Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU II

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Yesu, Mungu wangu mpenzi,/ upo hapa katika Altare mbele yangu;/ na mimi napiga magoti mbele yako.// Waniangalia sana,/ siyo kwa kunipeleleza,/ lakini kwa sababu wapenda kuniona hivi karibu na wewe,/ wafurahiwa nikija kukuabudu./ Wayasikiliza maneno yangu yote/ yenye kutoka mdomoni mwangu,/ na zaidi wapokea maneno yangu yanayotoka moyoni./ Nataka kuzungumza na wewe peke yako,/ na kusahau mambo mengine yote/ na watu wengine walioko kanisani pamoja nami./

Yesu wangu,/ nakushukuru/ kwa sababu umekubali kutupa Sakramenti hii kuu kabisa,/ ukitaka kukaa pamoja na sisi,/ na hata ukakubali kuwa chakula chetu/ chenye nguvu ya ajabu./ Mfalme wangu Yesu,/ Sultani wangu Mkuu,/ naamini kabisa kwamba upo katika Altare/ na kwamba umejificha chini ya umbo la mkate./ Ulipokuwapo bado hapa duniani mbele za watu,/ ulikuwa hujifichi kama sasa;/ lakini hata siku zile/ watu hawakuweza kukuona vile ulivyo./ Hawakuweza kuutambua Umungu wako,/ ikalazimu kukuamini tu sawa kama sisi./ Wakainama kichwa wakisema,/ β€œBwana wangu na Mungu wangu”./ Na mimi kadhalika naungama/ U Bwana wangu na Mungu wangu/ na Mkombozi wangu/ na salama yangu yote./ U Yesu wangu tu,/ siwezi kusema zaidi./ Nakuabudu ee Yesu./ Najua sana, mimi ni mdogo kabisa,/ sina maana hata kidogo./ Mimi ni dhaifu na maskini mno./ Lakini Wewe katika hruuma yako kubwa/ waniita nije kwako./ Wewe huuangalii umaskini wangu,/ bali wanivuta katika mapendo yako./

Nasikia maneno yako usemayo:/ β€œNjooni kwangu ninyi nyote mnaoelemewa na mizigo/ nami nitawasaidia”./ Kwa ajili ya maneno hayo/ nakuja kwako bila hofu./ Najua kwamba wanipenda,/ najua wataka kunisaidia na kuniponya,/ najua kuwa wataka kunitakasa./

Nahitaji sana msaada wako, hakika./ Unaniona katika mwendo wangu wa kila siku,/ Jinsi ninavyohangaika na vishawishi mara nyingi;/ jinsi nilivyo na lazima ya kushindana kila siku/ nikitaka kukaa mwema na safi katika utumishi wako./ Naungama mbele yako Wewe Mkombozi wangu,/ kwamba sikukaa imara siku zote vile nilivyopaswa./ Naungama kwamba nimeshindwa mara nyingine/ na kwa hivi naomba toba./ Lakini kwa nini nimeshindwa mara nyingine?/ Kwa nini nikakosa?/ Ni kwa sababu nalikuwa nimekwenda mbali nawe;/ nalianza kujitegemea mwenyewe./ Katika majivuno yangu nikajisifu mwenyewe,/ nikajiona mwema,/ nikasahau udhaifu wangu./ Na kwa ajili hiyo nikajitia katika hatari bure,/ sikujilinda tena,/ nikampa shetani nafasi ya kunishambulia kwa hila zake zote./ Unihurumie ee Yesu wangu./

Sasa nafahamu jinsi nilivyokuwa mjinga kwelikweli./ Ndiyo maana nakuabudu kwa moyo wangu wote./ Najiweka mikononi mwako/ ufanye nami vile unavyotaka./ Wewe utanitunza;/ Wewe utanilinda vema;/ Wewe utaniongoza nijue namna ya kuepa hatari zote,/ na jinsi ya kufukuza kila kishawishi./ Chukua moyo wangu kabisa,/ kwa sababu ni mali yako kamili;/ Wewe ndiwe uliyeniumba,/ ndiwe uliyenipeleka katika Ukristo,/ nawe ndiwe utakayenihukumu siku ya mbele./ Ndivyo ninavyojitolea kwako./ Ndivyo ninavyokuabudu,/ wala sijui njia nyingine ya kukusifu zaidi./

Yesu wangu mpenzi,/ naomba upokee kwa uzuri heshima hiyo yangu./ Angalia: naitolea pamoja na heshima yote/ unayopewa daima na watakatifu wako/ na malaika wako./ Nikipiga magoti hapa mbele yako sasa,/ siko peke yangu,/ nakuabudu pamoja na Mama yako Bikira Maria,/ ambaye sala zake zinakupendeza kabisa./ Sala zangu naweka pamoja na sala zake yeye,/ uzipokee zote pamoja,/ zikupendeze zote sawa./ Ee Mama Maria!/ Nifundishe maneno ya kumsifu Mwanao Yesu vizuri./ Nipeleke kwa Yesu tumwabudu pamoja./ Nifunike na utakatifu wako/ kusudi Yesu asiangalie tena umaskini wangu/ na makosa yangu,/ aniponye katika huruma yake./

