Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Tafakari Kuhusu Matumizi Ya Mali

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Usiwe Bahili wa kutumia Mali ulizojaliwa na Mungu. Mungu amekupa Mali hizo ili ufurahie maisha uliyonayo ambayo siku moja yana mwisho.

Biblia inatufundisha hivi katika Kitabu cha Hekima ya Yoshua Bin Sira;

3Si sawa kwa mtu mchoyo kuwa tajiri.
Utajiri una maana gani kwa mtu bahili?
4Mtu anayekusanya mali kwa kujinyima mwenyewe,
anawakusanyia watu wengine.
Hao wataiponda mali yake katika anasa.
5Aliye bahili kwake mwenyewe atakuwa mkarimu kwa nani,
kama hafurahii utajiri wake mwenyewe?
6Hakuna mtu bahili kuliko anayejichukia mwenyewe;
ndivyo ubaya wake unavyomlipa yeye mwenyewe.
7Hata kama akitenda wema, hutenda kwa ajali,
na mwishowe hujulisha hali yake duni.
8Mtu mwenye kijicho ni mwovu;
huangalia pembeni na kuwadharau watu.
9Jicho la mchoyo haliridhiki na kile alicho nacho,
na uchoyo huidhoofisha roho.
10Mtu mchoyo ni bahili wa chakula,
haweki chakula mezani pake.
11Mwanangu, tumia vitu vyako kukufurahisha uwezavyo,
na mtolee Bwana tambiko zitakiwazo.
12Kumbuka kwamba kifo hakitakawia,
na kwamba hujatangaziwa kauli ya kuzimu.
13Mtendee rafiki yako mema kabla hujafa;
uwe mkarimu na kumpa kadiri ya uwezo wako.
14Usijinyime siku moja ya furaha,
usiache sehemu yako ya furaha halali ikuponyoke.
15Siku moja utawaachia wengine matunda ya jasho lako;
yote uliyochuma kwa kazi ngumu yatagawanywa kwa kura.
16Wape wengine na kupokea kwao ujifurahishe moyo,
maana mtu hatazamii starehe huko kuzimu.
17Viumbe vyote hai huchakaa kama vazi,
maana kauli ya tangu zama ni: β€œLazima mtakufa!”
18Kama vile majani katika mti uliotanda matawi:
Hupukutika yakaanguka na mengine huota,
ndivyo ilivyo kwa binadamu wenye mwili na damu:
Mmoja hufa na mwingine huzaliwa.
19Kila kilichotengenezwa huchakaa na kutoweka,
naye mtengenezaji hutoweka na kazi yake.Β (Sira 14:3-19)

Unaweza ukajikuta unatafuta Mali katika Maisha yako yote kwa kujinyima na kujikatalia lakini mwisho wa siku Mali ulizotafuta hutozifaidi wewe. Tena hata wale watakaozifaidi wanaweza wakasahau kwamba wewe ndio uliyezitafuta. Na tena wanaweza wakazitumia vibaya.

Inawezekana unajibana masha yako yote kutafuta hela bila hata kula chakula kizuri na kunywa vizuri pamoja na kuishi maisha ya furaha, lakini maisha yako yatakapokuwa yameisha wale utakaowaachia mali hizo wakaziponda na kuzitumia vibaya.

Kwa ubahili na ugumu wa kutumia Mali unaweza ukashindwa kuonyesha upendo wako kwa watoto wako, ndugu na marafiki zako. Ukiwa bahili wa kutumia mali huna nafasi ya kufurahi na wanao, ndugu na marafiki. Wakati maisha yako yatakapokuwa yameisha hao uliowabania kutumia mali zako wataishia kukuona kuwa hukuwapenda japokuwa ulitafuta mali kwa ajili yao na umewaachia mali hizo. Utakaowaachia mali hawatakukumbuka kwa sababu hukuwahi kuishi nao kwa furaha kwa kuwa ulikuwa unabania matumizi ya mali zako.

Kwa sababu ya ubahili unashindwa kutimiza wajibu wako kwa Mungu wako wa kutoa zaka na sadaka pamoja na kusaidia masikini na wahitaji.

Matokeo ya ubahili wa matumizi ya mali ni kukosa yote na kupoteza yote.

ANGALIZO:Β Sikwambii kwamba utumie mali vibaya bila kujalli Maisha yako ya baadae na maisha ya wale wanaokutegemea. Nakwambia kwamba tumia mali zako kwa staha na kwa kujinufaisha mwenyewe na wale ulionao wakati ungali hai. Usijibane sana kwa kujinyima nafasi ya kufurahia maisha yako na ya wale unaoishi nao.

