Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Sala ya Usiku kabla ya kulala

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

SALA YA KUSHUKURU

Tunakushukuru, ee Mungu, kwa mapaji uliyotujalia leo. Amina.

Baba yetu …

Salamu Maria …

SALA YA IMANI

Mungu wangu, nasadiki maneno yote. Linayosadiki na linayofundisha Kanisa Katoliki la Roma. Kwani ndiwe uliyetufumbulia hayo. Wala hudanganyiki, wala hudanganyi. Amina.

SALA YA MATUMAINI

Mungu wangu, natumaini kwako, nitapewa kwa njia ya Yesu Kristo. Neema zako hapa duniani, na utukufu mbinguni. Kwani ndiwe uliye agana hayo nasi, nawe mwamini. Amina.

SALA YA MAPENDO

Mungu wangu, nakupenda zaidi ya chochote. Kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza. Nampenda na jirani yangu, kama nafsi yangu, kwa ajili yako. Amina.

KUTUBU DHAMBI

Tuwaze katika moyo wetu makosa ya leo tuliyomkosea Mungu kwa mawazo, kwa maneno, kwa vitendo na kwa kutotimiza wajibu. (Husubiri kidogo ).

Nakuungamia Mungu Mwenyezi, nanyi ndugu zangu, kwani nimekosa mno, kwa mawazo, kwa maneno, kwa vitendo, na kwa kutotimiza wajibu.
Nimekosa mimi, nimekosa mimi, nimekosa sana. Ndiyo maana nakuomba Maria mwenye heri, Bikira daima, Malaika na Watakatifu wote, nanyi ndugu zangu, niombeeni kwa Bwana Mungu wetu.
Mungu Mwenyezi atuhurumie, atusamehe dhambi zetu, atufikishe kwenye uzima wa milele. Amina.

SALA YA KUWAOMBEA WATU

Ee Mungu, nawaombea watu wa nchi hii, wapate kusikia maneno yako na kukupenda wewe Bwana Mungu wetu.

SALA KWA MALAIKA MLINZI

Malaika mlinzi wangu, unilinde katika hatari zote za roho na za mwili. Amina.

MALAIKA WA BWANA

(kipindi kisicho cha Pasaka)
Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria.
Naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
Salamu, Maria,…..
Ndimi mtumishi wa Bwana.
Nitendewe ulivyonena.
Salamu, Maria….
Neno la Mungu akatwaa mwili.
Akakaa kwetu.
Salamu, Maria….
Utuombee, Mzazi mtakatifu wa Mungu.
Tujaliwe ahadi za Kristu.
Tuombe:
Tunakuomba, Ee Bwana, utie neema yako mioyoni mwetu, ili sisi tuliojua kwa maelezo ya Malaika kwamba Mwanao amejifanya Mtu kwa mateso na msalaba wake tufikishwe kwenye utukufu wa ufufuko. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. AMINA.

AU;

MALKIA WA MBINGU (kipindi cha Pasaka)

Malkia wa mbingu, furahi, aleluya.
Kwani uliyestahili kumchukua, Aleluya.
Amefufuka alivyosema, Aleluya.
Utuombee kwa Mungu, Aleluya.
Furahi shangilia, ee Bikira Maria, Alaluya.
Kwani hakika Bwana amefufuka Aleluya.
Tuombe.
Ee Mungu, uliyependa kuifurahisha dunia kwa kufufuka kwake Bwana wetu Yesu Kristu, Mwanao, fanyiza, twakuomba, kwa ajili ya Bikira Maria, tupate nasi furaha za uzima wa milele. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. Amina.

ATUKUZWE (mara tatu)
Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu. Kama mwanzo na sasa na siku zote na milele. Amina.

KUJIKABIDHI

Enyi Yesu, Maria na Yosefu nawatolea moyo na roho na uzima wangu!
Enyi Yesu, Maria na Yosefu mnijilie saa ya kufa kwangu!
Enyi Yesu, Maria na Yosefu mnijalie nife mikononi mwenu!

(Rehema ya siku 300).

WIMBO:

Kwa heri Yesu mpenzi mwema,
Naenda usiudhike mno.
Nakushukuru, nakupenda,
Kwa hizo nyimbo za mwisho.
Asubuhi nitarudi.
Yesu kwa heri.

Kwa heri Mama mtakatifu,
Sasa napita pumzika.
Asante kwa moyo na nguvu,
Leo umeniombea.
Asubuhi nitarudi.
Mama kwa heri.

Kwa heri Yosefu mnyenyekevu,
Kazi zatimilizika.
Kama mchana, leo usiku,
Nisimamie salama.
Asubuhi nitarudi.
Yosefu kwa heri.

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

KUOMBA ULINZI WA USIKU

Mungu wangu naenda kulala naomba malaika 14, waende nami, wawili juu, wawili chini, wawili upande wa kuume, wawili upande wa kushoto, wawili wanifunike, wawili waniamshe, wawili wanipeleke juu mbinguni. Mimi mtoto mdogo, roho yangu ni ndogo, haina nafasi kwa mtu yoyote ila kwa Yesu pekee. Amina.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Ruth Wanjiku Guest Feb 16, 2018
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Stephen Kikwete Guest Feb 9, 2018
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Raphael Okoth Guest Jan 24, 2018
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest Nov 12, 2017
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Bernard Oduor Guest Jul 1, 2017
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Dorothy Majaliwa Guest Apr 24, 2017
πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote
πŸ‘₯ Nora Kidata Guest Jan 8, 2017
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Margaret Mahiga Guest Dec 29, 2016
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest Dec 19, 2016
πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai
πŸ‘₯ Grace Minja Guest Nov 8, 2016
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Kenneth Murithi Guest Nov 4, 2016
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Rose Waithera Guest Aug 23, 2016
πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu
πŸ‘₯ Henry Sokoine Guest Apr 7, 2016
πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako
πŸ‘₯ John Mushi Guest Jan 6, 2016
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ John Mushi Guest Dec 15, 2015
πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema
πŸ‘₯ Jane Muthui Guest Nov 13, 2015
Amina
πŸ‘₯ Peter Mugendi Guest Nov 7, 2015
πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri
πŸ‘₯ Elijah Mutua Guest Oct 15, 2015
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Anna Mchome Guest Aug 9, 2015
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Joyce Aoko Guest Jun 28, 2015
πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo
πŸ‘₯ Francis Njeru Guest Jun 26, 2015
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Grace Wairimu Guest Apr 5, 2015
πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe
πŸ‘₯ James Mduma Guest Apr 2, 2015
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About