Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁

Kwa nini tarehe ya Pasaka hubadilika

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
KALENDA za mwanzo ziliutumia mwezi wa angani kama kipimo cha muda. Ziliitwa “Lunar calender” au Kalenda-Mwezi. Tarehe 1 ya Mwezi ilikuwa ni siku ulipoandama yaani Mwezi-Mdogo (Crescent Moon). Mwezi unapofika siku ya 15 unakuwa umefikia ukubwa wa juu na huitwa Mwezi- Mkubwa (Full Moon). Hivyo kwa kalenda ile tarehe 15 ilikuwa ni siku ya Mwezi-Mkubwa. Mwaka 45KK, Julius Caesar alitangaza kalenda mpya ikaitwa “Julian Calender” iwe na siku 365. Wakati huo ikijulikana kwamba jua huzunguka kwa siku 365.25. Hivyo pengo la kalenda na mzunguko likabaki robo siku. Robo hiyo ifidiwe kila baada ya miaka minne mwishoni mwa mwezi Februari ambayo sasa ulifanywa kuwa wa pili baada ya January. Inapofanyika hivyo, huo ukaitwa mwaka- mrefu (Leap year). Mwaka mrefu ukachaguliwa kuwa ni ule tu unaogawanywa kwa nne mfano miaka ifuatayo 1700, 1800, 1900, 2100, 2200, 2300. Baadaye iligundulika kuwa jua huzunguka kwa siku 365.24218967 ziitwazo “Tropical year”. Hizi ni chache kuliko siku 365.25 zilizokadiriwa mwanzoni. Uchache huu husababisha kuwe na pengo la dakika 11 na sekunde 14.812512 kwa mwaka. Pengo hili ni dogo, lakini hupanuka hadi kuwa siku nzima kila baada ya miaka 128.0355. Mwaka 1545 lilivuka siku 9.25. Kuondoa tatizo hili, Papa Gregory XIII aliamuru iundwe kalenda mpya na akachagua Oktoba 04, 1582 iwe siku ya mwisho kutumika “Julian Calender”. Kesho yake, kalenda mpya ikaanza kutumika. Ungetegemea hiyo kesho iwe ni Oktoba 05, 1582. Lakini ili uzibe pengo lile lililofikia siku kumi, ilibidi kalenda mpya kuziruka siku hizo siku kumi. Hivyo hii mpya iliyoitwa “Gregorean Calender” ikaanza kama Oktoba 15 badala ya Oktoba 05. Ndiyo sababu katika historia ya nchi nyingi Ulaya, hakuna tarehe za Oktoba 05, 1582 hadi Oktoba 14, 1582. Watu walilala Oktoba 04, 1582 kesho yake wakaamka ikiwa ni Oktoba 15, 1582. Teresa Alonso huandikwa kwamba alifariki Oktoba 1582, kwenye usiku wa tarehe NNE kuamkia tarehe KUMI NA TANO! Alipotangazwa kuwa Mtakatifu, Kanisa Katoliki likaifanya Oktoba 15 kuwa siku ya kumkumbuka, yaani siku ya Mtakatifu Teresa wa Avila. Usipofahamu kwamba Mtakatifu Teresa alifariki siku kalenda zinabadilishwa, utadhani aliyeandika vile tarehe za kifo chake amekosea! Waandishi, William Shakespeare wa Uingereza na Miguel de Cervantes wa Spain huandikwa kwamba wote walifariki Aprili 23, 1616. Lakini ukweli ni kwamba hawakufa siku moja bali walipishana siku kumi kwani England ilichelewa kwa karibu miaka 200 kuikubali “Gregorean Calender”! “Gregorean Calender” haikuundwa ili kuishia kuliziba lile pengo. Bali pia, kuhakikisha halitokei tena. Tumeshaona kuwa lile pengo ni dakika 11 na sekunde 14.812512. Hivyo, linapanuka na kuwa siku tatu ndani ya miaka 400. Hivyo kuliziba inatakiwa kupunguza siku tatu kila baada ya miaka 400.

Je, zipunguzweje?

