Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-25 10:23:10 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Unga - 2 Vikombe
Cocoa ya unga - 1 Kijiko cha supu
Sukari ya hudhurungi - 1 Kikombe
Siagi - ¾ Kikombe
Yai - 1
Molasses - ¼ Kikombe
Baking soda - 2 vijiko vya chai
Mdalasini wa unga - 1 kijiko cha chai
Tangawizi mbichi - 1 kijiko cha supu
Karafuu ya unga - ½ kijiko cha chai
Chumvi ½ kijiko cha chai
Vanilla ½ kijiko cha chai
MAANDALIZI
Katika bakuli, chunga unga, baking soda, chumvi na cocoa. Weka kando. Washa oven lipate moto huku unatayarisha biskuti. Katika bakuli jengine, mimina siagi na sukari upige kwa mashini ya keki hadi mchanganyiko uwe laini kama dakika mbili. Mimina molasses na yai ndani ya mchanganyiko wa siagi na sukari uchanganye vizuri. Mimina unga kidogo kidogo huku unachanganya na mwiko hadi unga wote umalizike. Mimina mdalasini, karafuu na tangawizi, changanya vizuri. Weka mchanganyiko wako ndani ya friji kama masaa mawili. (Ukipenda unaweza kuhifadhi mchanganyiko wako ndani ya mfuko wa freezer na uoke siku nyengine.) Tengeneza viduara vidogo vidogo.
Chovya kila kiduara katikati sukari, kisha panga kwenye treya ya kuoka
Rudisha viduara katika friji kama nusu saa.
Oka katika oven 350ºF kwa muda wa dakika 15.
Toa biskuti kwenye oven na uache zipoe kama dakika kumi. Panga kwenye sahani tayari kuliwa.
Jinsi ya kupika Biskuti Nyembamba (Wafer Bar) Za Chokoleti Na Njugu
Updated at: 2024-05-25 10:23:08 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Wafer Powder/gram wafer (unga wa biskuti uliosagwa wa tayari) - vikombe 2
Maziwa ya Mgando Matamu ya Kopo - 2 vikombe
Nazi iliyokunwa - ½ Kikombe
Chokoleti vipande vipande - 1 Kikombe
Njugu vipande vipande - ½ Kikombe
Siagi - 227 g
MAPISHI
Yeyusha siagi motoni kisha changanya na unga wa wafer acha kidogo motoni Mimina katika treya unayochomea itandaze vizuri, kisha mimina maziwa juu yake pamoja na njugu vipande , nazi iliyokunwa na vipande vya chokoleti. Choma (bake) kwenye oveni kwa moto wa 350ºC kwa dakika 20. Katakata tayari kwa kuliwa
Mapishi ya Wali maharage,mchuzi wa samaki na spinach
Updated at: 2024-05-25 10:37:46 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele (rice 1/2 kilo) Maharage yaliyochemshwa (boiled red kidney beans 1 kikombe cha chai) Samaki waliokaangwa ( 2 fried fish) Nyanya ya kopo (tin tomato 1/2 ya tin) Vitunguu vilivyokatwa (onion 2) Kitunguu swaum (garlic 3 cloves) Tangawizi (ginger kiasi) Limao (lemon 1/2) Chumvi (salt) Pilipili (scotch bonnet pepper 2) Mafuta (vegetable oil) Spinach Tui la nazi (coconut milk 1 kikombe cha chai)
Matayarisho
Saga nyanya, kitunguu, tangawizi na kitunguu swaum pamoja. Tia kwenye sufuria na upike mpaka maji yakauke kisha tia curry powder, mafuta na chumvi na upike tena mpaka mchanganyiko uive kisha tia samaki na limao na maji kiasi na uache uchemke kiasi. Na hapo mchizi utakuwa tayari. Osha na uzikate spinach kisha kaanga kitunguu na mafuta kiasi (hakikisha visiwe vya brown kisha tia spinach na chumvi. zipike kwa muda wa dakika 3-4 na hapo zitakuwa tayari zimeshaiva. Wali: Chemsha maji kiasi kisha tia, chumvi, pilipili nzima(isikatwe) mafuta na tui la nazi. Baada ya hapo koroga na utie mchele na maharage na ufunike uache uchemke mpaka maji yakauke. Kisha geuza na ufunike tena na uuache mpaka uive. Baada ya hapo chakula chako kitakuwa tayari kwa kuseviwa.
Updated at: 2024-05-25 10:23:06 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga - 4 Vikombe vya chai
Siagi - 1 Kikombe cha chai
Hiliki ½ Kijiko cha chai
VIAMBAUPISHI:SHIRA
Sukari - 2 Vikombe vya chai
Maji - 1 Kikombe cha chai
Vanilla ½ Kijiko cha chai
(cocoa ukipenda kugawa visheti aina mbili) 2 Vijiko vya chai.
JINSI YA KUTENGENEZA
Tia unga kwenye bakuli pamoja na siagi na hiliki. Changanya vizuri isiwe na madonge. Tia maji baridi vikombe viwili kasoro vya chai changanya ukiona bado ongeza maji kidogo, iwe kama chapati usikande uchanganye tu. Halafu utakata sampuli unayopenda mwenyewe. Unaweka karai ya mafuta yakisha kupata moto unaanza kuchoma moto usiwe mkali sana, kiasi, baadae unaweza kuongeza moto na vikaange hadi viwe rangi ya dhahabu, kisha viepue vichuje mafuta. . Ukipenda gawa visheti sehemu mbili, na shira pia igawe sehemu mbili Changanya nusu ya visheti kwa shira nyeupe. Nusu ya shira nyingine ibandike tena motoni na tia cocoa vijiko viwili vidogo vya chai. Inapochanganyika cocoa vizuri changanya nusu ya visheti ulivyogawa kupata visheti vya shira ya cocoa.
