 kikombe cha chai Carrot 1 kubwa Broccoli kidogo Cauliflower kidogo Kitunguu 1 Nyanya 1/2 kopo Swaum/tangawizi 1 kijiko cha chakula Curry power 1 kijiko cha chakula Coriander powder 1 kijiko cha chai Tarmaric 1/2 kijiko cha chai Olive oil Chumvi 1/4 ya limao
Matayarisho
Katika sufuria isiyoshika chini kaanga vitunguu mpaka viwe vya brown kisha tia swaum/tangawizi na spice zote kaanga kwa muda mfupi kisha tia nyanya na chumvi. pika mpaka nyanya ziive kisha tia vegetable zote na vimaji kidogo sana na kisha kamulia limao, baada ya hapo punguza moto na kisha funika na zipike mpaka vegetable zote ziive na rojo ibakie kidogo. Baada ya hapo mboga yako itakuwa tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:48 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Bilinganya 2 za wastani Nyanya kubwa 1 Kitunguu maji 1 kikubwa Swaum 1/2 kijiko cha chai Limao 1/4 Pilipili ya unga 1/2 kijiko cha chai Parpika 1/4 kijiko cha chai Pilipili mtama 1/4 kijiko cha chai Curry powder1/4 kijiko cha chai Chumvi kiasi Coriander Olive oil
Matayarisho
Katakata bilinganya slice nyembamba kisha ziweke pembeni. Baada ya hapo kaanga kitunguu maji mpaka kiwe cha brown kisha tia swaum na spice zote, zikaange kidogo kisha tia nyanya na chumvi kiasi. Pika nyanya mpaka iive na itengane na mafuta. Baada ya hapo tia mabilinganya na ukamulie limao kisha punguza moto na uyafunike na mfuniko usioruhusu kutoa mvuke ili yaivie na huo mvuke. Baada ya hapo yaonje kama yameiva na malizia kwa kutia fresh coriander na baada ya hapo yatakuwa tayari kwa kuliwa. kwa kawaida mi hupendaga kuyalia na wali na maharage badala ya kachumari kwahiyo nakuwa naitumia hiyo kama kachumbari