Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

SALA YA KUOMBEA FAMILIA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Ewe Mungu Mwenyezi, sisi kama familia tunakushukuru kwa zawadi ya Mama Kanisa Katoliki ambaye siku zote hutupatia malezi bora kwa ajili ya wokovu wetu. Kanisa halichoki kutuhimiza tutafakari na kuishi utakatifu wa familia ya Nazareti ya Yesu, Maria na Yosefu. Familia hii iliishi upendo uliojengwa kwa fadhila za imani, uaminifu, utii, uvumilivu na upole hata wakawa watakatifu. Tunapoadhimisha mwaka wa Familia, tunaiweka mbele yetu familia ya Nazareti iwe dira, baraka na mfano kwa familia zetu.

Tunakushukuru Baba kwa ajili ya familia zote zinazojitahidi kuishi fadhila hizo za Familia takatifu na tunakuomba uzidi kuwaimarisha wanandoa ili tupate kwao mifano mingi na bora ya kuigwa. Ee Bwana, tunaomba Roho Mtakatifu atuangazie tuweze: kutambua familia kuwa Kanisa la nyumbani na shule ya imani na upendo; kuimarisha familia kwa sala, sakramenti na tunu za kiinjili na kushirikiana kwa heshima katika familia kwa usitawi wa roho na wa mwili kwa wanafamilia wote.

Tunaziombea familia zetu na Jumuiya Ndogondogo za Kikristo ziwe bustani bora na salama za kuchipusha na kulea miito mitakatifu ya Ndoa, Utawa na Upadre. Tunawaombea vijana na watoto wetu Uchaji wa Mungu ili wawe na bidii ya kujitunza kwa kushika amri za Mungu na kuishi fadhila za kiinjili, wawe na roho ya kimisionari yaani walipende Kanisa na kuwa na moyo wa kueneza ufalme wako kwa matendo ya imani. Baba wa huruma, tunakukabidhi familia zenye misukosuko ya mafarakano, ulevi, ubinafsi, uregevu-dini, uvivu, ushirikina, hofu, magonjwa sugu na mengineyo yenye kuleta huzuni; kwa hisani yako uwape neema, mwanga na nguvu za kuanza maisha mapya yenye amani, waweze kufurahia upatanisho na uponyi wa pendo lako la kibaba kati yao.

Tunaomba toba na msamaha kwa ukatili, manyanyaso na hata mauaji katika familia zetu na uwaponye wote waliojeruhiwa kwa maneno, matendo na makwazo ya aina yeyote. Aidha tunakuomba uwe kitulizo na faraja kwa wagonjwa na wazee, pia tegemeo la yatima na wajane. Wenye matatizo ya kiafya au ya kijamii wasikate tamaa bali waunganishe hali zao na msalaba wa Mwanao na kukutumaini wewe Mweza yote. Jamii iwajibike nao kwa kuzijali haki zao na kuwapa misaada wanayohitaji.

Tunakuomba ubariki miradi na kazi zetu ili familia zipate usitawi na maendeleo; na utujalie hekima ya kukushukuru kwa maisha ya haki, amani na ukarimu na mwisho tukaimbe sifa zako pamoja na familia Takatifu ya Yesu, Maria na Yosefuna jeshi lote la mbinguni. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.

Baba yetu… …..Salamu Maria….…Atukuzwe Baba………

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Anthony Kariuki Guest Sep 12, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Joseph Kawawa Guest Sep 4, 2017
πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe
πŸ‘₯ Nancy Kabura Guest Jul 12, 2017
πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie
πŸ‘₯ Chris Okello Guest Mar 29, 2017
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest Mar 21, 2017
πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest Mar 14, 2017
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Janet Sumari Guest Jan 10, 2017
πŸ™β€οΈ Mungu akubariki
πŸ‘₯ Simon Kiprono Guest Dec 30, 2016
πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani
πŸ‘₯ Janet Mwikali Guest Jul 26, 2016
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Grace Mushi Guest Jul 11, 2016
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ James Kawawa Guest May 7, 2016
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Charles Mboje Guest Mar 3, 2016
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest Oct 19, 2015
πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose
πŸ‘₯ Grace Majaliwa Guest Oct 3, 2015
πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
πŸ‘₯ Ann Awino Guest Oct 2, 2015
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Nuru Guest Sep 8, 2015
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ David Musyoka Guest Aug 15, 2015
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Grace Mushi Guest Jul 22, 2015
πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu
πŸ‘₯ Grace Minja Guest Jun 17, 2015
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Jun 10, 2015
πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai
πŸ‘₯ Alex Nyamweya Guest May 18, 2015
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest May 16, 2015
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Joseph Mallya Guest Apr 3, 2015
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About