Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA, JUMAPILI JULAI 25 2021: DOMINIKA YA 17 YA MWAKA B WA KANISA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

2 Wafalme:4.42

Alikuja mtu kutoka Baal-shalisha, akamletea mtu wa Mungu chakula cha malimbuko, mikate ishirini ya shayiri, na masuke mabichi ya ngano guniani. Akasema, Uwape watu, ili wale. Na mtumishi wake akasema, Je! Niwaandikie hiki watu mia? Lakini akasema, Uwape watu, ili wale; kwa kuwa Bwana asema hivi, Watakula na kusaza. Basi akawaandikia, nao wakala, wakasaza, sawasawa na neno la Bwana.

WIMBO WA KATIKATI

1. Ee Bwana, kazi zako zote zitakushukuru, Na wacha Mungu wako watakuhimidi. Wataunena utukufu wa ufalme wako, Na kuuhadithia uweza wako. (K)

Waufumbua mkono wako, wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake.

2. Macho ya watu yakuelekea Wewe, Nawe huwapa chakula chao wakati wake. Waufumbua mkono wako, Wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake. (K)

3. Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, Na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote. Bwana yu karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu.

SOMO 2

Waefeso:4.1 - 6

Nawasihi, mimi niliye mfungwa katika Bwana, mwenende kama inavyoustahili wito wenu mlioitiwa; kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo; na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani. Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu. Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote.

SHANGILIO

Yohana:14.6

Aleluya Aleluya!

Mimi ndimi njia, na ukweli, na uzima, asema Bwana; Mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. Aleluya

INJILI

Yn. 6:1-15

Yesu alikwenda zake ng'ambo ya Bahari ya Galilaya, nayo ndiyo ya Tiberia. Na mkutano mkuu wakamfuata, kwa sababu waliziona ishara alizowafanyia wagonjwa. Naye Yesu akakwea mlimani, akaketi huko pamoja na wanafunzi wake. Na Pasaka, sikukuu ya Wayahudi, ilikuwa karibu. Basi Yesu alipoinua macho yake akaona mkutano mkuu wanakuja kwake, alimwambia Filipo, Tununue wapi mikate, ili hawa wapate kula? Na hilo alilinena ili kumjaribu; kwa maana alijua mwenyewe atakalotenda. Filipo akamjibu, Mikate ya dinari mia mbili haiwatoshi, kila mmoja apate kidogo tu. Wanafunzi wake mmojawapo, Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia, Yupo hapa mtoto, yuna mikate mitano ya shayiri na samaki wawili, lakini hivi ni nini kwa watu wengi kama hawa? Yesu akasema, Waketisheni watu. Na mahali pale palikuwa na majani tele. Basi watu waume wakaketi, wapata elfu tano jumla yao. Basi Yesu akaitwaa ile mikate, akashukuru, akawagawia walioketi; na kadhalika katika wale samaki kwa kadiri walivyotaka. Nao waliposhiba, aliwaambia wanafunzi wake, Kusanyeni vipande vilivyobaki, kisipotee cho chote. Basi wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili, vipande vya mikate mitano ya shayiri vilivyowabakia wale waliokula. Basi watu wale, walipoiona ishara aliyoifanya, walisema, Hakika huyu ni nabii yule ajaye ulimwenguni. Kisha Yesu, hali akitambua ya kuwa walitaka kuja kumshika ili wamfanye mfalme, akajitenga, akaenda tena mlimani yeye peke yake.

Neno la Bwana..... Sifa Kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Elizabeth Mrema Guest Jul 14, 2024
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Dorothy Majaliwa Guest Jul 5, 2024
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Nora Kidata Guest Jul 4, 2024
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ John Lissu Guest Jun 22, 2024
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Peter Mugendi Guest Apr 25, 2024
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Sarah Achieng Guest Dec 16, 2023
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Mary Kendi Guest Dec 9, 2023
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Martin Otieno Guest Nov 22, 2023
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Monica Adhiambo Guest Oct 15, 2023
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest Sep 23, 2023
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Lucy Mahiga Guest Sep 6, 2022
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Dorothy Nkya Guest Aug 27, 2022
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Janet Mwikali Guest Apr 30, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Janet Sumaye Guest Dec 20, 2021
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Jackson Makori Guest May 12, 2021
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ David Nyerere Guest May 11, 2021
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest May 2, 2021
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Moses Mwita Guest Mar 29, 2021
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest Feb 5, 2021
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest Dec 28, 2020
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Joyce Nkya Guest Oct 26, 2020
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Janet Mwikali Guest Oct 23, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Victor Malima Guest Sep 16, 2020
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Joyce Mussa Guest Jul 4, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Dorothy Majaliwa Guest Apr 22, 2020
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Edith Cherotich Guest Oct 27, 2019
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Patrick Akech Guest Sep 4, 2019
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Jane Muthui Guest Aug 31, 2019
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Victor Mwalimu Guest Feb 12, 2019
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Jane Muthoni Guest Nov 9, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Ann Awino Guest Oct 19, 2018
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Joseph Mallya Guest Aug 8, 2018
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ John Mushi Guest Jul 21, 2018
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Paul Kamau Guest Apr 22, 2018
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Robert Ndunguru Guest Mar 7, 2018
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Robert Okello Guest Jan 4, 2018
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ John Mushi Guest Nov 27, 2017
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Sarah Mbise Guest Jun 6, 2017
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Irene Makena Guest Mar 4, 2017
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Diana Mallya Guest Feb 16, 2017
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Elizabeth Mtei Guest Dec 14, 2016
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Isaac Kiptoo Guest Dec 13, 2016
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ John Lissu Guest Oct 29, 2016
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ David Sokoine Guest Oct 10, 2016
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Susan Wangari Guest Aug 15, 2016
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Mary Kendi Guest Aug 13, 2016
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Linda Karimi Guest Mar 4, 2016
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Grace Wairimu Guest Mar 2, 2016
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest Jan 12, 2016
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Grace Minja Guest Oct 19, 2015
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About