Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-25 10:37:38 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Mchele basmati, pishori - 3 vikombe
Vitunguu katakata - 2
Nyanya/tungule katakata - 5 takriban
Viazi/mbatata menya katakata - 3 kiasi
Thomu (saumu/garlic) ilosagwa - 1 kijiko cha supu
Bizari mchanganyiko - 1 kijiko cha kulia
Hiliki ya unga - ½ kijiko cha chai
Kidonge cha supu - 2
Chumvi - kisia
Mafuta - ½ kikombe
Maji ya moto au supu - 5 takriban
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha na roweka mchele Katika sufuria weka mafuta yashike moto, tia viazi, vitunguu ukaange. Vikianza tu kugeuka rangi tia thomu na bizari, hiliki, endelea kukaanga kidogo. Tia nyanya kaanga lakini usiache zikavurugika sana. Tia mchele ukaange chini ya dakika moja. Tia maji ya moto, na kidonge cha supu au supu yoyote kiasi cha kufunika mchele yazidi kidogo. Koroga vichanganyike vitu, kisha funika upike kama pilau. Pakua ikiwa tayari, tolea kwa samaki wa kukaanga au kitoweo chochote kile
2. Unaweza kutwanga kwa kutumia kinu au kuchemsha kidogo na kisha kusaga kwa kutumia mashine. Ukitumia mashine uwe makini usije ukasaga sana ukaharibu.
3. Kaanga karanga kidogo na kisha zisage ziwe unga unga.
4. Chemsha kisamvu chako hadi kiive.
5. Katakata kitunguu, karoti na na nyanya
6. Anza kuunga kisamvu kwa kukaanga vitunguu, weka karoti na kisha nyanya na vikishaiva weka kisamvu na koroga pamoja kisha weka karanga. Acha vichemke kwa muda na unaweza pia weka na nazi tui la kwanza.
7. Baada ya muda mfupi epua na kitakiwa tayari. Waweza kula kwa ugali, wali, chapati, makande n.k
Updated at: 2024-05-25 10:37:55 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Nyanya 1 kg Maji Iita ½ Chumvi kijiko kidogo 1 Sukari
Hatua
• Osha nyanya, katakata na chemsha na maji mpaka zilainike. • Chuja juisi. • Pima juisi - vikombe 2 vya juisi kwa kikombe 1 cha sukari, weka kwenya sufuria safi . • Ongeza chumvi, chemsha ukikoroga mpaka ichemke. • Mara ikichemka epua, pozesha na weak kwenya chombo safi kwa kunywa.
Updated at: 2024-05-25 10:23:09 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Philo (thin pastry) manda nyembamba - 1 paketi
Siagi - ¼ Kikombe cha chai
Baking powder - 2 Vijiko vya chai
Pistachio/ lozi - 2 vikombe vya chai
Mafuta - ½ Kikombe
VIAMBAUPISHI VYA SHIRA
Sukari - 2 Vikombe vya chai
Maji - 2 ½ Vikombe vya chai
ndimu - ½ kijiko cha chai
JINSI YA KUANDAA
Tafuta treya iliyokuwa sawa na ukubwa wa hizo manda nyembamba (philo) au zikate hizo manda kwa ukubwa wa treya (mraba au mstatili) Kisha yeyusha siagi changanya na mafuta. Kisha panga manda moja pakaza mafuta juu yake kisha weka manda nyingine juu yake kisha pakaza mafuta tena weka manda nyingine juu yake, endelea kufanya hivyo mpaka ziwe kama sita au saba kisha nyunyizia pistachio na lozi halafu panga tena manda na mafuta manda na mafuta tena sita au saba kisha nyunyizia tena pistachio na lozi. Panga namna hivyo mpaka treya ijae inapofika manda ya mwisho kata vipande vya mraba vidogodogo humo humo kwenye treya kisha nyunyizia mafuta yaliyobaki. Washa moto wa oven 350°F kwa muda wa dakika 20 au hadi rangi ibadilike kidogo (isikauke sana) Chemsha syrup yako kama shira ya majimaji lakini isiwe nzito sana ikishakuwa tayari mwisho tia ndimu acha ipoe kidogo kisha miminia juu ya treya yote halafu malizia kunyunyizia pistachio na lozi zilizobaki. Zikishakuwa tayari zipange kwenye sahani tayari kwa kuliwa.
