Log in to access your menu with tools for managing π tasks, π₯ clients, π° finances, π learning, π personal growth, and π spirituality, all in one place!.
eBooks: Sala za Katoliki: Sala Muhimu Kwa Mkristu Mkatoliki - Topic 3 - AckySHINE
Matendo ya Rozari Takatifu: Mchanganuo kwa siku zote za Saba za Juma
π β
Available in PDF
Updated at: 2024-05-27 07:13:41 (11 months ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)
Tendo la kwanza; Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.
Tendo la pili; Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti. Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.
Tendo la tatu; Yesu anazaliwa Betlehemu. Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara
Updated at: 2024-05-27 07:14:26 (11 months ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Malaika wa Mungu Mlinzi wangu mpenzi, Ambaye upendo wake unanifanya niwepo hapa, Uwe nami leo hii, Kuniangaza na kunilinda, Kunitawala na kuniongoza. Amina.
Updated at: 2024-05-27 07:13:46 (11 months ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Mungu wangu, nasadiki maneno yote linalosadiki na linalofundisha kanisa katoliki la Roma; Kwani ndiwe uliyefundisha hayo, wala hudanganyiki, wala hudanganyi. Amina
Updated at: 2024-05-27 07:14:28 (11 months ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Tumia tasbihi ya kawaida yenye chembe ndogo 53.
Kwenye Msalaba Sali:
βEe Yesu tupe moyo wako kama amana ya upendo wako na kimbilio letu, ili tupate pumziko salama wakati wa maisha yetu na faraja tamu saa ya kufa kwetuβ. Baba Yetu β¦β¦.. Salamu Maria β¦β¦. (mara tatu) Nasadiki β¦β¦β¦..
Updated at: 2024-05-27 07:14:05 (11 months ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Novena ya Noeli (maarufu kama novena ya Mt. Andrea)
Husaliwa kuanzia tar 30 Nov hadi usiku wa Noeli, tar 24 Disemba. Inajulikana kama novena ya Mt. Andrea kwa sababu novena hii huanza kusaliwa katika siku ya kumbukumbu ya Mt. Andrea Mtume.
Updated at: 2024-05-27 07:14:08 (11 months ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Ee Mungu Mwenyezi wa milele, mpaji wa mema yote, unayetusamehe na kutulinda. Utujalie sisi tunaokusihi, tufurahie hali njema ya hewa na mvua tunayoitamani na kuhitaji. Tutumie daima vipawa vya wema wako kwa ajili ya utukufu wa jina lako, na kwa ajili ya wokovu watu. Tunaomba hayo kwa njia ya Bwana
Updated at: 2024-05-27 07:13:45 (11 months ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Ee Mtakatifu Teresia wa mtoto Yesu, ulistahili kuitwa Msimamizi wa misioni katoliki za dunia yote. Kumbuka ile tamaa yako kuu uliyoonyesha huku duniani ya " kusimika Msalaba wa Yesu Kristu, katika nchi zote na kuhubiri Injili mpaka mwisho wa dunia"
Updated at: 2024-05-27 07:14:10 (11 months ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Kumheshimu Mungu wangu, Namtolea roho yangu, Nifanye kazi nipumzike, Amri zake tu nishike, Wazo neno tendo lote, Namtolea Mungu pote, Roho, mwili chote changu, pendo na uzima wangu, Mungu wangu nitampenda, Wala dhambi sitatenda, Jina lako nasifia, Utakalo hutimia, Kwa utii navumilia, Teso na matata pia, Nipe Bwana neema zako, Niongezee sifa yako, Amina.
Updated at: 2024-05-27 07:13:54 (11 months ago by DIN - Melkisedeck Leon Shine)
Ee uliye Mkuu, Mt. Yosefu, uliyatii kabisa maongozi ya Roho Mt. Unijalie neema ya kufahamu aina ya maisha ambayo Mungu anapenda mimi niishi. Usiniache nidanganyike katika jambo muhimu kama hili, ambalo furaha yangu hapa duniani inalitegemea, na hata pia wokovu wa roho yangu.