Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/katoliki/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ
AckyShine

Mambo ya Msingi kuyajua Ili uishi na watu vizuri

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Nimezipenda hizi nasaha. Naamini na nyinyi wenzangu hamtakosa japo machache ya kujifunza:-
1. Epuka hasira za ovyo na kila mtu, kuwa msikivu kabla ya kukimbilia maamuzi (elewa kuwa ukiwa na hasira huwezi kupata suluhu ya jambo)
2. Usiwatendee wengine ubaya ukadhani kuwa utakuwa salama (ubaya hulipwa kwa ubaya, ipo siku ubaya wako kwa wengine utakurejea kama sio kuwarejea watu wa kizazi chako)

3. Usichukue maamuzi kabla ya kutafiti ukweli (pengine wapo wanadamu wanaopenda kuonekana wao wema kwa kuumiza wengine). Mtuhumu mtu lakini mpe muda wa kumsikiliza, usimshambulie mtu kwa maneno makali bila kuujua ukweli, ukijua ukweli nafsi inaweza kukusuta.

4. Mchukulie kila mwanadamu ni mkosaji (tambua kuwa hata wewe unawakosea sana wengine na wanakuvumilia. Hivyo usiwe mwepesi wa kuwaadhibu wenzio kwa ubaya).

5. Usipande mbegu ya chuki na ubaya katika jamii unayoishi ukadhani itakuacha salama (chuki hukua kama mti utambaao, ukiipanda ndani ya jamii yako, haitatoka kwako na inaweza kutafuna kizazi chako ukajutia.

6. Tambua kuwa yule unayeishi nae ni mwanadamu kama wewe, mpe heshima na mwonyeshee upendo hata kama huoni anafanana nawe. Maisha ni duara huenda ulikuwa kama yeye au atakuja kuwa kama wewe baadae.

6. Usiwe muongeaji ovyo ovyo na usiye na subira. Kuongea sana kunapoteza busara.

7. Jiepushe na maisha ya kusukumwa na wengine kufanya jambo usilojua manufaa yake. Jifunze kujitegemea kiakili. Sio kila unayemdhania rafiki moyoni mwake yupo pamoja nawe, na ukashirikiana nae, wengi wa marafiki zetu hututumia sana kuliko tunavyoweza kuwatumia wao.

8. Usipende sana kugombana na watu kwa njia ya maongezi yanayodumu kama vile, ujumbe wa maandishi, mawasiliano ya simu au ujumbe wa maneno (SMS). Kumbuka kuwa maneno yanaishi kuliko ugomvi au uadui, ipo siku yatakurudi na utajiona mpumbavu na kukosa pa kujificha. Jifunze kusubiri.

9.Usifumbue mdomo wako kutamka ubaya au kunyanyua kidole chako kuandika ubaya juu ya mwenzio bila kujiuliza mara mbili moyoni mwako hatima ya unachokitoa kwa mwingine.

10. Jishushe na jifunze kusikiliza wengine wakati wa mazungumzo ili uweze kujifunza kabla ya kukurupuka kujibu, usikivu ni kipimo cha busara, mtu anayekurupuka kujibu jibu kila anachosikia hawezi kuwa kiongozi, Mume au Mke mwema kwani mara nyingi atapotoka tu.

10. Usitunze hasira nyingi moyoni kwani hasira hukaa kifuani mwa mpumbavu. Jitahidi pia kuepuka kuwa na hasira mara kwa mara na zisizo na maana. Elewa kuwa hasira zisizo maana hukupunguzia maisha na kukupa maumivu wewe mwenyewe kuliko yule uliyemfanyia hasira, utakufa kwa magonjwa kabla ya wakati ufaao.

11. Thamani yako inategenezwa na watu wengine, wewe kama ni mtoto, mheshimu sana mzazi wako na kama umeoa au kuolewa, heshimu wazazi na familia ya mke au mumeo kwa kuwa bila wao, usingekuwa hivyo ulivyo leo unajivunia ndoa njema, kwa kuwa yupo mtu alimzaa huyo mwenzio. Mheshimu kwa lolote liwe jema au baya, utalipwa kwa wakati ufaao.

13. Usijibizane na mtu usiyemjua au ambaye hawezi kukupunguzia kitu katika maisha yako. Tambua kuwa unapunguza sehemu kubwa ya maisha yako kwa kutafuta magomvi na mtu wa mbali nawe.

14. Kumbuka asili yako, kumbuka upo hapo kwa kuwa kuna mahali ulitoka, maisha yanabadilika, usidharau pale ulipokuwa zamani kwa kuwa ndipo palipokufanya leo uwe hapo.