Sasa najisikia vizuri, Yesu wangu./ Sasa nina moyo wa kuweza kuendelea vema/ katika njia njema./ Sasa ninatumaini kwamba/ nitakaa mkristo mwema,/ nitakuwa mtumishi wako mwaminifu./ Nasikia amani kubwa sana moyoni mwangu,/ kwa kuwa nimo mikononi mwako./ Baada ya dakika chache/ nitaondoka tena kanisani,/ nitarudi nyumbani kwangu,/ lakini hatutaachana,/ hapana./ Mapendo yetu yatatuunganisha pamoja daima./ Wewe utanikumbuka nikiwa kazini,/ nikilala usingizi,/ nikienda njiani,/ kila mahali nilipo,/ Wewe utaniona,/ utafuatana na mimi./ Kadhalika nitakukumbuka tu./ Nitafanya bidii nisikuache kabisa./ Amina.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ James Kimani Guest Jul 12, 2024
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Henry Sokoine Guest May 15, 2024
πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose
πŸ‘₯ Lucy Mushi Guest Mar 21, 2024
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest Feb 27, 2024
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ David Musyoka Guest Dec 14, 2023
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest Nov 13, 2023
πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
πŸ‘₯ David Chacha Guest Oct 2, 2023
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Charles Wafula Guest Sep 14, 2023
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ Kevin Maina Guest Jul 11, 2023
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Betty Kimaro Guest Jul 8, 2023
πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest May 21, 2023
πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi
πŸ‘₯ Nancy Kawawa Guest Jan 30, 2023
πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri
πŸ‘₯ Lydia Mutheu Guest Dec 1, 2022
πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha
πŸ‘₯ Sharon Kibiru Guest Oct 18, 2022
πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu
πŸ‘₯ Lydia Mahiga Guest Sep 9, 2022
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Agnes Sumaye Guest Sep 2, 2022
πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest Sep 2, 2022
πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka
πŸ‘₯ Peter Mugendi Guest Aug 25, 2022
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Joyce Mussa Guest Aug 16, 2022
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ George Ndungu Guest Aug 16, 2022
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ John Malisa Guest Aug 10, 2022
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Linda Karimi Guest Jul 16, 2022
πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu
πŸ‘₯ Ruth Mtangi Guest Jan 8, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Betty Cheruiyot Guest Sep 25, 2021
πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani
πŸ‘₯ Lucy Mushi Guest Aug 30, 2021
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Alice Jebet Guest Aug 14, 2021
πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu
πŸ‘₯ Peter Tibaijuka Guest Aug 7, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Richard Mulwa Guest Jul 31, 2021
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Thomas Mwakalindile Guest May 16, 2021
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest May 11, 2021
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Anna Mahiga Guest Mar 15, 2021
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Janet Sumaye Guest Feb 11, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Alice Wanjiru Guest Nov 19, 2020
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Sep 10, 2020
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Janet Mwikali Guest May 10, 2020
πŸ™β€οΈ Mungu akubariki
πŸ‘₯ Thomas Mtaki Guest May 5, 2020
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Joseph Kiwanga Guest May 2, 2020
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Ruth Kibona Guest Mar 25, 2020
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Tabitha Okumu Guest Mar 23, 2020
πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai
πŸ‘₯ Grace Majaliwa Guest Mar 23, 2020
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ John Kamande Guest Mar 21, 2020
πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo
πŸ‘₯ Wilson Ombati Guest Feb 25, 2020
πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
πŸ‘₯ Fredrick Mutiso Guest Feb 14, 2020
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Grace Mushi Guest Jan 19, 2020
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Grace Majaliwa Guest Oct 9, 2019
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Violet Mumo Guest Aug 11, 2019
πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest Jul 2, 2019
πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie
πŸ‘₯ Lucy Mushi Guest Dec 29, 2018
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Francis Mrope Guest Oct 1, 2018
πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana
πŸ‘₯ Irene Makena Guest Jul 19, 2018
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Rose Kiwanga Guest Jul 4, 2018
πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest Jun 15, 2018
πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu
πŸ‘₯ Edward Lowassa Guest Jan 14, 2018
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Lydia Mzindakaya Guest Dec 16, 2017
Amina
πŸ‘₯ Linda Karimi Guest Dec 7, 2017
πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe
πŸ‘₯ Fredrick Mutiso Guest Nov 23, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Thomas Mwakalindile Guest Nov 20, 2017
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Nov 13, 2017
πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu
πŸ‘₯ Azima Guest Oct 25, 2017
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Sep 24, 2017
πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About