Kipande cha miaka 400 kina miaka mitatu ya karne inayogawanyika kwa 4 lakini haigawanyiki kwa 400. Ikakubalika kwamba unaogawanyika kwa 4, lakini haugawanyaiki kwa 400, usiendelee kuwa mrefu. Humo siku moja ichomolewe na uwe mfupi. Ndipo miaka 1700, 1800, 1900 haikuwa tena mirefu. Ndivyo pia miaka 2100, 2200, 2300 nayo haitakuwa mirefu. Kwa sababu ni miaka ambayo “Gregorean Calender” inachomoa siku moja ili kutosababisha pengo tena. Kipande hiki cha miaka 400 kikaleta wastani mpya wa siku 365.2425 kwa mwaka. Sasa lile pengo lile la siku moja si rahisi kufikiwa. Kwenye “Julian Calender” tumeona lilikuwa miaka 128.0355 lakini sasa limekuwa miaka 3,222. Sasa tuijadili tarehe ya siku ya Pasaka tukiwa na ufahamu wa kalenda zile. +++ Je, tarehe ya Pasaka imetajwa ndani ya Biblia? Kuna kifungu kinasema hivi: “..Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi, wakati wa jioni, ni Pasaka ya BWANA. Na siku ya kumi na tano ya mwezi huohuo ni sikukuu ya BWANA, ndiyo siku ya mikate isiyotiwa chachu. (Walawi 23:5)..”. Hivyo Pasaka ni tarehe 15 ya mwezi wa Kwanza. Lakini Biblia pia inautaja mwezi wa kwanza kwa jina la Nisan (Esta 3:7, Nehemia 2:1). Yesu alisulubiwa mwaka ambao Ijumaa iliitangulia sikukuu ya Pasaka kwa siku moja (Yohana 18: 28, Marko 15:42-43). Hivyo tarehe ya Yesu kusulubiwa ni Ijumaa, Nisan 14. Siku moja kabla ya Nisan 15. Siku moja kabla ya Mwezi-Mkubwa. Baada ya Yesu, Wakristo wengi Pasaka waliiadhimisha Jumapili, lakini utata ulijitokeza kuhusu tarehe ya kuiweka hiyo Jumapili ya Pasaka. Ilifika wakati jimbo moja la Wakristo linaadhimisha siku tofauti na jingine na kwa njia wanayoijua wao. Utata huu uliondolewa kule Nicaea mwaka 325 ambapo Kanisa Katoliki lilipoamua kuwa, tarehe ya Pasaka iwe moja tu duniani kote, yaani iwe ni Jumapili inayokuja baada ya Mwezi-Mkubwa (Full Moon) unaotokea baada ya siku ya Ikweta, yaani baada ya Machi 21 (Equinox). Baada ya uamuzi huu, wataalamu walipania kuunda chati maalum zenye tarehe za Mwezi- Mkubwa zitazokasaidia kuitambua tarehe ya Pasaka kwa mwaka wowote. Mwezi huizunguka dunia kwa siku 29.5305891203704 (Synodic Month), wakati dunia hulizunguka jua kwa siku 365.24218967 (Tropical year). Mizunguko hii miwili ikianza safari siku moja, itapishana kila mwaka, lakini itakutana tena mwezi unapokamilisha mizunguko 235. Dunia nayo inakuwa imekamilisha mizunguko 19, yaani miaka 19. Wataalamu wakaitumia hii miaka 19 kutengeneza chati yenye tarehe za Mwezi- Mkubwa unaotokea March 22 hadi April 18. Tarehe zile zikaitwa tarehe za Mwezi- Mkubwa Wa Pasaka au Ecclesiastical Full Moon (EFM). Ndani ya ile miaka 19, kila mwaka ukapewa tarakimu iitwayo Golden Number inayosimama badala ya mwaka ikiwa na tarehe zile ziliorekodiwa za Mwezi Mkubwa wa Pasaka. Chati yenyewe ya Golden Number na tarehe zake (siku/Mwezi) ni hii ifuatayo: {1=5/4, 2=25/3, 3=13/4, 4=2/4, 5=22/3, 6=10/4, 7=30/3, 8=18/4, 9=7/4, 10=27/3, 11=15/4, 12=4/4, 13=24/3, 14=12/4, 15=1/4, 16=21/3, 17=9/4, 18=29/3, 19=17/4} Golden Number ya mwaka inapatikana kuanza kuugawa mwaka kwa 19. Tulifundishwa mashuleni kuwa namba inayosalia baada ya kugawa huitwa “Baki” . Hii “Baki” ukiijumlisha na 1 