ANGALIZO
Ukishatoa treya kwenye oven wacha ipoe kidogo na syrup yako pia wacha ipoe kidogo kabla hujamimina, ukitia ya motomoto zitalainika. Manda nyembamba za baklawa zinauzwa tiyari madukani kwenye pakiti.
Updated at: 2024-05-25 10:37:43 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Viazi (potato) 1 kilo Nyama ya ng'ombe 1/2 kilo Nyanya ya kopo iliyosagwa 1/2 tin Vitunguu maji 2 Tangawizi/ swaum 1 kijiko cha chai Hoho 1 Curry powder 1 kijiko cha chai Pilipili ya unga 1/2 kijiko cha chai Limao 1/2 Chumvi Coriander Mafuta ya kupikia
Matayarisho
Safisha na katakata nyama ktk vipande vidogovidogo kisha weka pembeni. Baada ya hapo kaanga vitunguu mpaka viwe vya brown kisha tia nyama, swaum/ tangawizi, chumvi na limao. Ichanganye vizuri kisha funika na uipike mpaka iive na maji yote yakauke yani yabaki mafuta tu. Baada ya hapo tia viazi vilivyokatwa vipande vya wastani vikaange kwa muda wa dakika 10 kisha tia pilipili na curry powder na nyanya. Funika na punguza moto.Pika mpaka nyanya iive vigeuze kisha tia vimaji kidogo vya kuivishia viazi. Viazi vikikaribia kuiva(hakikisha vinabaki na rojo kidogo) tia hoho na upike kwa muda wa dk 5 kisha malizia kwa kutia coriander. Changanya vizuri kisha ipua na viazi vyako vitakuwa tayari kwa kuliwa.
Mapishi ya Pilau Ya Nyama Ng'ombe Karoti Na Zabibu
Updated at: 2024-05-25 10:37:34 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo - Nyama
Nyama ng’ombe ya mifupa ilokatwa vipande - 1 kilo
Tangawizi na thomu (somu/garlic) ilosagwa - 2 vijiko vya supu
Bizari mchanganyiko/garama masala - 1 kijiko cha chai
Chumvi - Kiasi
Vipimo - Wali
Mchele - 4 glass
Mbatata/viazi menya katakata - 3 kubwa
Vitunguu katakata - 5
Kitunguu thomu kilosagwa (garlic/somu) - 1 kijiko cha supu
Hiliki ya unga - 1 kijiko cha chai
Bizari nzima ya pilau/cumin - 1 mti
Samli au mafuta - 2 Vijiko vya supu
Karoti zilokatwakatwa nyembamba - 6-7
Zabibu - Kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Katika sufuria weka mafuta kijiko kimoja cha supu tia nyama na viungo vyake. kaushe katika moto hadi ikaribie kukauka kisha tia maji kiasi cha kuivisha na kubakisha supu ya mchele. Katika sufuria ya kupikia weka samli au mafuta ishike moto. Tia mbatata/viazi kaanga, tia vitunguu kaanga kidogo. Tia kitunguu thomu, hiliki, bizari ya pilau endelea kukaanga hadi viwe rangi ya brown kidogo. Tia mchele kaanga kidogo, kisha mimina nyama na supu yake. Funika wali uwive. Weka kikaangio katika moto, tia samli kijiko kimoja kisha tia karoti na zabibu, kaanga kwa sekunde chache tu kwa ajili ya kulainisha karoti na zabibu. Utakapopakuwa wali, pambia juu karoti na zabibu.
