Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

ROSARI YA BIKIRA MARIA MAMA WA MSAADA WA DAIMA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Namna ya kusali Rozari kwa Bikira Maria Mama wa Msaada wa Daima

(Tumia rosari ya kawaida)

Mwanzo, kwenye Msalaba:

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

Kwenye chembe ndogo za awali:

K: Ee Mungu utuelekezee msaada W: Ee Bwana utusaidie hima
W: Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu,
Kama mwanzo na sasa na siku zote na milele. Amina.

Maria ametusaidia,
Maria anataka kutusaidia,
Maria anaweza kutusaidia,
Maria atatusaidia.

KATIKA KILA FUNGU SALI SALA ZIFUATAZO:

Kwenye chembe kubwa:

Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu,
Kama mwanzo na sasa, na siku zote, na milele. Amina.

Maria ametusaidia,
Maria anataka kutusaidia,
Maria anaweza kutusaidia,
Maria atatusaidia.

Ee Maria Mama wa Msaada wa daima
Sikiliza maombi ya roho zetu
Unaweza kutusaidia katika mahitaji yetu
Ee Maria kwa matumaini twakuita wewe.

Kwenye chembe ndogo:

Kama unasali mwenyewe: β€œEe Maria, utusaidie! (mara kumi)
Kama mnasali zaidi ya mmoja kwa pamoja: K; Ee Maria, W: Utusaidie. (mara kumi)

MWISHO SALI SALA ZIFUATAZO:

Salamu Maria

Salamu Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu, sasa, na saa ya kufa kwetu. Amina. (mara tatu)

Tunaukimbilia

Tunaukimbilia ulinzi wako, ee Mzazi Mtakatifu wa Mungu, usitunyime tukiomba katika shida zetu, utuokoe siku zote, kila tuingiapo hatarini, ee Bikira Mtukufu na mwenye baraka,. Amina.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Agnes Lowassa Guest Sep 20, 2017
πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha
πŸ‘₯ Anna Malela Guest Sep 6, 2017
πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
πŸ‘₯ John Malisa Guest Aug 23, 2017
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Sarah Karani Guest Aug 19, 2017
πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri
πŸ‘₯ Anna Mahiga Guest Jun 24, 2017
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest Jun 22, 2017
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Samuel Were Guest Mar 25, 2017
πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu
πŸ‘₯ Victor Sokoine Guest Mar 16, 2017
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ John Malisa Guest Jan 3, 2017
πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe
πŸ‘₯ Edith Cherotich Guest Dec 4, 2016
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Bernard Oduor Guest Dec 4, 2016
πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu
πŸ‘₯ Moses Kipkemboi Guest Sep 4, 2016
πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
πŸ‘₯ Anna Mchome Guest Aug 21, 2016
πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest Aug 19, 2016
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Peter Mbise Guest May 10, 2016
πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani
πŸ‘₯ Samuel Omondi Guest Feb 26, 2016
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Alice Jebet Guest Jan 16, 2016
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Diana Mallya Guest Dec 31, 2015
πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua
πŸ‘₯ Robert Okello Guest Oct 8, 2015
πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
πŸ‘₯ John Lissu Guest Jul 31, 2015
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Catherine Mkumbo Guest May 29, 2015
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest May 9, 2015
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Sarah Mbise Guest Apr 17, 2015
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About