unapata Golden Number (GN). Mfano unatafuta GN ya 27. Hatua ya kwanza ni kutafuta “Baki” baada ya kugawa 27 kwa 19. Hizi ni hesabu za “modulo” , yaani zinahitaji tu namba inayobaki baada ya kugawa. Ikiandikwa hivi: (27 mod 19) inatakiwa namba inayobaki baada ya kuigawa 27 kwa 19. Jibu ni 8. Hivyo tulipaswa tuandike hivi: (27 mod 19=8). “Baki” 8 tuliyoipata, ndiyo tunaihitaji ili tuijumlishe na 1 ili tupate GN ambayo hapa ni 9 kwani (8+1=9). Tungeweza pia kuandika hivi : 27 mod 19 + 1=9. Hivyo kanuni ya kupata GN kwa mwaka wowote ni hii: (MWAKA mod 19 + 1). Yaani, ugawe huo mwaka kwa 19, kisha namba itakayobaki ijumlishe na moja. Ukishaipata GN, itafute kwenye ile chati ambapo utaiona ikiwa na mwezi na tarehe. Jumapili inayofuata baada ya tarehe hii ndiyo tarehe ya Pasaka ya mwaka huo. Tutumie chati ile na kanuni hii kujua tarehe ya Pasaka ya mwaka 1474. GN ni (1474 mod 19 + 1=12). Hivyo GN ni 12. Kwenye chati, 12 inaonyesha ni tarehe 4/4. Hivyo, mwaka 1474 Mwezi-Mkubwa wa Pasaka ulikuwa tarehe 4/4/1474. Hiyo ilikuwa ni Jumatatu. Hivyo Pasaka ilikuwa ni Jumapili iliyofuata yaani tarehe 10/4/1474. Lakini, Kanisa Katoliki liliikubali kanuni hii karne ya sita. Hii ndiyo sababu, tarehe za Pasaka zinazojulikana ni zile tu zinazoanza mwaka 533. Ndivyo Pasaka ilivyotafutwa miaka ile. Sasa tuone Pasaka ya kizazi chetu. Kizazi cha “Gregorean Calender” iliyoanza mwaka 1582. Tumelijadili lile pengo la siku lililofikia ambalo mwaka 1582 lilishafika siku 10. Ukweli ni kwamba kabla halijazibwa, Pasaka ilikuwa inawadia lakini uhalisi ni kwamba inakuwa tayari imepitwa siku 10. Kinyume kabisa na maamuzi ya Kanisa kule Nicaea! Ili kulizuia lisitokee tena, tumeona uchomoaji wa siku moja toka kwenye miaka inayofunga karne, isiyogawanyika kwa 400. Uchomoaji huu umewekwa kwenye kanuni (formula) iitwayo “Solar Equation”. Kama mwendo wa kuzunguka jua umezingatiwa na “Gregorean Calender”, vipi kuhusu mwendo wa mwezi? Tumeuona kwamba mizunguko ya mwezi na dunia hukutana kila baada ya miaka 19. Kadirio la dunia kuzunguka kwa siku 365.25 linafanya ikizunguka kwa miaka 19 zinakuwa siku 6,939.75. Mwezi utakuwa nao umezunguka mara 235, huku kila mzunguko ukitumia siku 29.5305891203704. Hivyo, kukutana kule ndani ya kila miaka 19, huleta pengo dogo la saa 1, dakika 28, sekunde 38.5. Mapengo madogo haya tunayoyapuuza mwanzoni, yameshatugharimu vya kutosha. Pengo hili kwa mwaka ni dogo lakini kwa miaka 2500 linakuwa hadi kufika siku nane. Kwenye hesabu za kutafuta Pasaka urekebishaji wa hili pengo hutokea kwenye kanuni iitwayo “Lunar Equation”. Lakini kwa sababu ya tofauti ya uelekeo wa mzunguko wa mwezi na dunia, “Lunar Equation” hujumlisha mara nane kila baada ya miaka 2500. Hivyo, mahesabu yoyote ya kuitafuta tarehe ya Pasaka hayakosi kanuni hizi mbili “Solar Equation” na “Lunar Equation” . Tumeona kwamba kalenda ilianza mwaka 1582. “Solar Equation” inaondoa siku moja toka kwenye miaka 1700, 1800, 1900. Hivyo, ni kujidanganya kusema kwamba miaka yote inayogawanyika kwa nne ni mirefu, jambo ambalo hata mimi nilifundishwa shuleni. Hapa tumeona kwamba “Solar Equation” imeondoa siku moja kwenye mwaka 1900 na hivyo haukuwa