Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/katoliki/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁
AckyShine

SALA YA NOVENA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Ee Moyo Mtakatifu sana wa Yesu, chemchemi ya kila baraka, ninakuabudu, ninakupenda, na kwa majuto halisi ya dhambi zangu, nakutolea moyo wangu dhaifu. Nifanye mnyenyekevu, mvumilivu na safi, nikikubali na kuyatii kabisa mapenzi yako. Ee Yesu mwema, unijalie niishi nawe na kwa ajili yako. Unilinde niwapo katikati ya hatari, unifariji katika mateso, unipe afya ya mwili na msaada katika mahitaji ya mwili, Baraka yako juu ya kila nilifanyalo, na neema ya kifo chema. Amina.

Ee Yesu uliyesema “Kweli nawaambieni, ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtapata, gongeni nanyi mtafunguliwa”, tazama ninagonga, ninatafuta na kuomba …….. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Yesu uliyesema “Kweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu mtapewa”, tazama kwa jina lako ninaomba ……. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Yesu uliyesema “Kweli nawaambieni, mbingu na dunia zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamwe”, tazama, nikitiwa nguvu na maneno yako ya kweli ninaomba …….. (Taja ombi lako)
Baba Yetu….., Salamu Maria …….., Atukuzwe Baba……..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!

Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ambaye kwako ni kitu kimoja tu kisichowezekana, ambacho ni kutoacha kutowaonea huruma wenye huzuni, utuhurumie sisi wakosefu maskini na utujalie neema tukuombayo kwa njia ya Moyo Imakulata wa Maria, Mama yetu mpole.

Sali ‘Salamu Malkia’ na kuongezea, ‘Mtakatifu Yosefu Baba Mlishi wa Yesu, utuombee’.

P.S. – Sala hii ya Novena ilisaliwa kila siku na PADRE PIO kwa ajili ya kuwaombea wale wote waliomwomba msaada wa sala zake. Unaweza kuisali kwa namna tofauti tofauti. Mfano, kama Novena ya siku tisa, ambapo unasali sala hii mara moja au zaidi kila siku kwa siku tisa, au unaweza kuifanya kama Novena ya masaa, ambapo unasali sala hii kila baada ya saa moja kwa masaa tisa kwa siku hiyo hiyo, hasa kama kitu unachokiomba ni cha haraka au umesongwa moyoni. Vilevile unaweza kuifanya sala hii kama sehemu ya sala zako za kila siku katika mwezi Juni ambao ni mwezi uliotengwa na Kanisa kwa ajili ya kuuheshimu Moyo Mtakatifu wa Yesu, na hapo utaitumia kuwaombea watu waliokuomba msaada wa sala zako kama alivyofanya Mtakatifu Padre Pio. Pia unaweza kuitumia kama sala yako ya siku zote au ya mara kwa mara kwa ajili ya mahitaji mbalimbali.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Jackson Makori (Guest) on June 18, 2024

🙏✨❤️ Neema za Mungu zikufunike

Joseph Kitine (Guest) on March 31, 2024

🙏❤️💖 Tumshukuru Mungu kwa yote

Grace Njuguna (Guest) on March 19, 2024

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Nora Kidata (Guest) on September 18, 2023

🙏💖 Asante kwa neema zako Mungu

Mercy Atieno (Guest) on March 25, 2023

Baraka kwako na familia yako.

Catherine Mkumbo (Guest) on March 24, 2023

🙏❤️💖 Bwana akujalie baraka

Hellen Nduta (Guest) on March 20, 2023

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Andrew Odhiambo (Guest) on February 16, 2023

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Alex Nyamweya (Guest) on January 26, 2023

🙏🌟❤️ Nakuombea heri

Mary Njeri (Guest) on January 18, 2023

Tembea kwa imani, si kwa kuona

John Mushi (Guest) on January 16, 2023

🙏🌟 Neema za Mungu zisikose

David Chacha (Guest) on November 26, 2022

🙏💖 Nakusihi Mungu

Edward Lowassa (Guest) on September 26, 2022

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Betty Kimaro (Guest) on September 4, 2022

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Nancy Kawawa (Guest) on September 2, 2022

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Joseph Kitine (Guest) on August 13, 2022

Rehema zake hudumu milele

George Mallya (Guest) on July 24, 2022

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Anna Mchome (Guest) on March 25, 2022

🙏✨ Mungu atakuinua

Joseph Njoroge (Guest) on March 13, 2022

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Faith Kariuki (Guest) on January 8, 2022

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Josephine Nduta (Guest) on January 3, 2022

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Peter Mbise (Guest) on December 7, 2021

Nguvu hutoka kwa Bwana

Joy Wacera (Guest) on October 25, 2021

Katika imani, yote yanawezekana

Mary Njeri (Guest) on October 5, 2021

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Patrick Kidata (Guest) on October 3, 2021

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Andrew Mahiga (Guest) on August 5, 2021

🙏💖 Mungu wetu asifiwe

Rose Waithera (Guest) on July 12, 2021

Mungu akubariki!

