Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁

Ishi kama Penseli ili uwe mtu bora

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Muumbaji wa penseli alipomaliza kuiumba penseli yake aliiambia mambo muhimu ya kuzingatia ili iweze kuwa penseli bora kabla hajaituma kuingia kazini kwa matumizi.

“Kuna vitu sita unatakiwa uvitambue, “ Aliiambia penseli,

“Kabla sijakutuma kwenda kutumika, unatakiwa uviweke akilini vitu hivyo na usivisahau kamwe. Vitakusaidia siku zote na utakuwa penseli bora maisha yako yote.”

Alisema muumbaji wa penseli.

“Moja,” alianza kuvitaja,”utakuwa na uwezo wa kufanya vitu vingi, lakini kama utakubali na utaruhusu kuongozwa na mkono wa mtumiaji wako”

“Mbili” aliendelea kutoa nasaha, “utapata maumivu makali kutokana na kuchongwa mara kwa mara. Lakini vumilia kwani itakusaidia kuwa penseli bora na kuandika vizuri.”

“Tatu, utakuwa na uwezo wa kusahihisha makosa utakayo yafanya.”

“Nne, kitu pekee cha muhimu katika maisha yako ni kile kilicho ndani yako kwa sababu ndicho chenye uwezo wa kuandika.”

“Tano” alisisitiza mtengenezaji penseli, “kwenye kila sehemu utakayotumika, utaacha alama yako. Hata ikiwa ni kwenye sehemu ngumu au mbaya kiasi gani, ni lazima alama yako ibaki.

“Na sita”, alimalizia muumbaji yule wa penseli, “ipo siku utaisha na kupotea. Hivyo usiwe na hofu wala woga wala hudhuni uikaribiapo siku hiyo na ukaogopa kutimiza wajibu wako kwa kuhofia kuisha. Ukiogopa kuisha hautotumika na umuhimu wako hautonekana kwani hautatimiza wajibu uliombiwa kuufanya”

Penseli ilielewa na kuahidi kukumbuka na ikaingia sokoni ikiwa na dhamira yake moyoni.

Sasa tutumie mfano huo wa penseli katika maisha yetu halisi. Ukivikumbuka vitu hivyo sita ilivyopewa penseli, utaweza kuwa mtu bora kabisa kwenye maisha yako yote.

Moja, una uwezo wa kufanya mambo mengi na makubwa, kama utajiweka kwenye mikono ya Mungu.

Mbili, utakutana na magumu mengi ya kuumiza, lakini hayo ndiyo yatakufanya uwe mtu imara na bora, usiyakimbie.

Tatu, una uwezo wa kurekebisha makosa yote uliyoyafanya. Usijilaumu.

Nne, sehemu yako ya muhimu ni ile iliyo ndani yako kwani ndiyo inayoandika maisha yako. Ilinde.

Tano, kila sehemu utakayopita, acha alama yako kwa kufanya mazuri yatakayokufanya ukumbukwe daima, bila kujali mazingira. Timiza wajibu wako kwa kiwango cha juu.

Sita, tambua kuwa ipo siku utakufa. Usiwe na hofu yoyote juu ya kifo kwani ukiogopa kifo hutafanya lolote hapa duniani.

Tumia mfano huu wa penseli upate ujasiri wa kutambua kuwa wewe ni mtu muhimu hapa duniani na umeumbwa kwa madhumuni maalumu na umepewa uwezo mkubwa sana na Muumba wako! Ni wewe pekee mwenye uwezo wa kutimiza dhamira uliyotumwa na Muumba.

UBARIKIWE SANA.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
👥 Grace Minja Guest Apr 16, 2024
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
👥 James Kimani Guest Jul 25, 2023
Rehema hushinda hukumu
👥 Violet Mumo Guest Jul 10, 2023
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
👥 Edward Lowassa Guest Jun 20, 2023
Nakuombea 🙏
👥 Joyce Mussa Guest Dec 25, 2022
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
👥 David Sokoine Guest Apr 13, 2022
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
👥 Henry Mollel Guest Oct 19, 2021
Mwamini Bwana; anajua njia
👥 Andrew Mahiga Guest Oct 7, 2021
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
👥 Peter Mwambui Guest Aug 6, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 John Lissu Guest Jun 1, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
👥 Diana Mumbua Guest Apr 22, 2021
Endelea kuwa na imani!
👥 Nancy Kabura Guest Apr 11, 2021
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
👥 Richard Mulwa Guest Sep 17, 2020
Mungu ni mwema, wakati wote!
👥 Edward Lowassa Guest Jul 2, 2020
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
👥 James Mduma Guest Jul 1, 2020
Mwamini katika mpango wake.
👥 Martin Otieno Guest Jun 26, 2020
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
👥 Rose Amukowa Guest Feb 22, 2020
Wakati wa Mungu ni kamilifu
👥 Samson Tibaijuka Guest Jan 11, 2020
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
👥 Martin Otieno Guest Jan 9, 2020
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
👥 Richard Mulwa Guest Nov 25, 2019
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
👥 Charles Mboje Guest Jul 25, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
👥 Raphael Okoth Guest May 16, 2019
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
👥 Sarah Karani Guest May 6, 2019
Tembea kwa imani, si kwa kuona
👥 Lydia Mzindakaya Guest Feb 2, 2019
Dumu katika Bwana.
👥 Benjamin Masanja Guest Jan 19, 2019
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
👥 John Malisa Guest Dec 2, 2018
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
👥 Samuel Omondi Guest Sep 12, 2018
Kwa Mungu, yote yanawezekana
👥 Thomas Mwakalindile Guest Aug 11, 2018
Baraka kwako na familia yako.
👥 Elizabeth Malima Guest May 21, 2018
Neema na amani iwe nawe.
👥 Simon Kiprono Guest Jan 25, 2018
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
👥 Alice Jebet Guest Nov 20, 2017
Katika imani, yote yanawezekana
👥 John Lissu Guest Oct 30, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
👥 Jane Muthoni Guest Sep 23, 2017
Sifa kwa Bwana!
👥 Andrew Mahiga Guest Jun 3, 2017
Rehema zake hudumu milele
👥 Diana Mumbua Guest Feb 24, 2017
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
👥 Michael Onyango Guest Nov 29, 2016
Mungu akubariki!
👥 Betty Kimaro Guest Sep 29, 2016
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
👥 Paul Kamau Guest Sep 23, 2016
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
👥 Joseph Kitine Guest Jun 8, 2016
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
👥 John Lissu Guest Jun 4, 2016
Neema ya Mungu inatosha kwako
👥 Irene Akoth Guest May 15, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
👥 Peter Mugendi Guest May 6, 2016
Nguvu hutoka kwa Bwana
👥 Betty Kimaro Guest Mar 17, 2016
Tumaini ni nanga ya roho
👥 Nicholas Wanjohi Guest Feb 28, 2016
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
👥 Grace Wairimu Guest Jan 10, 2016
Imani inaweza kusogeza milima
👥 Samuel Were Guest Nov 5, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Nicholas Wanjohi Guest Aug 10, 2015
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
👥 Chris Okello Guest May 7, 2015
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
👥 Esther Cheruiyot Guest May 6, 2015
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
👥 Moses Kipkemboi Guest Apr 14, 2015
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

🔗 Related Posts

🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About