Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁

Asili na matumizi ya Neno "AMINA" kama kiitikio muhimu katika Liturujia

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Kiitikio hicho tunakifahamu sisi sote; tunaitikia mara nyingi lakini je, tunaelewa umuhimu wake? Binafsi nikichunguza wakati wa maadhimisho mbalimbali ya Liturujia hasa Adhimisho la Ekaristi, ni baadhi tu ya waamini wanaoitikiaAmina sehemu mbalimbali wakati wa Misa. Waamini wengine huitikia  kwa sauti  ya kuungama dhambi na wengine hawaitikii kabisa.

Asili yake 

Kwa asili Amina ni neno la kiebrania na maana yake ni: ni kweli kabisa.  Neno hilo lililotumika kukubali au kuthibitisha ukweli wa maneno au jambo lililokuwa limesemwa. Kwa hiyo mtu aliyesema Amina alitakiwa kusikia nini kilichosemwa na ndipo akubalie:    Amina.
Neno hilo limetumika katika Agano la Kale hasa katika Zaburi. Katika Agano Jipya Bwana Yesu alilitumia mara nyingi alipotaka kusisitiza siyo tu ukweli wa lile alilolisema bali pia uzito wake. Kwa namna hiyo Bwana Yesu alidhihirisha pia mamlaka yake katika lile alilosema.
Katika kitabu cha Ufunuo Yesu mwenyewe anaitwa Amina, kwani yeye ni mwaminifu kabisa katika maneno yake na kwamba yale anayosema kwa uhakika yatatimia. Tunasoma hivi: “Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina. Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli…” (Ufu 3:14). Yesu mwenyewe anajiita  “njia, na  ukweli na  uzima”(Yn 14:6).

Katika Liturujia

Katika Liturujia yetu Amina ni kiitikio muhimu sana. Tunapoanza Sala zetu na kuhitimisha tunafanya Ishara ya Msalaba na kuitikiaAmina.Tunaposema Amina tunasisitiza umuhimu wa kuanza Sala au Liturujia tunayoadhimisha kwa jina la Utatu Mtakatifu. Kwa Sala hiyo msingi tunautukuza Utatu Mtakatifu na kuomba utuongoze katika Liturujia yetu tunayoadhimisha au Sala yetu tunayoitoa. Kwa kupiga Ishara ya Msalaba tunajiweka mikononi mwa Utatu Mtakatifu tunapoanza Sala zetu au kuadhimisha Liturujia, na tunapomaliza tunapiga tena Ishara ya Msalaba na kusemaAmina. Katika Adhimisho la Liturujia kwa kawaida kuhani huhitimisha kwa Baraka ndipo waamini hujiandika Ishara ya Msalaba.
Hata hivi katika Adhimisho moja la Liturujia kuna Sala mbalimbali ambazo kuhani au atazitamka kwa sauti peke yake kama mwongoza Adhimisho ili waamini wasikie na hatimaye waitikie Amina lakini kuna Sala ambazo kuhani hutakiwa kusali pamoja na waamini na wote watazihitimisha kwa pamoja kwa kiitikio hichohicho Amina. Tufuatane kuangalia Aminakatika Adhimisho la Ekaristi, yaani Misa.

