Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

MASOMO YA MISA, MACHI 19, 2022: JUMAMOSI, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SHEREHE YA MT. YOSEFU, MUME WA BIKIRA MARIA

SOMO 1

2Sam. 7: 4 โ€“ 5, 12 โ€“ 14, 16

Ikawa usiku uo huo, neno la Bwana likamfikia Nathani kusema, Enenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, Bwana asema hivi, siku zako zitakapo timia, ukalala na Baba zako, nitainua mzao wako nyuma yako, atakayetoka viunoni mwako, nami nitaufanya imara ufalme wake.

Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa jina langu, nacho kiti cha enzi cha ufalme wake nitakifanya imara milele. Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu, akitenda maovu nitamwadhibu kwa fimbo yako, na ufalme wako, vitathibitishwa milele mbele yako. Nacho kiti chako kitafanywa imara milele.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 89:1 โ€“ 4, 26, 28 (K) 36(K)

Wazao wake watadumu milele.

Fadhili za Bwana nitaziimba milele;Kwa kinywa changu nitavijulisha vizazi vyote uaminifu wako.

Maana nimesema, Fadhili zitajengwa milele;Katika mbingu utauthibitisha uaminifu wako. (K)

Nimefanya agano na mteule wangu,Nimemwapia Daudi, mtumishi wangu.Wazao wako nitawafanya imara milele,Nitakijenga kiti chako cha enzi hata milele. (K)

Yeye ataniita, Wewe baba yangu,Mungu wangu na mwamba wa wokovu wangu.

Hata milele nitamwekea fadhili zangu,Na agano langu litafanyika amini kwake. (K)

SOMO 2

Rum. 4:13, 16 โ€“ 18, 22

Ahadi ile ya kwamba atakuwa mrithi wa ulimwengu alipewa Ibrahimu na uzao wake, si kwa sheria bali kwa haki aliyohesabiwa kwa Imani. Kwa hiyo ilitoka katika Imani, iwe njia ya neema, ili kwamba ile ahadi iwe imara kwa wazao wote; si kwa wale wa torati tu, ila kwa wale wa Imani ya Ibrahimu; aliye baba yetu sisi sote; (kama ilivyoandikwa, Nimekuweka kuwa baba wa mataifa mengi); mbele zake yeye aliyemwamini, yaani Mungu, mwenye kuwahuisha wafu, ayatajaye yale yasiyokuwako kana kwamba yamekuwako.Naye aliamini kwa kutarajia yasiyoweza kutarajiwa, ilia pate kuwa baba wa mataifa mengi, kama ilivyonenwa, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako. Kwa hiyo ilihesabiwa kwake kuwa ni haki.Neno la Bwanaโ€ฆ Tumshukuru Mungu.

SHANGILIO

Zab. 84:5

Heri wakaao nyumbani mwako, Ee Bwana.

INJILI

Mt. 1:16, 18 โ€“ 21, 24

Yakobo alimzaa Yusufu mumewe Mariamu aliyemzaa yesu aitwaye Kristo.Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi. Mariamu mama yake alipokuwa ameposwa na Yusufu, kabla hawajakaribiana, alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akimchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.Naye Yusufu alipoamka katika usingizi, alifanya kama malaika wa Bwana alivyomwagiza; akamchukua mkewe.

Neno la Bwanaโ€ฆ Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Richard Mulwa Guest Jul 18, 2024
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ James Kawawa Guest Jun 1, 2024
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ John Mwangi Guest Mar 26, 2024
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ George Mallya Guest Dec 1, 2023
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Samson Tibaijuka Guest Nov 9, 2023
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ Irene Akoth Guest May 9, 2023
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ Irene Akoth Guest May 4, 2023
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrema Guest Mar 24, 2023
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Mary Kendi Guest Feb 28, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ Lucy Mahiga Guest Feb 11, 2023
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ Rose Waithera Guest Dec 26, 2022
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ Janet Mwikali Guest Oct 28, 2022
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Paul Kamau Guest Sep 28, 2022
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Nancy Akumu Guest Apr 9, 2022
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Andrew Mchome Guest Mar 19, 2022
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Christopher Oloo Guest Mar 1, 2022
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Andrew Mchome Guest Sep 9, 2021
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Grace Wairimu Guest Aug 30, 2021
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ Alice Wanjiru Guest May 10, 2021
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Monica Adhiambo Guest Jan 5, 2021
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ John Kamande Guest Dec 29, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Rose Amukowa Guest Dec 8, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Grace Majaliwa Guest Dec 2, 2020
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Majaliwa Guest Mar 11, 2020
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Sarah Achieng Guest Jan 17, 2020
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Isaac Kiptoo Guest Nov 25, 2019
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Thomas Mtaki Guest Oct 27, 2019
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Anna Malela Guest Aug 15, 2019
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Vincent Mwangangi Guest Jun 28, 2019
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ Mary Njeri Guest May 16, 2019
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ Joseph Kawawa Guest Apr 26, 2019
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ Christopher Oloo Guest Oct 28, 2018
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Benjamin Masanja Guest Oct 24, 2018
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Violet Mumo Guest Mar 3, 2018
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Susan Wangari Guest Feb 24, 2018
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ Alex Nyamweya Guest Feb 8, 2018
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ Paul Kamau Guest Feb 6, 2018
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Stephen Mushi Guest Jun 25, 2017
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ James Kimani Guest May 10, 2017
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ George Mallya Guest Apr 26, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ Samuel Were Guest Mar 15, 2017
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Victor Malima Guest Feb 18, 2017
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Charles Mchome Guest Feb 14, 2017
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Ann Wambui Guest Feb 9, 2017
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Ruth Mtangi Guest Jan 23, 2017
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ Alice Mrema Guest Nov 20, 2016
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Alice Jebet Guest Apr 27, 2016
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Rose Kiwanga Guest Mar 7, 2016
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Martin Otieno Guest Sep 28, 2015
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ Betty Kimaro Guest Sep 4, 2015
Mungu ni mwema, wakati wote!

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About