mwaka mrefu ingawa unagawanyika kwa nne. “Lunar Equation” huongeza siku moja kwenye miaka 1800, 2100, 2400. Mwaka 1800 unaguswa na vyote “Solar Equation” na “Lunar Equation”. Hivyo hauathiriki. Kanuni zote za kuitafuta Pasaka huzingatia zaidi ya niliyoyaeleza, lakini cha muhimu zaidi ni hizi mbili yaani “Solar Equation” na “Lunar Equation” ambazo sijawahi kuzisikia kwa kiswahili. Ni vigumu kuepuka hesabu za “modulo” au “mod” unapotafuta tarehe ya Pasaka. Lakini ukiwauliza wanafunzi wa darasa la nne kwamba machungwa 2011 yakipangwa kwenye mafungu 19, ni mangapi yatakosa fungu? Wapo watakaopata jibu sahihi kwamba ni machungwa 16. Kimahesabu swali hilo linaandikwa hivi: (2011 mod 19) na jibu lake ni 16, yaani (2011 mod 19=16). Ifuatayo ni moja ya kanuni zinazotumika kuipata tarehe za Pasaka ya mwaka wowote kuanzia 1700 hadi 2099: (1) : a=MWAKA mod 19; (2) : b=MWAKA \ 100; (3) : c=MWAKA mod 100; (4) : d=b \ 4; (5) : e=b mod 4; (6) : f=c \ 4; (7) : g=c mod 4; (8) : h=(b + 8)\25; (9) : i=(b – h + 1)\3; (10) : j=(19xa + b – d – i + 15) mod 30; (11) : k=(32 + 2xe + 2xf – j – g) mod 7; (12) : m=(a + 11xj + 22xk) \ 451; (13) : n=j + k – 7xm + 114; (14) : Tarehe=(n mod 31) + 1 (15) : Mwezi =n\31; Penye neno MWAKA, andika mwaka unaotafuta kujua tarehe yake ya Pasaka. Panapotokea alama (\) ni kugawanya ambako hata kama jibu litaleta desimali, basi hiyo desimali unatakiwa kuachana nayo ili jibu libaki namba nzima. Penye alama (x) hiyo ni ya kuzidisha. Yafuatayo ni majibu niliyopata kwa hatua zote baada ya kuuingiza mwaka 2015 ili kujua siku ya Pasaka ya mwaka huu: (1): 1, (2): 20, (3): 15, (4): 5, (5): 0, (6): 3, (7): 3, (8): 1, (9): 6, (10): 13, (11): 1, (12): 0, (13): 128, (14): 5, (15): 4. Tarehe imepatikana kwenye hatua ya 14 ambako jibu ni “5”. Mwezi umepatikana kwenye hatua ya 15 ambako jibu ni “4”. Hivyo Pasaka ya mwaka (2015) huu ni Tarehe 5, mwezi wa 4. Hivyo, kwa njia hii, unaweza kujua tarehe za Pasaka kwa miaka ijayo kama unavyoijua tarehe ya Krismas. Kama kuna tukio lilifanyika siku ya Pasaka miaka iliyopita na hukumbuki tarehe, basi tumia kanuni hii. Zifuatazo ni siku zinazoitangulia Pasaka kwa idadi ya siku zilizoandikwa kwenye mabano: Jumatano Ya Majivu (46), Jumapili ya Matawi (7), Ijumaa Kuu (2). Zinazotanguliwa na Pasaka ni hizi zifuatazo: Kupaa (42), Pentekoste (49), Utatu Mtakatifu (56), Ekaristi (63). Mwanzo tuliona kwamba Mwezi-Mkubwa wa Pasaka au “Ecclesiastical full Moon” ni ule wa March 22 hadi April 18. Ukitokea March 22 basi kuna uwezekano siku hiyohiyo ikawa Pasaka na ikawa imevunja rekodi ya kuwahi mapema. Ukitokea April 18, kuna uwezekano wa Pasaka kuwa siku saba zaidi ya hapa yaani April 25, na hiyo ikawa ni tarehe ya juu mno ya Pasaka. Hivyo, Pasaka yoyote haiwezi kuwa chini ya Machi 22, wala haiwezi kuwazaidi ya April 25. Pasaka tuliyoiona mwaka 2008 ndiyo ya mwisho kwa kizazi chetu kuiona ikiwahi mapema kiasi kile, kwani ilitokea Machi 23 na itairudia tena tarehe hiyo mwaka 2160! by JOSEPH MAGATA
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
👥 Thomas Mwakalindile Guest Jun 8, 2024
Imani inaweza kusogeza milima
👥 Michael Mboya Guest May 26, 2024
Sifa kwa Bwana!
