Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA, MEI, 28, 2023: SHEREHE YA PENTEKOSTE

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Mdo. 2:1-11

Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.


Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu. Basi sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe. Wakashangaa wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya? Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo? Waparthi na Wamedi na Waelani, nao wakaao Mesopotamia, Uyahudi na Kapadokia, Ponto na Asia, Frigia na Pamfilia, Misri na pande za Libia karibu na Kirene, na wageni watokao Rumi, Wayahudi na waongofu, Wakrete na Waarabu; tunawasikia hawa wakisema kwa lugha zetu matendo makuu ya Mungu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu

WIMBO WA KATI KATI

Zab. 104:1, 24, 29-31, 34, (K) 30

(K) Waipeleka roho yako, Ee Bwana, Nawe waufanya upya uso wa nchi. au: Aleluya.

Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana,
Wewe, Bwana, Mungu wangu,
Umejifanya mkuu sana;
Ee Bwana, jinsi yalivyo mengi matendo yako!
Dunia imejaa mali zako. (K)

Waiondoa pumzi yao, wanakufa,
Na kuyarudia mavumbi yao,
Waipeleka roho yako, wanaumbwa,
Nawe waufanya upya uso wa nchi. (K)

Utukufu wa Bwana na udumu milele;
Bwana na ayafurahie matendo yake.
Kutafakari kwangu na kuwe kutamu kwake;
Mimi nitamfurahia Bwana. (K)

SOMO 2

1 Kor. 12 :3b-7, 12-13

Hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu. Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule. Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule. Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote. Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.

Maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule, navyo ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Kristo. Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.
Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu

SHANGILIO

Aleluya, aleluya,
Uje Roho Mtakatifu, uzienee nyoyo za waamini wako uwatie mapendo yako.
Aleluya.

INJILI

Yn. 20 :19-23

Ikawa jioni, siku ile ya kwanza ya juma, pale walipokuwapo wanafunzi, milango imefungwa kwa hofu ya Wayahudi; akaja Yesu, akasimama katikati, akawaambia, Amani iwe kwenu. Naye akiisha kusema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi wale wanafunzi wakafurahi walipomwona Bwana.
Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawapeleka ninyi. Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu. Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Stephen Kangethe Guest Jul 9, 2024
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Jun 22, 2024
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Brian Karanja Guest Apr 5, 2024
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Michael Mboya Guest Feb 10, 2024
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest Sep 5, 2023
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ David Musyoka Guest Aug 16, 2023
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest Jul 16, 2023
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Irene Akoth Guest Jul 8, 2023
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Francis Njeru Guest May 7, 2023
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Carol Nyakio Guest Feb 26, 2023
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Ruth Kibona Guest Feb 18, 2023
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Josephine Nekesa Guest Jan 28, 2023
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Alex Nakitare Guest Jan 27, 2023
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ John Malisa Guest Dec 2, 2022
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Anna Mahiga Guest Oct 13, 2022
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest Sep 11, 2022
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Esther Nyambura Guest Jul 7, 2022
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ John Mwangi Guest Jun 29, 2022
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Lucy Kimotho Guest Apr 26, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Brian Karanja Guest Mar 18, 2022
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Anthony Kariuki Guest Jan 4, 2022
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Patrick Mutua Guest Oct 26, 2021
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Emily Chepngeno Guest Oct 18, 2021
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Frank Sokoine Guest Jul 16, 2021
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ John Mwangi Guest Jan 4, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ George Ndungu Guest Nov 11, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Alice Jebet Guest Oct 19, 2020
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ James Malima Guest Oct 5, 2020
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Diana Mallya Guest Sep 2, 2020
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Aug 31, 2020
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Frank Macha Guest Aug 19, 2020
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Victor Malima Guest Aug 5, 2020
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Paul Kamau Guest Jan 9, 2020
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest Jun 27, 2019
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Lucy Kimotho Guest Jun 22, 2019
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Charles Wafula Guest Apr 19, 2019
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Frank Macha Guest Feb 6, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Brian Karanja Guest Jan 13, 2019
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Victor Sokoine Guest Nov 27, 2018
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Stephen Malecela Guest Aug 5, 2018
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Kenneth Murithi Guest Oct 18, 2017
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Mary Mrope Guest Jun 29, 2017
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Patrick Kidata Guest May 11, 2017
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Lucy Mahiga Guest Jan 10, 2017
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Bernard Oduor Guest Dec 6, 2016
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Catherine Naliaka Guest Jul 9, 2015
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Dorothy Mwakalindile Guest Jun 3, 2015
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Janet Wambura Guest May 8, 2015
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest May 6, 2015
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Alex Nyamweya Guest Apr 9, 2015
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About