Log in to access your menu with tools for managing 📝 tasks, 👥 clients, 💰 finances, 📖 learning, 🔍 personal growth, and 🌟 spirituality, all in one place!.
Welcome to AckySHINE, your go-to platform for personal growth, productivity, and well-being, offering tools tailored to organize your life, manage finances, and deepen your journey.
Updated at: 2024-05-25 10:35:26 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIPIMO
Unga wa mchele 500g
Samli 250g
Sukari 250g
Hiliki iliyosagwa 1/2 kijiko cha chai
Arki (rose flavour) 1/2 kijiko cha chai
Baking powder 1 kijiko cha chai
Mayai 4
Maji ya baridi 1/2 kikombe cha chai
NAMNA YA KUTAYRISHA NA KUPIKA
1. Saga sukari iwe laini kiasi, changanya unga wa mchele, baking powder, hiliki na sukari.
2. Pasha moto samli mpaka iwe nyepesi kama maji mimina kwenye ule mchanganyiko wa unga wa mchele, kisha uchanganye pamoja na arki.
3. Ongeza mayai yaliopigwa endelea kuchanganya mpaka unga umeanza kuchanganyika vizuri.
4. Ongeza maji ya baridi sana kama nusu kikombe tu ili uchanganyike vizuri.
5. Kata kwa design unayotaka viwe vinene visiwe kama cookies za kawaida kama ilivyo kwenye picha na ukipenda utaweka kidoto kwa kutumia zaafarani katikati ya kileja kama inavyoonesha hapo juu.
6. Choma kwa moto wa baina ya 300F na 350F kwa dakika 15 mpaka 20 visiwe vyekundu toa na tayari kwa kuliwa
Updated at: 2024-05-25 10:37:57 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Unga wa ngano vikombe vikubwa 3 Boga lililopondwa kikombe 1 Baking powder vijiko vidogo Sukari kikombe kikubwa 1 Blue band kikombe ½ Vanilla kijiko kidogo 1 Mayai 2 Maji kiasi/ maziwa (kama nilazima)
Hatua
• Osha boga, Kata, ondoa mbegu, kisha kata vipande vikubwa, chemsha na maji mpaka vilainike. • Kwangua boga la ndani ukiacha maganda na ponda sawasawa. • Chekecha unga (kila kikombe 1, vijiko vidogo 2 vya baking powder) kwenye bakuli kubwa. • Ongeza blue band na changanya sawasawa na vidole. • Ongeza sukari na changanya. • Ongeza mayai na koroga na mwiko. • Ongeza boga lililopondwa na koroga njia moja mpaka ilainike. • (Kama haikulainika ongeza yai /mayai au maziwa/ maji kidogo). • Ongeza vanilla na koroga. • Paka mafuta chombo cha kuokea au sufuria kisha chekecha unga kidogo wa ngano. • Mimina rojo la keki kwenye sufuria au chombo cha kuokea. • Oka kwenye oven au tumia sufuria na weka mkaa wa moto juu na chini moto kidogo mpaka iive. • Jaribu kuchoma kisu katikati, kama ni kavu keki imeiva, epua, pozesha kata tayari kwa kula, kama kitafunio.
