Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Sala za kuheshimu Damu Takatifu ya Yesu

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Tusali kila siku sala hizi, angalau kwa mwezi wa saba (Julai) kila mwaka, mwezi wa kuheshimu Damu Takatifu ya Mkombozi wetu.

Yesu alimwahidi Mt. Brigita wa Sweden kwamba wale watakaosali Baba Yetu 7 na Salamu Maria 7 kwa miaka 12 kwa kuheshimu damu yake takatifu na kutafakari juu ya Kutahiriwa kwake, jasho lake la damu, kupigwa kwake mijeledi, kuvikwa taji la miiba, kuchukua kwake Msalaba, kusuliwa kwake na kuchomwa ubavuni; watapata neema 5 zifuatazo: (1) Hawataingia toharani, (2) Yesu atawapa cheo cha mashahidi waliomwaga damu yao kwa ajili ya imani, (3) Yesu atawadumisha jamaa zake watatu katika hali ya neema, (4) Roho za jamaa zake zitakingwa na Jehanam mpaka kizazi cha nne, (5) Mwezi kabla ya kufa, Yesu atawajulisha. Wakifa kabla ya kutimiza miaka ile, watahesabiwa wamemaliza.

Ee Yesu, sasa ninataka kusali Baba yetu mara saba nikiungana na ule upendo ambao kwao uliitakasa sala hii katika Moyo wako. Uichukue kutoka mdomoni mwangu hadi moyoni mwako. Uiboreshe na kuikamilisha hivyo kwamba iupatie heshima na furaha kwa Utatu Mtakatifu kama vile Wewe ulivyoupatia kupitia sala hii wakati ulipokuwa bado hapa duniani. Utukuzwe ee Yesu, itukuzwe Damu Yako Takatifu sana uliyoimwaga kutoka katika Majeraha Yako Matakatifu.

1. Yesu anatahiriwa.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea Majeraha ya kwanza, maumivu ya kwanza na Damu ya kwanza aliyomwaga Mwanao mpenzi, Bwana wetu Yesu Kristu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu na dhambi za dunia nzima, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi ya kwanza ya mauti, hasa kati ya ndugu zangu.

2. Yesu anatokwa Jasho la Damu bustanini Gethsemane.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea mateso na mahangaiko makali sana ya moyoni, ya Bwana wetu Yesu Kristu katika mlima wa mizeituni na kila tone la jasho lake la damu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za kimoyomoyo, na dhambi za namna hiyo zinazotendwa na dunia nzima, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za moyoni na kwa ajili ya kueneza upendo wa kiMungu na wa kindugu.

3. Yesu anapigwa mijeledi.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea majeraha elfu elfu aliyopata, maumivu makali sana na Damu Takatifu sana aliyomwaga, alipopigwa mijeledi, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za tamaa ya mwili, kwa malipizi ya dhambi za tamaa ya mwili za wanadamu wote, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za tamaa ya mwili, na kwa kulinda usafi wa moyo, hasa kati ya ndugu zangu.

4. Yesu anavikwa taji la miiba.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea majeraha, maumivu na Damu Takatifu kutoka katika Kichwa Kitakatifu cha Yesu wakati alipovikwa taji la miiba, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za rohoni, kwa malipizi ya dhambi za rohoni za wanadamu wote, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za rohoni, na kwa ajili ya kueneza Ufalme wa Kristu hapa duniani.

5. Yesu anachukua Msalaba.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea mateso ya njia ya Msalaba, hasa donda lake la begani na Damu Takatifu iliyomwagika, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za ukaidi dhidi ya msalaba, na dhambi za ukaidi dhidi ya msalaba za wanadamu wote, malalamiko yote dhidi ya mipango yako mitakatifu na dhambi zote za ulimi, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za ulimi na kwa ajili ya upendo wa kweli kwa Msalaba.

6. Yesu anasulibiwa.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea Mwanao Msalabani, kupigwa kwake misumari na kuinuliwa kwake, madonda yake mikononi na miguuni na mifereji mitatu ya Damu yake Takatifu iliyomwagika kutoka katika majeraha haya, mateso yake makali sana ya mwili na roho, kifo chake kitakatifu, ukumbusho usio wa kumwaga wa damu wa kifo hiki katika Misa zote Takatifu ulimwenguni, kwa ajili ya majeraha yote yanayosababishwa na ukaidi wa nadhiri na kanuni katika madaraja matakatifu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu zote na za ulimwenguni mzima, kwa ajili ya wagonjwa na wanaokufa, kwa ajili ya mapadre watakatifu na walei, kwa ajili ya nia za Baba Mtakatifu za kukarabati familia za kikristu, kwa ajili ya kuimarika kwa imani ya kikristu ulimwenguni, kwa ajili ya nchi yetu na muungano kati ya mataifa ndani ya Kristu na Kanisa lake, na kwa ajili ya wokovu wa dunia nzima.

