Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

Je Bikira Maria Alizaa Watoto Wengine?

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Mapokeo kuhusu Bikira Maria yanaonyesha alikuwa binti pekee wa wazee watakatifu Yohakimu na Ana. Vilevile
Mt. Yosefu, ingawa kisheria alikuwa mume wake, hakutenda naye tendo la ndoa hata moja. Ndiyo maana kwenye
litania yake tunamuita mwenye usafi kamili. Yosefu likufa kabla Yesu hajaanza utume kwa kubatizwa kwenye mto
Yordani. Sisi tunasadiki Maria ni โ€œBikira daimaโ€.
Ndugu wa Yesu wanaosemwa katika Injili ni kina nani?
Wanaosemwa katika Injili โ€œndugu zake Yesuโ€ si watoto
wa Bikira Maria wala Yosefu mtakatifu, bali ndugu wa kiukoo waliokuwa jirani sana na familia hiyo takatifu. Kama
Bikira Maria angekuwa na watoto wengine, je, Yesu Bwana wetu asingekuwa amefanya kosa la kiudugu
kuwanyangโ€™anya Mama yao na kumfanya awe Mama wa mtume Yohane alipomkabidhi msalabani, โ€œโ€˜Mwana, tazama
Mama yakoโ€™. Na tangu saa ile huyo mwanafunzi alimchukua akae nyumbani kwakeโ€ (Yoh 19:27).
Katika Agano Jipya yupo Yakobo anayeitwa na mtume Paulo โ€œndugu yake Bwanaโ€ (Gal 1:19): Yakobo huyo
alikuwa maarufu katika Kanisa la Yerusalemu (Mdo 12:7; 15:13-21; 21:18-20; Gal 2:9). Yakobo huyo si mtume
Yakobo mwana wa Alfayo, wala mtume Yakobo kaka yake Yohane (Lk 6:12-16), bali ni Yakobo ndugu yake Yose na
mama yao kwenye Injili anaitwa โ€œMaria mwingineโ€, si Maria Mama wa Yesu. โ€œWalikuwepo pia wanawake
waliotazama kwa mbali. Miongoni mwao akiwa Maria Magdalena, Salome na Maria mama wa akina Yakobo mdogo
na Yoseโ€ (Mk 15:40). Maria lilikuwa jina la kawaida kwa Wayahudi: akina Maria wakiwa wengi hivyo, tujue
kuwatofautisha kwenye Injili. Bikira Maria Injili zinamtaja kama โ€œMama wa Yesuโ€.

Je, Bikira Maria ni Bikira Daima au alizaa watoto wengine?

Jibu fupi ni kwamba Bikira Maria hakuzaa watoto wengine na hakuwa na watoto wengine zaidi ya Yesu
Hapo zamani hakuna mkristu au dehebu lolote lililokuwa linapinga kuwa Bikira Maria sio Bikira Daima hata Waprotestanti/walokole waliamini Bikira Maria ni Bikira Hata Baada ya Kumzaa Yesu. Kwenye Miaka ya 1400-1600 Watu wote wakwanza waliopinga Kanisa Katoliki walikubali kuwa Bikira Maria ni Bikira daima wakiwemo Martin Lutha aliyeanzisha kanisa la Lutheran, John Calvin aliyeanzisha Ulokole/Protestanti, Mchungaji Ulrich Zwingli, Heinrich Bullinger, and Thomas Cranmer. Kwa miaka zaidi ya 350 Waprotestant/walokole waliendelea kuamini kuwa Bikira Maria ni Bikira Daima.
Lakini baadae wakristo wengi walianza kupinga kuwa Bikira Maria ni Bikira Daima.

Tunaweza kuthibitisha kuwa Bikira Maria hakuzaa watoto wengine kwa kunukuu Biblia Kama ifuatavyo;

1. Bikira Maria Alikuwa Bikira Kabla ya kumzaa Yesu

Biblia inatuambia wazi kwamba Bikira Maria alikuwa Bikira Kabla ya kumzaa Yesu Kama tunavyosoma katika Luka 1:26-35
26 Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya, 27 kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi. 28 Malaika akamwendea, akamwambia, "Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe." 29 Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini? 30 Malaika akamwambia, "Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema. 31 Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu. 32 Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake. 33 Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho." 34 Maria akamjibu, "Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?" 35 Malaika akamjibu, "Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu. (Luka 1:26-35)

2. Biblia Haiwataji ndugu wa Yesu wakati Yosefu na Maria walipokimbilia Misri kumficha Yesu na wakati waliporudi

19 Baada ya kifo cha Herode, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto kule Misri, 20 akamwambia, "Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, urudi tena katika nchi ya Israeli, maana wale waliotaka kumwua mtoto huyo wamekwisha kufa." 21 Basi, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akarejea katika nchi ya Israeli. 22 Lakini Yosefu aliposikia kwamba Arkelao mwanawe Herode alikuwa mfalme wa Yudea mahali pa baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye baada ya kuonywa katika ndoto, alikwenda katika mkoa wa Galilaya, 23 akahamia katika mji uitwao Nazareti. Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyonenwa kwa njia ya manabii: "Ataitwa Mnazare." Matayo 2:19-23
Kama wangekuwepo wadogo zake Yesu Biblia ingetuambia kwamba walikuwa wapi wakati huo na walikuwa na Yesu au la.