Updated at: 2024-05-25 10:37:47 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Nyama ya ng'ombe (beef 1/2 kilo) Mchele (rice 1/2 kilo) Vitunguu (onion 2) Viazi (potato 2) Vitunguu swaum (garlic 3 cloves) Tangawizi (ginger) Nyanya ya kopo (tomato 1/2 ya tin) Curry powder (1/2 kijiko cha chai) Binzari nyembamba ya kusaga (cumin 1/2 kijiko cha chai) Binzari manjano (tarmaric 1/2 kijiko cha chai) Mafuta (vegetable oil) Chumvi (salt) Rangi ya chakula (food colour) Giligilani (fresh coriander) Maziwa ya mgando (yogurt kikombe 1 cha chai) Hiliki nzima (cardamon 3cloves) Karafuu (clove 3) Pilipili mtama nzima (black pepper 5) Amdalasini (cinamon stick 1)
Matayarisho
Katakata nyama kisha ioshe na uiweke kwenye sufuria kisha tia kitunguu swaum, tangawizi, nyanya, curry powder, binzari zote, chumvi na maziwa ya mgando kisha bandika jikoni ichemke mpaka nyama iive na mchuzi ubakie kidogo.Baada ya hapo kaanga viazi na uweke pembeni, kisha kaanga vitunguu na mafuta mpaka viwe ya brown na kisha uvitie viazi vitunguu, na mafuta yake katika nyama. Koroga na uache uchemke kidogo kisha ipua na utie fresh coriander iliyokatwa na hapo mchuzi wako utakuwa tayari. Baada ya hapo loweka mchele wako kwa muda wa dakika 10, kisha chemsha maji yatie chumvi, hiliki, karafuu, pilipili mtama na abdalasin na mafuta. Yakisha chemka tia mchele na uache uchemke mpaka ukauke maji yakisha kauka tia rangi ya chakula na uanze kugeuza ili ichanganyike na wali wote. Baada ya hapo ufunike na uache mpaka uive. Na baada ya hapo biriani litakuwa tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:46 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Ndizi laini (Matoke 6) Viazi mbatata (potato 3) Samaki wabichi wa wastani ( Fresh tilapia 2) Kitunguu swaum (garlic 6 cloves) Tangawizi (fresh ground ginger vijiko 2 vya chai) Nyanya ya kopo (tin tomato 1/2 kopo) Vitunguu (onion 1) Pilipili (chilli 1 nzima) Chumvi (salt to your taste) Mafuta (vegetable oil) Limao (lemon 1/2) Curry powder (1/2 kijiko cha chai)
Matayarisho
Safisha samaki kisha wakate vipande vitatu. Wakaushe maji kisha wamarinate na kitunguu swaum,tangawizi, chumvi, na limao kwa muda wa masaa 2. baada ya hapo waoke kwenye oven kwa muda wa dakika 30. baada ya hapo andaa ndizi na viazi kwa kuzimenya na kuziosha kisha ziweke pembeni. Kisha katakata vitunguu maji, Tangawizi, vitunguu swaum na nyanya kisha vitie kwenye blenda na usage mpaka mchanganyiko usagike vizuri. Baada ya hapo tia mchanganyiko katika sufuria na ubandike jikoni, acha uchemke mpaka maji yote yakauke. Maji yakisha kauka punguza moto na utie mafuta, curry powder, pilipili na chumvi. Kaangiza mpaka mchanganyiko uive na baada ya hapo tia viazi na maji kiasi na uache viazi vichemke mpaka vikaribie kuiva kisha tia ndizi na samaki na ufunike. Pika mpaka ndizi na viazi viive. Baada ya hapo chakula kitakuwa tayari kwa kuseviwa.
Updated at: 2024-05-25 10:23:10 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Unga - 2 Vikombe
Cocoa ya unga - 1 Kijiko cha supu
Sukari ya hudhurungi - 1 Kikombe
Siagi - ¾ Kikombe
Yai - 1
Molasses - ¼ Kikombe
Baking soda - 2 vijiko vya chai
Mdalasini wa unga - 1 kijiko cha chai
Tangawizi mbichi - 1 kijiko cha supu
Karafuu ya unga - ½ kijiko cha chai
Chumvi ½ kijiko cha chai
Vanilla ½ kijiko cha chai
MAANDALIZI
Katika bakuli, chunga unga, baking soda, chumvi na cocoa. Weka kando. Washa oven lipate moto huku unatayarisha biskuti. Katika bakuli jengine, mimina siagi na sukari upige kwa mashini ya keki hadi mchanganyiko uwe laini kama dakika mbili. Mimina molasses na yai ndani ya mchanganyiko wa siagi na sukari uchanganye vizuri. Mimina unga kidogo kidogo huku unachanganya na mwiko hadi unga wote umalizike. Mimina mdalasini, karafuu na tangawizi, changanya vizuri. Weka mchanganyiko wako ndani ya friji kama masaa mawili. (Ukipenda unaweza kuhifadhi mchanganyiko wako ndani ya mfuko wa freezer na uoke siku nyengine.) Tengeneza viduara vidogo vidogo.
