Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

SALA MUHIMU ZA MKRISTO ZA KILA SIKU ASUBUHI

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SALA YA ASUBUHI

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, milele na milele, Amina.

Ee Utatu Mtakatifu wa Mwenyezi Mungu, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, nasadiki kuwa upo hapa na mahali pote. Ee Mungu wangu, umeniumba, umenikomboa, umenifanya mkristo, umenizidishia neema zako hapa duniani, umenitayarishia makao yangu mbinguni, umenijalia na siku hii nikutumikie. Ee Mungu wangu! Nakuabudu, nakushukuru, nakuomba toba, nakupenda! Ee Mungu wangu, nakutolea roho yangu, na mawazo, na maneno, na kazi, na furaha, na mateso yangu: uyapokee unipe neema yako nisikutende leo dhambi!

Majitoleo ya Asubuhi

Ee Baba yetu Mungu Mkuu, Umenilinda usiku huu, Ninakushukuru kwa moyo, Ee Baba, Mwana na Roho, Nilinde tena siku hii, Niache dhambi nikutii, Naomba sana Baba wee, Baraka yako nipokee, Bikira safi ee Maria, Nisipotee unisimamie, Mlinzi Mkuu Malaika wee, Kwa Mungu wetu niombee, Nitake nitende mema tu, Na mwisho nije kwake juu, Amina.

Kuweka nia njema

Kumheshimu Mungu wangu, Namtolea roho yangu, Nifanye kazi nipumzike, Amri zake tu nishike, Wazo neno tendo lote, Namtolea Mungu pote, Roho, mwili chote changu, pendo na uzima wangu, Mungu wangu nitampenda, Wala dhambi sitatenda, Jina lako nasifia, Utakalo hutimia, Kwa utii navumilia, Teso na matata pia, Nipe Bwana neema zako, Niongezee sifa yako, Amina.

Majitoleo

Ee Yesu, kupitia mikono safi ya Bikira Maria, na kwa maungano na sadaka yako kuu, ninakutolea sala, matendo, kazi, masumbuko, na furaha zangu zote za siku hii ya leo, kwa ajili ya nia za Moyo wako Mtakatifu, Ee Yesu ufalme wako utufikie!

Baba Yetu….
Salamu Maria, …..
Nasadiki …….
Amri za Mungu ……
Amri za Kanisa ……

Sala ya Malaika wa Bwana

Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria, naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Salamu Maria,….

Ndimi Mtumishi wa Bwana, nitendewe ulivyonena. Salamu Maria, ……
Neno wa Bwana akatwaa Mwili, akakaa kwetu. Salamu Maria, …..

Utuombee, ee Mzazi Mtakatifu wa Mungu, tujaliwe ahadi za Kristo.

Tuombe:

Tunakuomba ee Bwana, utie neema yako mioyoni mwetu, ili sisi tuliojua kwa maelezo ya Malaika, kwamba, Kristo Mwanao amejifanya mtu: kwa mateso na Msalaba wake, utufikishe kwenye utukufu wa ufufuko. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu, Amina.

Sala kwa Malaika Mlinzi

Ee Malaika wangu, uliyewekwa na Mungu mwema unilinde, naomba uniongoze leo, unitunze, unisimamie, unishauri. Amina.

Sala kwa wenye kuzimia

Ee Yesu mwenye huruma, mpenda roho za watu, nakuomba kwa ajili ya kuzimia kwa Moyo wako Mtakatifu, na kwa ajili ya Mama Yako asiye na doa, uwatakase kwa damu yako, watu wote wenye dhambi wanaokufa sasa, na watakaokufa leo.
Moyo wa Yesu uliozomia, uwahurumie watu wanaokufa X3.

Sala kwa Mtakatifu Yosef

Ee Yosef mwenye heri, tunakimbilia kwako, katika masumbuko yetu, na kishaomba shime ya Mchumba wako Mtakatifu, tunaomba pia kwa matumaini usimamizi wako. Kwa ajili ya mapendo uliyompenda nayo Bikira Mtakatifu, Mzazi wa Mungu, na kwa ajili ya tunza ya Baba, uliyomtunza nayo Mtoto Yesu, tunakuomba sana, utuangalie kwa wema, sisi tuliokuwa fungu lake Yesu Kristo, tuliokombolewa kwa damu yake, utusimamie katika masumbuko yetu, kwa enzi na shime yako.
Ee Mlinzi amini wa Jamaa Takatifu, uwakinge watoto wateule wa Yesu Kristo, ee Baba uliyetupenda mno, utuepusha na kilema chochote cha madanganyo na upotevu. Ee kinga yetu mwezaji,utusimamie huko juu mbinguni ulipo, tunaposhindana na wenye nguvu wakaao gizani. Kama vile siku za kale ukamwokoa Mtoto Yesu katika hatari ya kuuawa, na leo hivi, ulikinge Kanisa Takatifu la Mungu katika mitego ya adui, na katika shida yote, mtunze daima kila mmoja wetu, tupate mfano wako, tusaidie kwa msaada wako, kukaa na utakatifu maisha, kufa kifo chema, na kupokelewa mbinguni makao ya raha milele. Amina

Sala kwa Mtakatifu Yuda Thadei

(Sala hii inaweza kusaliwa kila siku au kama Novena ya siku tisa mfululizo kuomba kitu kilekile)
Mtakatifu Yuda Tadei,/ Mtume Mtakatifu,/ Mtumishi mwaminifu na rafiki wa Yesu./ Jina la yule msaliti aliyemwuza Yesu/ limewafanya wengi wakusahau./ Walakini Kanisa zima linakuheshimu/ na kukuomba kama Msaidizi katika mashaka makubwa,/ na katika mambo yasiyo na matumaini tena./
Uniombee mimi mnyonge./ Ninaomba utumie uwezo ule uliojaliwa/ wa kuleta upesi msaada kwa watu walioukosa./ Unisaidie sasa katika mahitaji yangu,/ ili nipate kitulizo na msaada wa mbinguni/ katika lazima zangu,/ masumbuko na mateso,/ hasa/ (taja shida yako)./ Pia ili niweze kumsifu Mungu nawe na wateule wote milele./
Mtakatifu Yuda Tadei,/ utuombee,/ na uwaombee watu wote wanaokuheshimu na kukuomba msaada./
Baba yetu……. Salamu Maria ……… Atukuzwe ……….

