Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

MASOMO YA MISA, MACHI 24, 2022: ALHAMISI, JUMA LA 3 LA KWARESIMA

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Yer. 7:23-28

ย 

Naliwaamuru neno hili, nikisema, Sikilizeni sauti yangu, nami nitakuwa Mungu wenu, nanyi mtakuwa watu wangu; mkaende katika njia ile yote nitakayowaamuru, mpate kufanikiwa. Lakini hawakusikiliza, wala kutega sikio lao, bali walikwenda kw amashauri yao wenyewe, na kwa ushupavu wa mioyo yao mibaya, wakaenda nyuma wala si mbele. Tokea siku ile baba zenu walipotoka katika nchi ya Misri hata leo, nimewatuma watumishi wangu wote manabii kwenu ninyi, nikiamka mapema kila siku na kuwatuma. Lakini hawakunisikiliza, wala kutega sikio lao; bali walifanya shingo yao kuwa ngumu; walitenda mabaya kuliko baba zao. Nawe utawaambia maneno hayo yote; lakini hawatakusikiliza; nawe utawaita; lakini hawatakuitikia. Nawe utawaambia, Taifa hili ndilo lisilosikiliza sauti ya Bwana, Mungu wao, wala kupokea mafundisho; uaminifu umepotea, umekatiliwa mbali vinywa vyao.

ย 

Neno la Bwanaโ€ฆ Tumshukuru Mungu.

ย 

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 95:1-2, 6-9 (K) 7

ย 

(K) Ingekuwa heri leo msikie sauti yake! Msifanye migumu mioyo yenu.

ย 

Njoni, tumwimbie Bwana,

Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu.

Tuje mbele zake kwa shukrani,

Tumfanyie shangwe kwa zaburi. (K)

ย 

Njoni, tuabudu, tusujudu,

Tupige magoti mbele za Bwana aliyetuumba.

Kwa maana ndiye Mungu wetu,

Na sisi tu watu wa malisho yake,

Na kondoo za mkono wake. (K)

ย 

Ingekuwa heri leo msikie sauti yake!

Msifanye migumu mioyo yenu;

Kama vile huko Meriba,

Kama siku ya Masa jangwani.

Hapo waliponijaribu baba zenu,

Wakanipima, wakayaona matendo yangu. (K)

ย 

SHANGILIO

Zab. 51:10, 12

ย 

Ee Mungu, uniumbie moyo safi,

Unirudishie furaha ya wokovu wako.

ย 

INJILI

Lk. 11:14-23

ย 

Yesu alikuwa akitoa pepo bubu; ikawa pepo alipotoka, yule bubu akanena, makutano wakastaajabu. Wengine wao wakasema, Atoa pepo kwa Beelzebuli, mkuu wa pepo. Wengine walimjaribu, wakitaka ishara itokayo mbinguni. Naye akajua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme uliofitinika wenyewe kwa wenyewe hufanyika ukiwa; na nyumba juu ya nyumba huanguka. Basi, ikiwa Shetani naye amefitinika juu ya nafsi yake, ufalme wake utasimamaje? Kwa kuwa ninyi mnasema kwamba mimi natoa pepo kwa Beelzebuli, wana wenu je! Huwatoa kwa nani? Kwa sababu hiyo, hao ndio watakaowahukumu. Lakini, ikiwa mimi natoa pepo kwa kidole cha Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia. Mtu mwenye nguvu aliyejifunga silaha zake, alindapo nyumba yake, vitu vyake vi salama; lakini mtu mwenye nguvu kuliko yeye atakapomwendea na kumshinda, amnyangโ€™anya silaha zake zote alizokuwa akizitegemea, na kuyagawanya mateka yake.

ย 

Mtu ambaye si pamoja nami yu kinyume changu; na mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya.

ย 

Neno la Bwanaโ€ฆ Sifa kwako Ee Kristo.

ย 

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Frank Macha Guest Jun 7, 2024
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ Mary Mrope Guest Apr 12, 2024
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Stephen Kikwete Guest Feb 10, 2024
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Monica Nyalandu Guest Nov 11, 2023
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ Margaret Anyango Guest Jul 27, 2023
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Christopher Oloo Guest Jun 20, 2023
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Majaliwa Guest Jun 3, 2023
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Benjamin Masanja Guest Feb 25, 2023
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ Carol Nyakio Guest Nov 8, 2022
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ Irene Akoth Guest May 20, 2022
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Sarah Karani Guest Apr 5, 2022
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ David Musyoka Guest Feb 7, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Jane Muthui Guest Feb 3, 2022
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Edith Cherotich Guest Jan 5, 2022
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Elijah Mutua Guest Dec 17, 2021
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ Anna Kibwana Guest Dec 6, 2021
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Linda Karimi Guest Oct 3, 2021
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ Joseph Kiwanga Guest Sep 26, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Catherine Mkumbo Guest Jul 22, 2021
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Jane Muthui Guest May 16, 2021
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ John Kamande Guest Mar 25, 2021
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Lucy Kimotho Guest Mar 17, 2021
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Anna Mchome Guest Feb 1, 2021
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Anna Sumari Guest Nov 30, 2020
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Irene Makena Guest Nov 12, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ John Lissu Guest Oct 15, 2020
Rehema zake hudumu milele
๐Ÿ‘ฅ Monica Nyalandu Guest Sep 29, 2020
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Anna Sumari Guest Apr 30, 2020
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Nkya Guest Jan 10, 2020
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Janet Sumaye Guest Dec 20, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ David Ochieng Guest Dec 19, 2019
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Andrew Mchome Guest Oct 25, 2019
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ John Mushi Guest Feb 16, 2019
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ Joy Wacera Guest Nov 3, 2018
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Sarah Mbise Guest Oct 12, 2018
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Vincent Mwangangi Guest Oct 7, 2018
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ George Mallya Guest Jul 22, 2018
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ Diana Mallya Guest Jul 9, 2018
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Sarah Achieng Guest Mar 5, 2018
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Joseph Kawawa Guest Feb 23, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Sarah Karani Guest Dec 15, 2017
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ Michael Mboya Guest Sep 12, 2017
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ Rose Waithera Guest Jul 8, 2017
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Nancy Komba Guest Mar 19, 2017
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ Nicholas Wanjohi Guest Dec 30, 2016
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ John Mushi Guest Nov 17, 2016
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Edward Chepkoech Guest Mar 31, 2016
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ David Musyoka Guest Oct 19, 2015
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Ruth Wanjiku Guest May 26, 2015
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Edward Lowassa Guest May 11, 2015
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About