Mwanzo wa Misa  

Mwanzoni kuhani huanza: Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Kama tulivyosema hapo juu hii ni Sala ya msingi ambayo inatuweka mikononi mwa Utatu Mtakatifu tunapoanza kuadhimisha Liturujia yetu. Kuhani akishasema vile Wakristo wote wanatakiwa kuitikia Amina. Wale wasioitikia wanafanya kosa kubwa la kutokukiri imani kwamba tunajiweka mikononi mwa Utatu Mtakatifu. Wanatakiwa kujiuliza wamefika kanisani kufanya nini?
Kuhani huwasalimu waamini na kisha hutualika kukiri dhambi zetu. Hapo kuna namna mbalimbali za kukiri dhambi, lakini zote huishia na Sala anayotamka kuhani: Mungu mwenyezi atuhurumie, atusamehe dhambi zetu, atufikishe kwenye uzima wa milele. Waamini wote hutakiwa kuitikia  Amina. Kwa nini wengine basi hawaitikii?
Hata hivi tukumbuke tendo hilo ni la kukiri dhambi na kuomba msamaha wa jumla katika kujiweka tayari kuadhimisha mafumbo matakatifu kama mwaliko wa kuhani unavyosema. Hiyo siyo nafasi ya Sakramenti ya Kitubio na Upatanisho. Mkristo mwenye dhambi kubwa lazima aende kuungama kwa kuhani yaani padri au Askofu.
Baada ya tendo la kukiri dhambi na kuomba msamaha hufuata Utenzi wa Utukufu ambao huimbwa au kusemwa siyo na kwaya peke yaobali na waamini wote pamoja na kuhani. Utenzi huishia na Amina. Waamini wote pamoja na kuhani hukiri kwamba walivyoimba au kusali ni ukweli kabisa.
Sehemu ya Mwanzo wa Misa huhitimishwa na Sala iitwayo Kolekta, kutokana na neno la kilatini lenye maana ya kukusanya. Kuhani akishasema: Tuombe, inampasa kunyamaa kitambo ili kila Mkristo na kuhani mwenyewe wasali kimya ndipo kuhani ahitimishe maombi yao kwa sala iliyomo katika kitabu cha Misa. Sala anayosali kuhani ni kama inakusanya na kuhitimisha maombi ya Wakristo wote wanaoshiriki Misa hiyo. Mwishoni mwa Kolekta hiyo wote hutakiwa kuitikia Amina. Asiyeitikia huwaza nini moyoni mwake?

Liturujia ya Neno

Wakati wa Liturujia ya Neno, kabla ya Injili, kuhani hujiandaa kwa Sala fupi  ili kutangaza Injili. Iwapo Misa huongozwa na Askofu, shemasi au padri iwapo shemasi hayuko huomba Baraka kwa Askofu. Anapopata Baraka hupiga ishara ya Msalaba na kutikia Amina.
Baada ya mahubiri, siku za Dominika na Sherehe hufuata Kanuni ya Imani ambayo, kama utenzi wa Utukufu kwa Mungu juu, huimbwa au husemwa na Wakristo wote, na mwishoni wote humaliza kwa Amina.
Tunapomaliza sehemu ya Liturujia ya Neno kuhani huwaalika waamini kusali: Salini ndugu, ili sadaka yangu na yenu ikubalike kwa Mungu Baba mwenyezi. Wakristo wakishasali hawasemiAmina kwa sababu kuhani huendelea mara na Sala iitwayo Sala juu ya Vipaji (oratio super oblata) ambayo ni ya kuombea dhabihu. Baada ya Sala hiyo ndipo Wakristo wote huitikia Amina.Tujibidishe kufanya vile.

Sala Kuu ya Ekaristi

Sala ya kuombea vipaji huhitimisha sehemu ya kuandaa vipaji. Hufuata Sala Kuu ya Ekaristi inayoanza na dayalojia: Bwana awe nanyi,… Inueni mioyo .. Mwishoni mwa Sala Kuu ya Ekaristi hufuata kiitikio cha Amina, ambayo huitwa Amina Kuu. Waamini wote hutakiwa kuitikia kwa nguvu Amina hiyo Kuu. Katika Sherehe  waamini wote siyo kwaya peke yao, waimbe Amina mara tatu. Wanamuziki wazingatie hilo wakitunga muziki.
Baada ya Amina kuu hufuata sehemu ya kujiandaa kwa Komunyo Takatifu, inayoanza na Sala ya Bwana: Baba yetu uliye mbinguni. Baada ya sala hiyo hatuitikii Amina kwa sababu kuhani huendelea`mara :Ee Bwana, tunakuomba utuopoe …hatimaye wote huitikia: Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu…
Hufuata mara Sala ya kuomba Amani ambayo kuhani husali na mwishoni wote huitikia Amina. Wakati wa kupokea Ekaristi kila Mkristo hutakiwa kuitikia Amina kabla ya kupokea Mwili wa Bwana. Ni tendo la kukiri imani kwamba unasadiki huo ni Mwili wa Kristo. Wote huitikiaAmina mwishoni mwa Sala baada ya Komunyo.