Chovya kila kiduara katikati sukari, kisha panga kwenye treya ya kuoka
Rudisha viduara katika friji kama nusu saa.
Oka katika oven 350ºF kwa muda wa dakika 15.
Toa biskuti kwenye oven na uache zipoe kama dakika kumi. Panga kwenye sahani tayari kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:37:44 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Mahitaji
Mchele (Basmati rice) 1 kilo Vitunguu (chopped onion) 2 vikubwa Garlic powder 1/2 kijiko cha chai Njegere (peas) 1 kikombe Turmaric 1/2 kijiko cha chai Coriander powder 1/2 kijiko cha chai Cumin seeds 1/2 kijiko cha chai Mafuta ya kupikia 2 vijiko vya chakula Chumvi kiasi
Matayarisho
Osha kisha loweka mchele kwa muda wa dakika 5 na kisha uchuje maji na uweke pembeni. Baada ya hapo kaanga vitunguu mpaka viwe vya brown na kisha tia spices zote.Zikaange kwa muda wa dakika 3 kisha tia mchele na uchanganye vizuri na spice.Ukaange mchele pamoja na spice uku ukiwa unageuzageuza kwa muda wa dakika 5. Baada ya hapo tia maji ya moto(kiasi ya kuivisha wali) na chumvi kisha ufunike. Upike mpaka uive kisha malizia kwa kutia njegere na uchanganye vizuri baada ya dakika 2 uipue utakuwa tayari kwa kuliwa.Unaweza kuula kwa mboga yoyote uipendayo
Updated at: 2024-05-25 10:23:06 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
VIAMBAUPISHI
Unga - 4 Vikombe vya chai
Siagi - 1 Kikombe cha chai
Hiliki ½ Kijiko cha chai
VIAMBAUPISHI:SHIRA
Sukari - 2 Vikombe vya chai
Maji - 1 Kikombe cha chai
Vanilla ½ Kijiko cha chai
(cocoa ukipenda kugawa visheti aina mbili) 2 Vijiko vya chai.
JINSI YA KUTENGENEZA
Tia unga kwenye bakuli pamoja na siagi na hiliki. Changanya vizuri isiwe na madonge. Tia maji baridi vikombe viwili kasoro vya chai changanya ukiona bado ongeza maji kidogo, iwe kama chapati usikande uchanganye tu. Halafu utakata sampuli unayopenda mwenyewe. Unaweka karai ya mafuta yakisha kupata moto unaanza kuchoma moto usiwe mkali sana, kiasi, baadae unaweza kuongeza moto na vikaange hadi viwe rangi ya dhahabu, kisha viepue vichuje mafuta. . Ukipenda gawa visheti sehemu mbili, na shira pia igawe sehemu mbili Changanya nusu ya visheti kwa shira nyeupe. Nusu ya shira nyingine ibandike tena motoni na tia cocoa vijiko viwili vidogo vya chai. Inapochanganyika cocoa vizuri changanya nusu ya visheti ulivyogawa kupata visheti vya shira ya cocoa.
