Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

Historia Fupi ya Ibada ya Rozari

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Katika Kalenda ya Kanisa Katoliki,
huwa mwezi wa tano na mwezi wa kumi
ni miezi ambayo imewekwa kwa ajili ya
Bikira Maria na Mama Kanisa. Hivyo
hiyo miezi huwa inasaliwa rozari.
Wengi waweza kujiuliza kuwa ni kwa
nini ifanyike miezi hiyo? Yafuatayo nimajibu, mwezi wa tano umewekwa kwa
heshima ya Bikira Maria kutokana na
nini kilitokea katika historia hapo
nyuma.
Mnamo Karne ya 16 mwezi
watano kwa miaka yote ulikuwa ni
mwezi ambao sikukuu nyingi za
kiserikali ndo zilikuwa zikifanyika.
Kanisa kwa kutambua hilo nalo
likahidhinisha pia mwezi wa tano uwe
ni mwezi wa Rozari, na kwa makusudi
zaidi Kanisa lililenga kuwa sherehe hizo
ziendane na taratibu za wakristu, ni
kwa msingi huo sherehe hizo ziliendana
na mwezi wa rozari na kutokea hapo
ikahidhinishwa kuwa mwezi wa tano wa
mwaka ni mwezi wa Bikira Maria. Pia
mwezi wa kumi (October) pia ni mwezi
wa Bikira Maria na pia ni mwezi wa
Kusali Rozari kutokana na historia ya
hapo nyuma pia, na ilikuwa kwamba
baada ya ushindi wakristo walioupata
katika vita baina yao na yule aliyeitwa
Lepanto mnamo 7 October, 1571, Papa
wa wakati ule Papa Pius V aliufanya
huo ushindi kuwa ulitokana na
maombezi ya Bikira Maria, na alisema
kuwa rozari ni silaha kubwa hata kuliko
silaha kubwa za kivita. Ni Kwa msingi
huu tunaona kuanzia hapo mwezi wa
kumi ukawa mwezi uliotengwa na
Mama Kanisa kwa Bikira Maria, na pia
ukaitwa mwezi wa Rozari.