Hatima

Mwishoni mwa Misa wakati kuhani anapowabariki waamini ndipo wote wakiinamisha vichwa vyao, hupiga Ishara ya Msalaba na kuitikia Amina ya mwisho.Wito kwa Wakristo wote: Tuitikie AMINA wakati wa Liturujia, bila kusita.Kwa kufanya vile tunashiriki na kusali  na kuhani tena tunakiri imani yetu kwamba alivyotamka kuhani ninakubali, ni kweli kabisa na Sala hiyo huwa Sala yetu pia.
AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
👥 Catherine Mkumbo Guest May 11, 2024
Neema ya Mungu inatosha kwako
👥 Ruth Wanjiku Guest Apr 21, 2024
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
👥 Wilson Ombati Guest Jan 21, 2024
Nguvu hutoka kwa Bwana
👥 Ruth Mtangi Guest Dec 23, 2023
Mwamini katika mpango wake.
👥 Ruth Wanjiku Guest Dec 15, 2023
Neema na amani iwe nawe.
👥 Rose Lowassa Guest Jul 15, 2023
Mungu ni mwema, wakati wote!
👥 Henry Mollel Guest Feb 12, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
👥 James Kawawa Guest Sep 20, 2022
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
👥 Ruth Kibona Guest May 10, 2022
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
👥 John Mushi Guest Feb 21, 2022
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
👥 Patrick Kidata Guest Dec 24, 2021
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
👥 Grace Mligo Guest Oct 30, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
👥 Linda Karimi Guest Sep 24, 2021
Kwa Mungu, yote yanawezekana
👥 Nancy Kabura Guest Aug 4, 2021
Mungu akubariki!
👥 Lydia Mutheu Guest May 17, 2021
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
👥 Esther Cheruiyot Guest Apr 5, 2021
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
👥 Diana Mallya Guest Oct 16, 2020
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
👥 Dorothy Majaliwa Guest Jun 16, 2020
Rehema zake hudumu milele
👥 Patrick Kidata Guest Jun 10, 2020
Katika imani, yote yanawezekana
👥 John Lissu Guest May 2, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
👥 Nancy Komba Guest Feb 1, 2020
Nakuombea 🙏
👥 Philip Nyaga Guest Jan 26, 2020
Tumaini ni nanga ya roho
👥 Samson Mahiga Guest Apr 17, 2019
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
👥 Frank Macha Guest Mar 9, 2019
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
👥 Agnes Sumaye Guest Mar 7, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
👥 Francis Mrope Guest Feb 28, 2019
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
👥 Charles Wafula Guest Dec 19, 2018
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
👥 Ann Wambui Guest Nov 23, 2018
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
👥 Rose Mwinuka Guest Apr 9, 2018
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
👥 John Lissu Guest Dec 29, 2017
Tembea kwa imani, si kwa kuona
👥 Janet Mbithe Guest Oct 14, 2017
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
👥 Joseph Kawawa Guest Sep 18, 2017
Mwamini Bwana; anajua njia
👥 Rose Lowassa Guest Sep 2, 2017
Baraka kwako na familia yako.
👥 Peter Tibaijuka Guest Jul 21, 2017
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
👥 Alice Jebet Guest Jun 12, 2017
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
👥 Michael Onyango Guest Apr 24, 2017
Endelea kuwa na imani!
👥 Nancy Komba Guest Apr 4, 2017
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
👥 John Mwangi Guest Mar 5, 2017
Sifa kwa Bwana!
👥 Lucy Kimotho Guest Feb 13, 2017
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
👥 John Mushi Guest Jan 16, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
👥 Alex Nakitare Guest Jul 8, 2016
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
👥 Fredrick Mutiso Guest May 18, 2016
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
👥 Stephen Amollo Guest Apr 18, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 Alex Nyamweya Guest Feb 22, 2016
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
👥 James Kimani Guest Feb 10, 2016
Dumu katika Bwana.
👥 Anthony Kariuki Guest Dec 17, 2015
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
👥 Patrick Mutua Guest Oct 15, 2015
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
👥 Lucy Wangui Guest Jul 2, 2015
Imani inaweza kusogeza milima
👥 Nora Kidata Guest May 16, 2015
Wakati wa Mungu ni kamilifu
👥 Ruth Wanjiku Guest Apr 22, 2015
Rehema hushinda hukumu

🔗 Related Posts

🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About