15. Subiri, sikiliza, elekeza, vumilia. Elewa sio kila mtu ana uelewa kama wako. Jitahidi kuwa mvumilivu katika kila jambo, usiinuke kuwafokea au kuwakaripia wengine kwa jambo ambalo pengine nao wanahitaji muda kueleweshwa ili walifanye vyema. Kumbuka sana, kuna wakati nawe ulikuwa huelewi kabisa lakini wapo wenzio walikuvumilia, wakakuelekeza njia njema, kufokea wengine mara kwa mara sio njia njema ya kuwafundisha bali ni kuwaweka mbali nawe.

Kumbuka: Ishi kwa kumpendeza Mungu.

Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke

Kitabu hiki niย Soft copy [pdf]ย kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.

[products columns="2" ids="30827"]
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Kuimarisha Upatanishi na Uwiano katika Mahusiano

Kuimarisha Upatanishi na Uwiano katika Mahusiano

Kuimarisha Upatanishi na Uwiano katika Mahusiano

Mahusiano ni muhimu kwa maisha ya kila si... Read More

Jinsi ya Kushiriki majukumu ya nyumbani na majukumu ya malezi na mpenzi wako

Jinsi ya Kushiriki majukumu ya nyumbani na majukumu ya malezi na mpenzi wako

Kushiriki majukumu ya nyumbani na majukumu ya malezi ni muhimu katika kujenga usawa na ushirikiano k... Read More
Ushawishi wa Teknolojia katika Kufanya Mapenzi: Changamoto na Fursa za Zama za Kidijitali

Ushawishi wa Teknolojia katika Kufanya Mapenzi: Changamoto na Fursa za Zama za Kidijitali

  1. Teknolojia imebadilisha jinsi watu wanavyofanya mapenzi. Kwa sasa, kuna zana nyingi za ... Read More

Jinsi ya Kuimarisha uhusiano na familia ya mpenzi wako

Jinsi ya Kuimarisha uhusiano na familia ya mpenzi wako

Kuimarisha uhusiano na familia ya mpenzi wako ni muhimu katika kujenga msingi thabiti na kuwa sehemu... Read More
Je, kuna umuhimu wa kuwa na uelewa wa afya ya uzazi na uzazi katika ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuna umuhimu wa kuwa na uelewa wa afya ya uzazi na uzazi katika ngono/kufanya mapenzi?

Habari yako rafiki! Leo, ningependa kuzungumza nawe kuhusu umuhimu wa kuwa na uelewa wa afya ya u... Read More

Njia za Kuimarisha Ushirikiano wa Kijamii na Familia katika Mahusiano

Njia za Kuimarisha Ushirikiano wa Kijamii na Familia katika Mahusiano

  1. Elewa Uzito wa Ushirikiano wa Kijamii na Familia: Jamii na familia ni muhimu sana katik... Read More

Kuwa na Wazi kuhusu Matumizi ya Dawa katika Kufanya Mapenzi: Mwongozo na Mjadala wa Kimahusiano

Kuwa na Wazi kuhusu Matumizi ya Dawa katika Kufanya Mapenzi: Mwongozo na Mjadala wa Kimahusiano

Kuwa na Wazi kuhusu Matumizi ya Dawa katika Kufanya Mapenzi: Mwongozo na Mjadala wa KimahusianoRead More

Njia za Kujenga Urafiki Mzuri na Msichana Kabla ya Kuwa na Uhusiano

Njia za Kujenga Urafiki Mzuri na Msichana Kabla ya Kuwa na Uhusiano

Karibu ndugu yangu kwenye makala hii ambao inazungumzia njia mbalimbali ambazo utaweza kutumia ku... Read More

Njia za Kuimarisha Ushirikiano wa Kijamii na Kuweka Mipango ya Shughuli za Familia

Njia za Kuimarisha Ushirikiano wa Kijamii na Kuweka Mipango ya Shughuli za Familia

Katika jamii, ushirikiano wa kijamii ni muhimu sana katika kuwezesha maendeleo na ustawi wa wanaj... Read More

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kuendeleza na kudumisha stadi za uongozi

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kuendeleza na kudumisha stadi za uongozi

Karibu kwenye makala hii inayozungumzia "Jinsi ya Kusaidiana na Mpenzi Wako Katika Kuendelez... Read More

Kujenga Kujiamini katika Kufanya Mapenzi: Jinsi ya Kukubali na Kufurahia Utu wako

Kujenga Kujiamini katika Kufanya Mapenzi: Jinsi ya Kukubali na Kufurahia Utu wako

  1. Kujenga kujiamini katika kufanya mapenzi ni muhimu sana kwa afya yetu ya kihisia na kim... Read More

Vidokezo vya Kuwa na Mazungumzo ya Kusisimua na Msichana

Vidokezo vya Kuwa na Mazungumzo ya Kusisimua na Msichana

Kama mvulana, unajua kuwa mazungumzo na msichana yako yanaweza kuwa magumu sana. Unaweza kuwa na ... Read More

๐Ÿ“– Explore More Articles
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About