Updated at: 2024-05-25 10:34:40 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Vipimo
Ndizi mbichi - 10
Nyama - kilo 1
Nazi ya kopo - 1
Chumvi - 1 Kijiko cha chakula
Ndimu - 1
Bizari ya manjano - 1 Kijiko cha chai
Pili pili mbichi - 3
Nyanya (tomatoes) - 2
Kitunguu maji - 1
Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi iliyosagwa - 1 Kijiko cha chakula
Namna ya Kutayarisha Na Kupika
Kata nyama vipande vipande na uisafishe. Chemsha nyama weka chumvi, thomu, tangawizi na ndimu. Iache iwive. Kata kata nyanya na kitunguu, kisha mimina kwenye nyama inayochemka, weka na bizari nusu kijiko. Wacha supu iwive kisha weka pembeni. Ukumbusho: Hakikisha supu inakuwa kiasi na si nyingi. Menya maganda ndizi na uzikate vipande vipande vya kiasi. Zikoshe ndizi na uziweke ndani ya sufuria. Weka maji ndani ya sufuria kisha zichemshe ndizi mpaka ziwe laini kidogo. Zimwage maji ndizi kisha mimina supu na nyama ndani ya ndizi. Mimina nazi pili pili na bizari nusu kijiko ndani ya ndizi na uziweke kwenye jiko zichemke mpaka zibakie na urojo kiasi. Onja chumvi na uongeze kadri utakavyopenda. Weka pembeni zipoe. Pakua ndizi kwenye sahani au bakuli tayari kwa kuliwa.
Updated at: 2024-05-25 10:34:54 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
Viamba upishi
Unga 2 Magi (kikombe kibuwa cha chai)
Sukari 1/3 Kikombe cha chai Mayai 5
Siagi 4 Vijiko vya chakula
Hamira 1 Kijiko cha chakula
Baking Powder 1 Kijiko cha chai
Vanilla 1 Kijiko cha chai
Hiliki zilizosagwa 1 Kijiko cha chai
Sukari ya laini ya unga
(icing sugar) 1 Magi
Jinsi ya kuandaa na kupika
Unavunja mayai, unatia sukari, hamira, baking powder, vanilla na hiliki ikisha unapiga kwa kutumia mchapo wa kupigia keki. Unapiga mchanganyiko kwa muda wa dakika tano.
Unatia siagi kwenye sufuria na unaiyayusha na kuipasha moto mpaka iwe moto ikisha unaimimina kwenye mchanganyiko na unapiga tena kwa dakika mbili tu.
Unatia unga kwenye sinia au bakuli kubwa ikisha unamimina ule mchanganyiko kwenye unga na unaukanda kutumia mkono, mpaka ulainike.
Ukiona unga mwingi basi ongeza maziwa kidogo mpaka uwe sawa, na ukiona unga mwepesi sana basi unaweza kuongeza unga kidogo pia mpaka ukae sawa mfano wa unga wa maandazi.
Sukuma na ukate madonge kama unavyoyaona hapo juu. Tumia kifuniko cha chupa kwa kukatia kiduara kidogo katikakti ya madonge. Ukimaliza kukata madonge yote, yaweke kidogo yavimbe halafu teleka mafuta na uyachome. Ukitoa kwenye mafuta yachuje moto na kabla ya kupoa yawe moto moto yarovye kwenye icing sugar na uhakikishe yote yameenea sukari juu. Ukimaliza tia kwenye sahani acha zipowe na zitakuwa tayari kwa kuliwa.
Jinsi ya kupika Biskuti Za Kopa Za Kunyunyuziwa Sukari Za Rangi
Updated at: 2024-05-25 10:34:43 (11 months ago by SW - Melkisedeck Shine)
MAHITAJI
Unga vikombe 2 ¼
Siagi 250g
Sukari kukaribia kikombe ½ (au takriban vijiko 10 vya kulia)
Baking powder ½ kijiko cha chai
Ute wa yai 1
Vanilla 1 kijiko cha chai
Sukari Ya Kunyunyizia na rangi mbali mbali.
MATAYARISHO
Kagawa sukari katika vibakuli utie rangi mbali mbali uweke kando. Changanya siagi na sukari katika mashine ya kusagia keki upige mpaka ilainike iwe nyororo. Tia ute wa yai vanilla uhanganye vizuri. Tia unga na baking powder kidogo kidogo uchanganye upate donge. Sukuma donge ukate kwa kibati cha shepu ya kopa. Pakaza siagi katika treya ya kupikia kwenye oveni upange biskuti Nyunyizia sukari za rangi rangi kisha pika katika oven moto mdogo wa baina 180 – 190 deg F kwa takriban robo saa. Epua zikiwa tayari.