HISTORIA YENYEWE

Ni kwamba sala ya Rozari inasemekana
kuanzishwa na Mt. Dominico
aliyezaliwa mnamo mwaka 1170 na
kufariki mwaka 1221 na hiyo sala Mt.
Dominico aliipata kwa njia ya ufunuo
ambapo Bikira Maria alimtokea na
kumwamuru awe anasali rozari. Bikira
Maria alimwamuru mtakatifu Dominico
kusali rozari kwa kipindi hicho iwe
kama silaha yake ili kupambana na
uzushi uliokuwa umeibuka ukipingana
na mafundisho ya Kanisa, na huo
uzushi uliitwa โ€˜ Albigensiaโ€™ hili ni kundi
lilokuwa na imani kuwa Duniani kuna
nguvu nguvu mbili zenye uwiano sawa
lakini hupingana na kupigana moja
baada ya nyingine, nazo nguvu hizo ni
Mungu na Shetani. Hivyo hawa
waliamini kabisa kuwa Mungu na
Shetani wana nguvu sawa ( Dualistic )
waliamini pia kuwa dunia hii imejaa
uovu kwa kuwa iliumbwa na mwovu. Ni
kwa msingi huu Kanisa liliamua
kupambana na hawa wazushi ambao
pia walionekana kupotosha mafundisho
ya Kanisa. Ndipo tunaona Bikira Maria
anamtokea Mtakatifu Dominico na
kumwambia asali rozari ili kupambana
na mafundisho hayo ya kizushi. Ni Papa
Pio V ambaye mnamo mwaka 1569
alihidhinisha rasmi kusali rozari kwa
kanisa nzima na kuhidhinisha rozari
iwe jinsi tunavyoiona sasa. Katika zile
zama za kati, watawa wamonaki
walizoea kusali zaburi 150, na kwa
upande wa waumini walei ambao kwa
kipindi hicho hawakujua kusoma zaburi
iliwabidi wasali sala ya Baba yetu mara
150 baadala ya zaburi 150 na hizo baba
yetu walizisali kwa kuhesabu punje 150
zilizokuwa zimefungwa kwenye kamba
ndefu ambayo kwa lugha ya kitaalamu
iliitwa โ€œ Corona โ€ au kwa Kiingereza โ€œ
Crown โ€ kadiri ibada kwa Bikira Maria
ilivyoendelea kushamiri mnamo Karne
ya 12, sala kwa Bikira Maria
ilianzishwa na hivyo kuanza kusali
salamu maria 150 baadala ya baba yetu
150.
Salamu Maria 150 hapo baadaye
zilikuja kugawanywa katika makundi/
mafungu na Mtawa mdominica
aliyeitwa Henry Kalkar ( 1328-1408),
ambapo kila tendo la rozari lilikuwa na
mafungu 50 ya salamu Maria ambapo
pia kila fungu liligusia maisha ya Bikira
Maria na Yesu katika historia ya
wokovu wetu. Zaidi ya hapo, mtawa
mwingine wa mdominican aliyeitwa
Alanus de Rupe aliendelea kugawanya
hiyo historia ya matendo ya wokovu
wetu katika matendo ya furaha ,uchungu,
na utukufu kama tunavyoyaona sasa.
(NB Matendo ya mwanga hayo ni ya
majuzi siyo ya wakati ule). Na
nikuanzia hapo Bikira Maria amepewa
nafasi kubwa katika shirika la watawa
wa Dominican. Hivyo utamaduni wa
kusali rozari umeendelea karne hata
karne, mfano Papa Leo XIII (1878-1903)
aliweka msisitizo mkubwa juu ya ibada
ya rozari kwa Bikira Maria. Kuanzia
September 1, 1883 Baba Mtakatifu Leo
XIII aliandika jumla ya barua za
kichungaji 11 zote zikiwa zinaweka
mkazo juu ya rozari. Hivyo rozari ni
sala inayotokana na maandiko
matakatifu( Biblia). Mafumbo ya rozari
yote yanapatikana katika agano jipya
ambapo ndo tunaona matendo ya Bikira
Maria na Yesu Kristo katika wokovu
wetu.
tunakumbushwa uchungu aliopata
Bikira Maria Katika maisha yake hasa
ule utabiri wa Simeoni kwa Bikira
Maria juu ya mateso na kifo cha
mwanae Yesu, Matendo saba ya furaha
kwa Maria ambapo yaananza na
kupashwa habari kwa Bikira Maria na
Malaika wa Bwana, kupalizwa
mbinguni, na matendo ya huruma ya
Bikira Maria kwa wale ambao
wanaendelea kuteseka hapa duniani.
AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Margaret Mahiga Guest Jul 23, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Ann Awino Guest Apr 13, 2024
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Janet Mwikali Guest Apr 11, 2024
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Peter Mwambui Guest Jan 11, 2024
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ George Ndungu Guest Dec 21, 2023
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Alice Wanjiru Guest Jul 23, 2023
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ Susan Wangari Guest Mar 28, 2023
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Lydia Mahiga Guest Nov 13, 2022
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Jacob Kiplangat Guest Sep 26, 2022
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Sharon Kibiru Guest Sep 16, 2022
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ John Kamande Guest Sep 6, 2022
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Francis Njeru Guest May 7, 2022
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Monica Adhiambo Guest Apr 27, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Sarah Mbise Guest Nov 24, 2021
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ Fredrick Mutiso Guest Nov 23, 2021
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Benjamin Kibicho Guest Oct 15, 2021
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ Henry Mollel Guest Apr 28, 2021
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ Brian Karanja Guest Mar 8, 2021
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ Emily Chepngeno Guest Oct 23, 2020
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ John Lissu Guest Jul 14, 2020
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Joseph Kawawa Guest Jun 30, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Faith Kariuki Guest Jan 15, 2020
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrope Guest Oct 25, 2019
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ Victor Mwalimu Guest Oct 12, 2019
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Linda Karimi Guest Aug 9, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Joyce Aoko Guest Aug 5, 2019
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ John Lissu Guest Oct 18, 2018
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Alice Mrema Guest Sep 11, 2018
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ Mariam Hassan Guest Jul 20, 2018
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Lucy Kimotho Guest Jun 12, 2018
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Martin Otieno Guest May 8, 2018
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Peter Mbise Guest Mar 28, 2018
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Bernard Oduor Guest Mar 26, 2018
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ David Chacha Guest Nov 9, 2017
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ Rose Lowassa Guest Sep 11, 2017
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ Victor Sokoine Guest Aug 20, 2017
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Andrew Mahiga Guest Jul 26, 2017
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Margaret Mahiga Guest Jul 24, 2017
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Francis Njeru Guest Jun 30, 2017
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Joseph Kawawa Guest Jun 15, 2017
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Esther Cheruiyot Guest May 13, 2017
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Wilson Ombati Guest Apr 15, 2017
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ David Kawawa Guest Nov 21, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Paul Ndomba Guest Oct 2, 2016
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Faith Kariuki Guest Sep 8, 2016
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Paul Ndomba Guest Aug 9, 2016
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Rose Waithera Guest Apr 11, 2016
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ John Mwangi Guest Mar 8, 2016
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ Mariam Kawawa Guest Dec 26, 2015
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ Grace Wairimu Guest Sep 18, 2015
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About