3. Biblia haituambii kuwa Yesu alikua na wadogo zake alipokuwa na miaka 12

Wakati wa Maria, Yoseph na Yesu walipoenda Yerusalemu Yesu akiwa na miaka 12 Biblia haituambii kuwa Yesu alikuwa na wadogo zake na walikuwa wapi. Kumbuka walikuwa na Desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka kwa ajili ya Pasaka familia nzima kama familia. Je hao watoto wengine walikuwa wapi. Kwa nini walikuwa na Yesu Mwenyewe? Maana yake ni kwamba Yesu hakuwa na Wadogo zake.
41 Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka. 42 Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi. 43 Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari. 44 Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki. 45 Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta. 46 Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali. 47 Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima. 48 Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, "Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni." 49 Yeye akawajibu, "Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?" 50 Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia. 51 Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake. 52 Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.ย (Luka 2:41-52).
Kwa hiyo Biblia haionyeshi kuwa Yesu alikuwa na kaka na dada wakati akiwa na miaka 12. Kama wangekuwepo wangetajwa hapa kuwa walikuwa pamoja na Wazazi wao kama Yesu au walikuwa na Yesu wakati anapotea. Biblia haituambii chochote kwa hiyo wakati huo hapakuwa na wadogo zake Yesu.

4. Kukosekana kwa neneo "Binamu" kwenye lugha ya Yesu

Wakristu wa kwanza pamoja na Yesu aliongea Kiaramaiki au Kiebrania. Katika lugha zote hizo hakuna neno "Binamu" kwa hiyo mabinamu walijulikana kama dada na kaka wa mtu. Kwenye Agano jipya Neno kaka na Dada lilitumika pia kuwakilisha binamu.
Biblia inapotuambia kuwa Kaka na dada zake Yesu haimaanishi kaka wa kuzaliwa bali ndugu au Binamu
55 Je, huyu si yule mwana wa seremala? Je, mama yake si anaitwa Maria, na ndugu zake si kina Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda? 56 Na dada zake je, si wote wako hapa pamoja nasi? Basi amepata wapi haya yote?" (Mathayo 13:55-56)
Kwa hiyo wanaotajwa hapa ni ndugu wa Yesu kwa maana maneno kama; ndugu, kaka au dada lilitumika badala ya Binamu yaani mtoto wa shangazi au mjomba. Hapa juu Yosefu ametajwa kama kaka yake Yesu lakini tunajua kuwa Yosefu ni Baba yake Yesu. Baba na mwana hawawezi kuwa na jina sawa.

5. Biblia haitumii neno Ndugu, kaka au dada ikimaanisha ndugu wa kuzaliwa mama mmoja na baba mmoja

Sio mara zote Biblia imetumia neno Ndugu kumaanisha ndugu (Dada na Kaka) wa kuzaliwa yaani kaka na dada kwa mfano
Kwa kuangalia lugha ya Kiswahili na Kiingereza 1 Wakorintho 15:6 tunaona tafsiri tofauti.
KISWAHILIย 6 Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
ENGLISHย 6 After that, he appeared to more than five hundred of the brothers and sisters at the same time, most of whom are still living, though some have fallen asleep.
Kwa hiyo hapa neno kaka dada na ndugu linaonekana wazi halikumaanisha ndugu au kaka wa damu.