Sala ya Medali ya Mwujiza

Ee Bikira Maria uliyekingiwa dhambi ya asili, utuombee sisi wenye kukimbilia kwako, uwaombee na wale wasioukimbilia kwako, hasa maadui wa Kanisa Takatifu, na wale waliokabidhiwa kwako. Amina.

Majitoleo kwa Bikira Maria

(Sala iliyotungwa na Mtk. Aloisi)
Bibi yangu mtukufu Maria, nakuwekea amana ya roho yangu na mwili wangu, nikikuomba uipokee amana yangu, kuitunzia ulinzi mwema ulinzi bora, ninakuaminia na kila neno langu, matumaini na kitulizo na kisongo chote, na masumbuko na uzima na ukomo wa uzima wangu: nitakayo ndiyo unifanyizie kwa maombezi na stahili zako, ili mambo yangu yote yapate kuongoka, yakiwa na kufuata mapenzi yako, pamoja na mapenzi ya Mwanao. Amina.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Grace Mligo Guest Jun 21, 2024
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Lucy Wangui Guest May 2, 2024
πŸ™β€οΈ Mungu akubariki
πŸ‘₯ Peter Otieno Guest Feb 2, 2024
πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai
πŸ‘₯ Thomas Mwakalindile Guest Jan 8, 2024
πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana
πŸ‘₯ Irene Makena Guest Nov 14, 2023
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Nancy Kawawa Guest Oct 30, 2023
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Oct 20, 2023
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Victor Kimario Guest Oct 8, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Carol Nyakio Guest Sep 17, 2023
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Samuel Omondi Guest Aug 23, 2023
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Wilson Ombati Guest Jul 24, 2023
πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu
πŸ‘₯ Frank Sokoine Guest Jul 21, 2023
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Charles Mchome Guest Jul 6, 2023
πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie
πŸ‘₯ George Mallya Guest May 28, 2023
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Apr 3, 2023
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Samson Mahiga Guest Mar 8, 2023
πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani
πŸ‘₯ Charles Wafula Guest Jan 20, 2023
πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu
πŸ‘₯ Esther Cheruiyot Guest Nov 27, 2022
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Henry Mollel Guest Aug 21, 2022
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Victor Malima Guest Jun 29, 2022
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Elijah Mutua Guest May 15, 2022
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Andrew Mchome Guest Mar 11, 2022
πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
πŸ‘₯ Nancy Kabura Guest Mar 6, 2022
πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani
πŸ‘₯ David Chacha Guest Feb 19, 2022
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Michael Mboya Guest Jan 28, 2022
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Frank Macha Guest Dec 4, 2021
πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha
πŸ‘₯ Joyce Nkya Guest Dec 3, 2021
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Aug 30, 2021
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Edward Lowassa Guest Mar 31, 2021
πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha
πŸ‘₯ Janet Sumari Guest Mar 18, 2021
πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu
πŸ‘₯ Samuel Were Guest Jan 7, 2021
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ John Lissu Guest Dec 7, 2020
πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo
πŸ‘₯ Anthony Kariuki Guest Nov 5, 2020
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Joy Wacera Guest Oct 24, 2020
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Alice Wanjiru Guest Aug 21, 2020
πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe
πŸ‘₯ Andrew Mahiga Guest Aug 5, 2020
πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu
πŸ‘₯ Janet Mbithe Guest Apr 21, 2020
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Victor Kimario Guest Mar 24, 2020
πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu
πŸ‘₯ Joy Wacera Guest Feb 26, 2020
Amina
πŸ‘₯ Samson Mahiga Guest Jan 21, 2020
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Betty Cheruiyot Guest Dec 11, 2019
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Edith Cherotich Guest Oct 12, 2019
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Nancy Kabura Guest Aug 8, 2019
πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi
πŸ‘₯ Sarah Mbise Guest Jun 11, 2019
πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
πŸ‘₯ Betty Akinyi Guest Jun 5, 2019
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Stephen Kangethe Guest May 13, 2019
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest May 3, 2019
πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako
πŸ‘₯ James Kimani Guest Apr 28, 2019
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Lucy Wangui Guest Mar 21, 2019
πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri
πŸ‘₯ Josephine Guest Feb 23, 2019
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Jan 19, 2019
πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema
πŸ‘₯ Joseph Mallya Guest Jan 10, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Joyce Mussa Guest Nov 2, 2018
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Samson Tibaijuka Guest Oct 20, 2018
πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Oct 4, 2018
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Jane Malecela Guest Oct 2, 2018
πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
πŸ‘₯ Agnes Njeri Guest Sep 7, 2018
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Robert Ndunguru Guest Jul 29, 2018
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Anna Mchome Guest Jul 8, 2018
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Charles Mrope Guest Dec 15, 2017
πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About