Moses Mwita (Guest) on February 24, 2021

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Nora Kidata (Guest) on November 15, 2020

Neema ya Mungu inatosha kwako

Edwin Ndambuki (Guest) on October 6, 2020

🙏✨💖 Mungu atajibu maombi yako

Michael Onyango (Guest) on September 22, 2020

Neema na amani iwe nawe.

Mariam Kawawa (Guest) on September 20, 2020

🙏✨ Neema ya Mungu iwe nawe

Joseph Njoroge (Guest) on September 19, 2020

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Andrew Mahiga (Guest) on September 18, 2020

🙏❤️ Mungu ni mkombozi

Carol Nyakio (Guest) on September 14, 2020

Mwamini katika mpango wake.

Dorothy Mwakalindile (Guest) on August 12, 2020

🙏❤️ Mungu ni mlinzi wetu

Lucy Mushi (Guest) on August 8, 2020

🙏❤️✨ Mungu akujalie furaha

Monica Nyalandu (Guest) on June 11, 2020

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Anna Sumari (Guest) on May 14, 2020

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

John Lissu (Guest) on April 17, 2020

Tumaini ni nanga ya roho

Jane Muthui (Guest) on April 1, 2020

🙏❤️🌟 Asante Mungu kwa uhai

Edith Cherotich (Guest) on March 16, 2020

🙏❤️✨ Asante Mungu kwa kila kitu

Sarah Mbise (Guest) on February 9, 2020

🙏✨ Mungu atupe nguvu

Rose Kiwanga (Guest) on December 2, 2019

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

John Kamande (Guest) on October 1, 2019

Mungu ni mwema, wakati wote!

Hellen Nduta (Guest) on June 17, 2019

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Bernard Oduor (Guest) on June 3, 2019

Amina

Anna Sumari (Guest) on May 15, 2019

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Charles Mrope (Guest) on May 5, 2019

🙏❤️ Mungu akubariki

Rose Lowassa (Guest) on March 13, 2019

🙏💖✨ Neema yako ni ya kutosha

Janet Mbithe (Guest) on December 25, 2018

🙏🌟 Mungu akujalie amani

Linda Karimi (Guest) on December 19, 2018

Sifa kwa Bwana!

Michael Mboya (Guest) on December 3, 2018

Imani inaweza kusogeza milima

Janet Sumari (Guest) on October 26, 2018

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Betty Kimaro (Guest) on April 29, 2018

🙏🌟 Mungu alete amani

Wilson Ombati (Guest) on February 7, 2018

Mwamini Bwana; anajua njia

Henry Mollel (Guest) on December 14, 2017

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Andrew Mahiga (Guest) on November 30, 2017

Endelea kuwa na imani!

John Kamande (Guest) on November 19, 2017

🙏❤️💖 Baraka za Mungu ziwe nawe

Lucy Mushi (Guest) on October 3, 2017

🙏🙏🙏

Related Posts

Malkia wa Mbingu

Malkia wa Mbingu

Malkia wa mbingu, furahi, aleluya. Kwani uliyestahili kumchukua, Aleluya. Amefufuka alivyosema, A... Read More

Sala ya Malaika wa Bwana

Sala ya Malaika wa Bwana

Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria, naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Salamu M... Read More

SALA ZA IBADA KWA BIKIRA MARIA WA MATESO

SALA ZA IBADA KWA BIKIRA MARIA WA MATESO

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo ... Read More

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Novena ya Siku tisa kwa Mtakatifu Agustino wa Hippo: Sala zote na Litania

Anza Novena hii tarehe 19 Agosti ili kumalizia tarehe 27 Agosti na kush... Read More

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

Ee Yesu Kristu,/ Bwana wangu na Mungu wangu/ ambaye ninasadiki kuwa upo hapa/ katika Sakramenti T... Read More

SALA YA JIONI

SALA YA JIONI

TUNAKUSHUKURU, EE MUNGU KWA MAPAJI YOTE ULIYOTUJALIA LEO AMINA


BABA YETU…………... Read More

ROSARI YA BIKIRA MARIA MAMA WA MSAADA WA DAIMA

ROSARI YA BIKIRA MARIA MAMA WA MSAADA WA DAIMA

Namna ya kusali Rozari kwa Bikira Maria Mama wa Msaada wa Daima

(Tumia rosari ya kawaida... Read More

ATUKUZWE BABA

ATUKUZWE BABA

Atukuzwe Baba
na Mwana
na Roho Mtakatifu
Kama mwanzo
na sasa,
na siku zo... Read More

SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu, utulinde katika vita, uwe kinga yetu katika maovu na maoteo ya sh... Read More

Sala za kuheshimu Damu Takatifu ya Yesu

Sala za kuheshimu Damu Takatifu ya Yesu

Tusali kila siku sala hizi, angalau kwa mwezi wa saba (Julai) kila mwaka, mwezi wa kuhesh... Read More

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

Kwa nguvu zangu zote za moyo wangu/ ninakuabudu ee Moyo Mtakatifu/ na Mwabudiwa sana,/ Moyo Mtaka... Read More

SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE

SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE

Ee Mama mbarikiwa na Bikira mwenye uchungu, Malkia wa Mashahidi, uliyesimama chini ya msalaba na ... Read More

📖 Explore More Articles