Ni vizuri kujiwekea akiba ya Maisha ya baadae lakini ni vizuri zaidi kuweka wazi kwamba ni nani atakayemiliki mali zako wakati utakapokuwa haupo. Ukishaamua ni nani atakayemiliki mali zako wakati ukiwa haupo, ni wajibu wako pia kumuandaa na kumlea kwa namna ambayo ungependa aendeleze yale uliyoyaanza ili juhudi zako zisiishie tuu pale unapokua haupo, bali ziendelee hata utakapokuwa haupo.

Maisha ya binadamu ni kama majani ya mti; yanachipua, yanakomaa, yananyauka na mwishowe yanaanguka. Wakati jani linakauka na kuanguka, yapo mengine yanayo anza kujichipua na kukomaa. Jani likianguka, linaachia nafasi yale yanayochomoza na kukomaa.

Tutumie Maisha yetu vizuri, kwa furaha, amani na upendo huku tukiwatengenezea wale watakaokuja baada yetu mahali pema pa kuishi.

Zaidi sana, Tumuombe Mungu atupe hekima na Busara ya kutumia Mali anazotujalia kwa manufaa yetu na manufaa ya wenzetu huku tukimtukuza Mungu.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 100

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Grace Minja Guest Jul 7, 2024
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Jun 18, 2024
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Samson Mahiga Guest Jun 6, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Nancy Kawawa Guest Jan 1, 2024
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Charles Mrope Guest Dec 22, 2023
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest Nov 20, 2023
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ David Musyoka Guest Oct 16, 2023
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Grace Njuguna Guest Sep 10, 2023
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Bernard Oduor Guest Aug 27, 2023
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest Jul 22, 2023
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Agnes Njeri Guest Apr 26, 2023
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Patrick Akech Guest Apr 11, 2023
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Joseph Mallya Guest Apr 5, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Tabitha Okumu Guest Jan 15, 2023
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Jacob Kiplangat Guest Jan 4, 2023
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Ann Awino Guest Dec 23, 2022
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Susan Wangari Guest Dec 16, 2022
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Christopher Oloo Guest Dec 7, 2022
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Edith Cherotich Guest Oct 17, 2022
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Janet Mbithe Guest Sep 14, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Benjamin Kibicho Guest Aug 31, 2022
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Henry Mollel Guest Aug 5, 2022
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Alex Nyamweya Guest Jul 19, 2022
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ John Malisa Guest Jul 18, 2022
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Edward Chepkoech Guest May 16, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Betty Cheruiyot Guest Apr 29, 2022
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Nora Kidata Guest Apr 26, 2022
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Ann Awino Guest Apr 20, 2022
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Catherine Naliaka Guest Apr 15, 2022
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Mary Sokoine Guest Apr 6, 2022
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Faith Kariuki Guest Dec 29, 2021
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Elizabeth Mrema Guest Nov 25, 2021
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Mariam Hassan Guest Oct 30, 2021
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Lydia Wanyama Guest Oct 1, 2021
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Joy Wacera Guest Aug 7, 2021
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Joseph Kawawa Guest Jul 31, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Irene Makena Guest Jul 26, 2021
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Margaret Anyango Guest Jul 12, 2021
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Hellen Nduta Guest Apr 9, 2021
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Catherine Naliaka Guest Feb 28, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Robert Ndunguru Guest Nov 27, 2020
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Sep 21, 2020
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Paul Ndomba Guest Sep 9, 2020
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Ruth Mtangi Guest Aug 3, 2020
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Frank Sokoine Guest Jul 31, 2020
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Thomas Mtaki Guest Jun 17, 2020
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest Jun 8, 2020
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest Feb 27, 2020
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Isaac Kiptoo Guest Feb 26, 2020
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Janet Mbithe Guest Nov 29, 2019
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Thomas Mwakalindile Guest Oct 27, 2019
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ David Musyoka Guest Jul 20, 2019
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Ruth Kibona Guest Apr 18, 2019
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Henry Sokoine Guest Apr 8, 2019
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Apr 4, 2019
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Samuel Were Guest Mar 23, 2019
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest Mar 21, 2019
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Monica Lissu Guest Mar 19, 2019
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest Feb 17, 2019
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ John Kamande Guest Dec 31, 2018
Katika imani, yote yanawezekana

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About