Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Jinsi ya kujikinga na ubakaji

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Hata kama utafanya kila kitu usibakwe bado inaweza ikatokea. Ubakaji na unyanyasaji wa ujinsia unaweza kutokea kwa kila mtu. Hata hivyo kuna baadhi ya vitu ambavyo vinaweza kupunguza hatari ya kubakwa. Jizuie usiwe peke yako kwenye giza, kutembea peke yako katika misitu au sehemu ambazo zina watu wachache, kuchota maji sehemu ya mbali. Hakikisha kuwa kuna watu karibuni wa kukusaidia iwapo kuna hatari. Pia jihadhari na watu walevi na sehemu ya kunywea pombe maana watu walevi wanaweza wakawa hatari. Iwapo umelazimika kufanya kazi katika mazingira ya hatari, jaribu kujadili tatizo hili na wazazi wako au mtu unayemwamini na muulize huyu mwanamume au mwanamke azungumze na wazazi wako. Usikubali zawadi au upendeleo, kama unafikiri unapewa wewe kwa kubadilishana na ngono. Kama unajisikia unatishwa jaribu kukimbia na piga kelele kwa kutafuta msaada mara moja. Utafiti umeonyesha kuwa wasichana au wanawake ambao kwa ushupavu wanasema hapana na ambao wanathubutu kupiga kelele na kuvutia hisia za wengine wakati wanaposhambuliwa wana hatari kidogo ya kubakwa. Unapokuwa unajitetea kwa uhakika unapoanza unachopenda na usichopenda, ni sehemu muhimu ya kujilinda.
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 0

Please log in or register to comment or reply.
No comments yet. Be the first to share your thoughts! πŸ“

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About