👥 Edward Lowassa Guest Feb 1, 2024
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
👥 James Malima Guest Dec 18, 2023
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
👥 Joseph Kawawa Guest Dec 11, 2023
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
👥 Lydia Mahiga Guest Nov 27, 2023
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
👥 John Lissu Guest Oct 1, 2023
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
👥 Irene Akoth Guest Jul 2, 2023
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Ann Wambui Guest Mar 11, 2023
Mungu ni mwema, wakati wote!
👥 Vincent Mwangangi Guest Feb 19, 2023
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
👥 Francis Mrope Guest Oct 18, 2022
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
👥 David Musyoka Guest Jun 11, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
👥 Peter Mwambui Guest Apr 6, 2022
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
👥 Michael Onyango Guest Jan 24, 2022
Tumaini ni nanga ya roho
👥 Simon Kiprono Guest Sep 16, 2021
Endelea kuwa na imani!
👥 Anna Mchome Guest May 27, 2021
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
👥 Benjamin Kibicho Guest Apr 30, 2021
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
👥 Agnes Lowassa Guest Apr 6, 2021
Tembea kwa imani, si kwa kuona
👥 Lucy Kimotho Guest Feb 8, 2021
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
👥 Richard Mulwa Guest Feb 4, 2021
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
👥 Tabitha Okumu Guest Aug 31, 2020
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
👥 Grace Njuguna Guest Aug 27, 2020
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
👥 James Malima Guest May 11, 2020
Rehema hushinda hukumu
👥 Anna Mchome Guest Apr 11, 2020
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
👥 Fredrick Mutiso Guest Apr 4, 2020
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
👥 Esther Nyambura Guest Mar 11, 2020
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
👥 Peter Mugendi Guest Feb 18, 2020
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
👥 Alex Nakitare Guest Jan 29, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
👥 Alice Wanjiru Guest Jun 25, 2019
Mwamini katika mpango wake.
👥 Lydia Mahiga Guest Mar 10, 2019
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
👥 Charles Mchome Guest Jan 6, 2019
Katika imani, yote yanawezekana
👥 David Nyerere Guest Dec 16, 2018
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
👥 Mariam Kawawa Guest Aug 29, 2018
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
👥 Samuel Were Guest Aug 8, 2018
Dumu katika Bwana.
👥 Anthony Kariuki Guest Mar 18, 2018
Neema na amani iwe nawe.
👥 Mary Mrope Guest Oct 28, 2017
Wakati wa Mungu ni kamilifu
👥 Frank Sokoine Guest Sep 4, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
👥 Sharon Kibiru Guest Aug 11, 2017
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
👥 John Mwangi Guest Aug 1, 2017
Nguvu hutoka kwa Bwana
👥 Elizabeth Mrema Guest Jul 24, 2017
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
👥 Lydia Mutheu Guest May 19, 2017
Mwamini Bwana; anajua njia
👥 Samuel Omondi Guest Jul 17, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Charles Mrope Guest Jul 12, 2016
Kwa Mungu, yote yanawezekana
👥 Nora Lowassa Guest Jun 8, 2016
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
👥 David Chacha Guest Jan 9, 2016
Nakuombea 🙏
👥 Ann Wambui Guest Oct 27, 2015
Mungu akubariki!
👥 Anna Mahiga Guest Aug 24, 2015
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
👥 Violet Mumo Guest Aug 18, 2015
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
👥 Patrick Mutua Guest Apr 25, 2015
Rehema zake hudumu milele
👥 Grace Mligo Guest Apr 19, 2015
Baraka kwako na familia yako.

🔗 Related Posts

🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About