7. Yesu anachomwa kwa mkuki moyoni.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, ukubali kupokea, kwa ajili ya mahitaji ya Kanisa Takatifu na kwa ajili ya malipizi ya dhambi za wanadamu wote, Damu na Maji Takatifu vilivyomwagika kutoka jeraha la Moyo Mtakatifu wa Yesu. Utuhurumie. Damu Takatifu ya Yesu, tone lile la mwisho lililomwagika kutoka katika Moyo wake Mtakatifu, unioshe mimi na wengine wote dhambi zetu zote! Ee Maji kutoka katika Moyo Mtakatifu wa Yesu, unioshe na adhabu zote za dhambi zangu na uizime miale ya moto wa toharani kwa ajili yangu na kwa ajili ya roho zote zilizomo toharani. Amina.

Katika mwaka wa Kanisa wa kiliturjia, mwezi Julai ni wa kuiheshimu Damu Takatifu ya Yesu.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Janet Wambura Guest Jun 20, 2024
πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo
πŸ‘₯ Elizabeth Mrema Guest Jun 10, 2024
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Monica Nyalandu Guest Apr 21, 2024
πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe
πŸ‘₯ Paul Kamau Guest Mar 18, 2024
πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani
πŸ‘₯ Rose Amukowa Guest Mar 7, 2024
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Alice Mrema Guest Dec 21, 2023
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Joyce Mussa Guest Dec 9, 2023
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ James Mduma Guest Nov 19, 2023
πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote
πŸ‘₯ Stephen Kikwete Guest Jun 16, 2023
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Rose Mwinuka Guest Apr 19, 2023
πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani
πŸ‘₯ Wilson Ombati Guest Feb 23, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Thomas Mtaki Guest Jan 3, 2023
πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu
πŸ‘₯ Francis Mrope Guest Dec 27, 2022
πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu
πŸ‘₯ Mariam Kawawa Guest Dec 25, 2022
πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana
πŸ‘₯ Dorothy Nkya Guest Dec 20, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Robert Ndunguru Guest Nov 26, 2022
πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka
πŸ‘₯ Stephen Kikwete Guest Nov 2, 2022
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest Oct 29, 2022
πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai
πŸ‘₯ Faith Kariuki Guest Oct 1, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Robert Ndunguru Guest Aug 13, 2022
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ David Nyerere Guest Jul 25, 2022
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ George Tenga Guest Jul 5, 2022
πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe
πŸ‘₯ Betty Cheruiyot Guest Apr 28, 2022
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Raphael Okoth Guest Apr 21, 2022
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Benjamin Kibicho Guest Feb 10, 2022
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Stephen Kikwete Guest Jan 14, 2022
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Peter Mbise Guest Jan 8, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Lucy Kimotho Guest Oct 15, 2021
Amina
πŸ‘₯ Nancy Kawawa Guest Sep 15, 2021
πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
πŸ‘₯ John Malisa Guest Aug 25, 2021
πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu
πŸ‘₯ Susan Wangari Guest Jul 1, 2021
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Stephen Amollo Guest Apr 29, 2021
πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
πŸ‘₯ Linda Karimi Guest Apr 14, 2021
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Wilson Ombati Guest Mar 8, 2021
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Joyce Aoko Guest Feb 19, 2021
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest Jan 18, 2021
πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
πŸ‘₯ Lucy Wangui Guest Aug 18, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Chris Okello Guest Jul 26, 2020
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Anna Malela Guest Jul 3, 2020
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Peter Mbise Guest Jun 4, 2020
πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri
πŸ‘₯ Stephen Amollo Guest Apr 7, 2020
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Grace Minja Guest Mar 23, 2020
πŸ™β€οΈ Mungu akubariki
πŸ‘₯ David Chacha Guest Nov 26, 2019
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Tabitha Okumu Guest Aug 9, 2019
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Lydia Wanyama Guest Jul 20, 2019
πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema
πŸ‘₯ Andrew Odhiambo Guest Jul 9, 2019
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Edward Lowassa Guest Apr 28, 2019
πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi
πŸ‘₯ Patrick Mutua Guest Apr 6, 2019
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Mariam Hassan Guest Feb 11, 2019
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Andrew Mchome Guest Dec 25, 2018
πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose
πŸ‘₯ Patrick Akech Guest Dec 20, 2018
πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
πŸ‘₯ Grace Wairimu Guest Nov 28, 2018
πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu
πŸ‘₯ Carol Nyakio Guest Nov 15, 2018
πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha
πŸ‘₯ Mary Njeri Guest Oct 25, 2018
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Anna Malela Guest Oct 23, 2018
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Victor Kamau Guest Oct 9, 2018
πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie
πŸ‘₯ Rose Waithera Guest Sep 30, 2018
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Catherine Mkumbo Guest Sep 24, 2018
πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua
πŸ‘₯ Patrick Kidata Guest Aug 16, 2018
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Peter Mugendi Guest Aug 14, 2018
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About