6. Undugu wa Yakobo, Simoni, Yosefu na Yuda kwa Yesu Sio wa mtu na kaka zake

Wasemao kuwa Bikira maria alikuwa na wana zaidi ya Yesu wananukuu kifungu hiki;
55 Je, huyu si yule mwana wa seremala? Je, mama yake si anaitwa Maria, na ndugu zake si kina Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda? 56 Na dada zake je, si wote wako hapa pamoja nasi? Basi amepata wapi haya yote?" (Mathayo 13:55-56)
Kumbuka kulikuwa na Yakobo wawili wakati wa Yesu, Vifungu vifuatavyo yunaweza kuona kuwa kulikuwa na yakobo wawili ambao walikuwa ndugu za Yesu lakini sio kaka wa kuzaliwa kwa mama.
35 Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, walimwendea Yesu wakamwambia, "Mwalimu, tunataka utufanyie kitu tutakachokuomba." (Marko 10:35)
55 Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia. 56 Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo. (Matayo 27:55-56)
Tunaweza kuona Undugu huu na Yesu kwa kusoma;
19 Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana. (Wagalatia 1:19)
Lakini Yuda anasema;
1 Mimi Yuda, mtumishi wa Yesu Kristo, ndugu yake Yakobo, nawaandikia ninyi mlioitwa na Mungu na ambao mnaishi katika upendo wa Mungu Baba, na katika ulinzi wa Yesu Kristo. (Yuda 1:1)
Kwa hiyo Yakobo na Yohane walikuwa watoto wa Mama mwingine ambao baba yao ni Zebedayo. Na Yakobo na Yosefu walikuwa watoto wa Maria Mwingine. Kwa hiyo ni Yakobo wa wili wa Mama wengine Tofauti na Maria. Yuda alikuwa ni ndugu yake Yakobo. Yakobo vilevile alikuwa ndugu yake Yesu.
Kuthibitisha kuwa Hawa kina Mama ndio waliokuwa Mama zao kina Yakobo wote hao wawili na wengine tunaweza kusoma;
25 Karibu na msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mama yake, na dada ya mama yake, Maria mke wa Kleopa, na Maria Magdalene. (Yohana 19:25)
Kwa hiyo kwenye (Yohana 19:25) tunaona Kuwa ni kwenye Msalaba wa Yesu alikuwepo Mama yake Yesu (Bikira Maria), Dada yake Bikira Maria, Mke wa Cleopa na Maria Magdalena. Na kwenye (Matayo 27:55-56) wamwtajwa ni Mama za kina nani kama inavyoonekana kwenye kifungu kifuatachi;.
55 Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia. 56 Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo. (Matayo 27:55-56).
Kwa hiyo hii ina maanisha kulikua na wanawake watatu wenye majina sawa ya Maria waliokuwa chini ya Msalaba. Yakobo na Yuda walikuwa watoto wa Maria Mke wa Cleofasi, na sio Mama wa Yesu, na hivyo sio kaka za Yesu.

7. Yesu alimwacha Mama yake kwa Yohane kwa kuwa hakuwa na Kaka na dada wakumwachia mamaye

26 Yesu alipomwona mama yake, na karibu naye amesimama yule mwanafunzi aliyempenda, akamwambia mama yake: "Mama! Tazama, huyo ndiye mwanao." 27 Halafu akamwambia yule mwanafunzi: "Tazama, huyo ndiye mama yako." Na tangu saa ile huyo mwanafunzi alimchukua akae nyumbani kwake.
Ndiyo maana Bikira Maria tangu siku ile alihamia kwa Yohani kwa kuwa hakuwa na watoto wengine.
AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 51

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Aldo Guest May 5, 2024
Umeeleza sawa kabisa! Shukrani kaka
๐Ÿ‘ฅ Fredrick Mutiso Guest Feb 23, 2024
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ Sharon Kibiru Guest Feb 1, 2024
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Henry Mollel Guest Aug 2, 2023
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Joyce Mussa Guest Jun 26, 2023
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ Patrick Akech Guest Oct 8, 2022
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Mwakalindile Guest Oct 7, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ Fredrick Mutiso Guest Jul 13, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ James Malima Guest May 24, 2022
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ George Wanjala Guest Apr 12, 2022
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ Paul Kamau Guest Mar 2, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Andrew Odhiambo Guest Feb 28, 2022
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Betty Kimaro Guest Jun 9, 2021
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Peter Tibaijuka Guest May 23, 2021
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Brian Karanja Guest May 16, 2021
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Nancy Kawawa Guest Apr 10, 2021
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Margaret Anyango Guest Apr 2, 2021
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Lydia Wanyama Guest Jan 30, 2021
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Ruth Kibona Guest Oct 7, 2020
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ Francis Mtangi Guest Jun 1, 2020
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Christopher Oloo Guest May 27, 2020
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Stephen Kikwete Guest May 7, 2020
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Esther Nyambura Guest Apr 6, 2020
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Peter Tibaijuka Guest Mar 23, 2020
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Catherine Mkumbo Guest Nov 16, 2019
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Linda Karimi Guest Oct 7, 2019
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Rose Mwinuka Guest Jul 24, 2019
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Margaret Mahiga Guest Feb 20, 2019
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ John Malisa Guest Jan 27, 2019
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Joseph Njoroge Guest Jan 8, 2019
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Mary Kidata Guest Aug 18, 2018
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ Henry Sokoine Guest Jun 27, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Stephen Kikwete Guest Dec 21, 2017
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Nora Kidata Guest Nov 2, 2017
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ Simon Kiprono Guest Oct 8, 2017
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Mary Mrope Guest Sep 10, 2017
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Alex Nyamweya Guest Aug 22, 2017
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ Bernard Oduor Guest Apr 25, 2017
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ John Mushi Guest Apr 10, 2017
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Benjamin Masanja Guest Feb 25, 2017
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ Hellen Nduta Guest Dec 11, 2016
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ Rose Waithera Guest Oct 15, 2016
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Joseph Njoroge Guest Sep 15, 2016
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Benjamin Kibicho Guest Aug 30, 2016
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Edith Cherotich Guest Jul 6, 2016
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ James Mduma Guest May 11, 2016
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ David Kawawa Guest Feb 28, 2016
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Elizabeth Mrope Guest Dec 29, 2015
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Francis Mtangi Guest Dec 21, 2015
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Mariam Kawawa Guest Sep 18, 2015
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ Bernard Oduor Guest Jul 18, 2015
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About