Jinsi ya kutengeneza Muhogo Wa Nazi Na Samaki Wa Kukaanga
Updated at: 2024-05-25 10:34:39 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Muhogo - 3
Tui La Nazi - 2 vikombe
Chumvi - kiasi
Pilipili mbichi - 2
Mafuta - 1 kijiko moja
Kitunguu maji - 1 kidogo
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Chambua muhogo ukatekate au tumia iliyo tayari. Chemsha muhogo katika sufuria kwa maji kidogo na chumvi, funika uive muhogo. Karibu na kukauka maji tia tui, kitunguu maji ulichokatakata na pilipili mbichi. Unaupika moto mdogo mdogo hadi ukauke tayari kuliwa na samaki au kitoweo chochote kingine
Mapishi ya wali mtamu Wa Nazi Kwa Maharage Na Samaki Nguru Wa Kukaanga
Updated at: 2024-05-25 10:23:11 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Wali:
Mchele mpunga - 4 Vikombe
Tui la nazi - 6 vikombe
Chumvi - kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha mchele weka kando. Bandika tui jikoni likichemka tia mchele na chumvi. Funika uchemke, tui likikauka wacha moto mdogomdogo hadi wali uive ukiwa tayari. Ikiwa unatumia mkaa unapalia juu yake.
Maharage Ya Nazi
Maharage - 3 vikombe
Tui la nazi zito - 1 kikombe
Tui la nazi jepesi - 1 kikombe
Kitunguu maji - 1
Kitunguu saumu(thomu/galic) kilosagwa -1 kijiko cha chai
Chumvi - kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Chemsha maharage mpaka yaive. Katiakatia kitunguu maji na tia thomu, tia na tui jepesi kikombe kimoja. Tia tui zito endelea kuweka katika moto mdogomdogo hadi yakaribie kukauka yakiwa tayari.
Samaki Nguru Wa Kukaanga
Samaki Wa Nguru - 4 vipande
Kitunguu saumu(thomu/galic) & tangawizi ilosagwa - 1 kijiko cha supu
Pilipili mbichi - 4
Ndimu - 2 kamua
Bizari ya samaki -1 kijiko cha chai
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Mwoshe samaki kisha mtie kitunguu thomu, tangawizi ilosagwa, chumvi, pilipilimbichi ilosagwa, ndimu na bizari ya samaki. Mwache akolee viungo kwa muda kidogo. Makaange katika mafuta hadi aive akiwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:37:37 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Boga la kiasi - nusu yake
Tui zito la nazi 1 ½ gilasi
Sukari ½ kikombe
Hiliki ½ kijiko cha chai
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Menya boga kisha katakata vipande vya kiasi. Weka katika sufuri tia maji kiasi ya kuchemshia na kuwiva bila ya kubakia maji mengi. Changanya tui na sukari na hiliki kisha mimina juu ya boga wacha katika moto dakika chache tu bila ya kufunika. Epua mimina katika chombo likiwa tayari.
Updated at: 2024-05-25 10:37:49 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mackerel 2 Kitunguu swaum na tangawizi (ginger and garlic paste) 1 kijiko cha cha kula Pilipili iliyo katwakatwa (chopped scotch bonnet ) 1/2 Limao (lemon) 1/2 Chumvi (salt) kiasi Curry powder 1/2 kijiko cha chai Coriander powder 1/2 kijiko cha chai Mafuta 1 kijiko cha chai
Matayarisho
Safisha samaki kisha wakaushe maji ( ukipenda unaweza kuwakata kati au ukawapika wazima) Baada ya hapo wakate mistari kila upande ( ili spaces ziweze kuingia ndani) kisha waweke kwenye bakuli na utie spice zote. Wachanganye vizuri kisha waweke frijini na uwaache wamarinate kwa muda wa masaa 3. Baada ya hapo washa oven kisha wapakaze mafuta na uwafunge kwenye foil na uwatie kwenye oven kwa muda wa dakika 20. Baada ya hapo fungua foil na uwaache kwenye oven kwa muda wa dakika 10 ili wapate kukauka kidogo. Na hapo watakuwa tayari kwa kuliwa. Unaweza kuwala kwa kitu chochote upendacho.
Jinsi ya kupika Pilau ya Nyama ya Kusaga Na Mboga Mchanganyiko
Updated at: 2024-05-25 10:23:13 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele - 2 Mugs
Viazi - 3
Nyama ya Kusaga - 1 Pound
Mboga mchanganyiko za barafu - 1 Mug
(Frozen vegetable)
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi - 2 vijiko vya supu
Garam masala - 1 kijiko cha supu
Nyanya - 1
Kitungu maji - 1
Mdalasini nzima - 1 vijiti
Karafuu - 3 chembe
Pilipili mbichi - 1
Chumvi - kiasi
Maji - 2 ½ Mugs
Mafuta - 3 vijiko vya supu
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha mchele na uroweke kiasi kutegemea aina ya mchele. Katakata viazi kaanga katika mafuta, toa weka kando. Tia mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu maji mpaka kigeuke rangi ya hudhurungi (brown). Tia nyama ya kusaga, thomu na tangawizi, pilipili, bizari zote na chumvi. Kaanga hadi nyama iwive. Katakata nyanya uliyokatakata itie katika mchanganyiko wa nyama na endelea kukaanga kidogo tu. Tia mboga ya barafu (frozen vegetables) Tia maji, kidonge cha supu. Yatakapochemka tia mchele. Punguza moto uwe mdogo funika kwa muda wa ½ saa hadi wali ukauke na uwive. Utakuwa tayari kuliwa.