Updated at: 2024-05-25 10:37:27 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Kupata takriban gilasi 6
Mabungo - 3
Maji - 6 au 7 Gilasi
Sukari - kiasi upendacho
Chumvi - kidogo sana
Namna Ya Kutayarisha:
Kata mabungo na toa nyama yake tia katika mashine ya kusagia. Tia maji, sukari na chumvi usage kidogo tu. Chuja kisha mimina katika jagi uweke katika friji. Mimina katika gilasi.
Bizari ya unga (cummin powder) - 1 Kijiko cha chai
Mafuta ya kukaangia - Kiasi
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Safisha daal kwa kutoa mawe ikiwa yapo, kisha osha na roweka dakika 15 hivi. Kisha chemsha kwa kutia maji, bizari ya manjano, chumvi, pili pili ya unga na maji ya ndimu hadi iive na kuvurujika. Halafu chukua kisufuria na kaanga kitungu, kisha thomu na mwisho tia bizari ya pilau. Kisha mimina mchanganyiko wa kitunguu kwenye sufuria ya daal (iliyokwisha iiva)na uchanganye na iwache motoni kidogo itokote. Ukipenda mimina mchanganyiko kwenye blenda na usage mpaka iwe laini. Tia kwenye bakuli na itakuwa tayari kuliwa na wali na samaki ukipenda
Updated at: 2024-05-25 10:37:43 (1 year ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele 2 vikombe vya chai Choroko kikombe 1 na 1/2 Nazi kopo 1 Swaum 1 kijiko cha chakula Kitunguu 1 kikubwa Binzari nyembamba 1 kijiko cha chai Chumvi Mafuta
Matayarisho
Loweka choroko usiku mzima, pindi ukianza kupika loweka mchele nusu saa kisha katika sufuria kubwa, kaanga vitunguu vikianza kuwa vya brown tia swaum na binzari nyembamba kisha tia choroko, mchele, chumvi,nazi na maji mengi kiasi yakuivisha choroko pamoja na mchele. Pika mpaka vitu vyote viive na viwe vilaini kisha upondeponde kiasi.Baada ya mseto wako kuiva utakuwa unaonekana kama uji wa mchele vile. Na Baada ya hapo mseto wako utakuwa tayari kwa kuliwa na mboga yoyote uipendayo.Inapendeza zaidi kuliwa vile tu ukishamalizwa kupikwa
Safisha samaki na kisha uwamarinate na kitunguu swaum, tangawizi, limao na chumvi kwa muda wa nusu saa. Baada ya hapo wakaange na usiwakaushe sana kisha waweke pembeni. Chukua fry-pan kisha tia mafuta kidogo sana (kama 1/2 kijiko cha chai) kisha tia vitunguu maji na uvikaange kwa muda wa dakika 2 (kwani havitakiwi kuiva kabisa) kisha waweke samaki na uwachanganye na hivyo vitunguu. Kisha baada ya hapo tia giligilani iliyokatwa, kamulia limao na tia chumvi kidogo kisha geuzageuza ili kuchanganya vitu vyote na kisha ipua. Baada ya hapo menya na ukate viazi katika vipande vya wastani, na kisha uvichemshe kidogo na visiive kabisa. Baada ya hapo weka sufuria jikoni kwenye moto wa wastani na utie mafuta kidogo (kama vijiko 2 vya chakula) na kisha tia viazi na uanze kuvipika kwa kuvigeuzageuza mpaka viive na kuwa rangi ya brown kisha tia chumvi kidogo, curry powder na giligilani iliyokatwa.Vipike kwa muda wa dakika mbili kisha viipue. Na baada ya hapo malizia kwa kupika asparagus. Kwanza zioshe kisha zikate kati. Baada ya hapo weka mafuta kidogo kama 1/2 kijiko katika fry-pan yakisha pata moto tia kitunguu swaum, asparagus na chumvi.Zipike kwa kuzigeuzageuza kwa muda wa dakika 5 na hapo zitakuwa zimeshaiva na tayari kwa kuliwa pamoja na samaki na viazi. Unaweza kuvisevu kwa ketchup.