Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ

MASOMO YA MISA, APRILI 1, 2023: JUMAMOSI, JUMA LA 5 LA KWARESIMA

โ€ข
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Eze. 37:21 โ€“ 28

Bwana Mungu asema hivi: Tazama, nitawatwaa wana wa Israeli toka kati ya mataifa walikokwenda, nami nitawakusanya pande zote, na kuwaleta katika nchi yao wenyewe; nami nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi hiyo, juu ya milima ya Israeli; na mfalme mmoja atakuwa mfalme wao wote; wala hawatakuwa tena mataifa mawili, wala hawatagawanyikana kuwa falme mbili tena, hata milele. Wala hawatajitia uchafu tena kwa vinyago vyao, wala kwa vitu vyao vichukizavyo, wala kwa makosa yao mmojawapo; lakini nitawaokoa, na kuwatoa katika makao yao yote, ambayo wamefanya dhambi ndani yake, nami nitawatakasa; basi watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao. Na mtumishi wangu, Daudi, atakuwa mfalme juu yao, nao wote watakuwa na mchungaji mmoja; nao wataenenda katika hukumu zangu, na kuzishika amri zangu, na kuzitenda. Nao watakaa katika nchi niliyompa Yakobo, mtumishi wangu, walimokaa baba zenu; nao watakaa humo, wao na watoto wao, na watoto wa watoto wao, milele; na Daudi, mtumishi wangu, atakuwa mkuu wao milele. Tena nitafanya agano la Amani pamoja nao; litakuwa agano la milele pamoja nao; naami nitaweka na kuwazidisha, na patakatifu pangu nitapaweka katikati yao milele. Tena maskani yangu itakuwa pamoja nao; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Na mataifa watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, mimi niwatakasaye Israeli, patakatifu pangu patakapokuwa katikati yao milele.

Neno la Bwanaโ€ฆ Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Yer. 31:10 โ€“ 13 (K) 10

(K) Bwana anatulinda kama mchungaji alindavyo kundi lake.

Lisikieni neno la Bwana, enyi mataifa,

Litangazeni visiwani mbali;

Mkaseme: Aliyemtawanya Israeli atamkusanya,

Na kumlinda kama mchungaji alindavyo kundi lake.

Kwa maana Bwana amemweka huru Yakobo,

Amemkomboa mkononi mwake aliyekuwa hodari kuliko yeye. (K)

Watakuja na kuimba katika mlima Sayuni.

Wataukimbilia wema wa Bwana,

Nafaka, na divai, na mafuta,

Na wachanga wa kondoo na wa ngโ€™ombe. (K)

Ndipo bikira atafurahi katika kucheza,

Na vijana na wazee pamoja;

Maana nitageuza masikitiko yao kuwa furaha,

Nami nitawafariji, na kuwafurahisha waache huzuni zao. (K)

SHANGILIO

Zab. 95:8 , 9

Leo msifanye migumu mioyo yenu, lakini msikie sauti yake Bwana.

INJILI

Yn. 11:45 โ€“ 57

Wengi katika Wayahudi waliokuja kwa Maria, na kuyaona yale aliyoyafanya Yesu, wakamwamini. Lakini wengine wakaenda zao kwa Mafarisayo, wakawaambia aliyoyafanya.

Basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakakusanya baraza, wakasema, Tunafanya nini? Maana mtu huyu afanya ishara nyingi. Tukimwacha hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja watamuondolea mahali petu na taifa letu. Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lolote; wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima. Na neno hilo yeye hakulisema kwa nafsi yake; bali kwa kuwa alikuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, alitabiri ya kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa hilo, wala si kwa ajili ya taifa hilo tu; lakini pamoja na hayo awakusanye watoto wa Mungu waliotawanyika, ili waawe wamoja. Basi tangu siku ile walifanya shauri la kumwua.

Kwa hiyo Yesu hakutembea tena kwa wazi katikati ya Wayahudi; bali alitoka huko, akaenda mahali karibu na jangwa, mpaka mji uitwao Efraimu; akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.

Na Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu; na wengi wakakwea toka mashambani kwenda Yerusalemu kabla ya Pasaka, ili wajitakase. Basi wao wakamtafuta Yesu, wakasemezana hali wamesimama hekaluni, Mwaonaje? Haji kabisa sikukuu hii? Na wakuu wa makuhani wa Mafarisayo walikuwa wametoa amri ya kwamba mtu akijua alipo, alete habari, ili wapate kumkamata.

Neno la Bwanaโ€ฆ Sifa kwako Ee Kristo

AckySHINE Solutions
โœจ Join AckySHINE for more features! โœจ

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
๐Ÿ‘ฅ Peter Mbise Guest Apr 5, 2024
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
๐Ÿ‘ฅ Thomas Mwakalindile Guest Mar 13, 2024
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐Ÿ‘ฅ Andrew Mchome Guest Aug 5, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐Ÿ‘ฅ Faith Kariuki Guest Jul 3, 2023
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
๐Ÿ‘ฅ James Kimani Guest Jun 3, 2023
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Lydia Mutheu Guest Dec 3, 2022
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐Ÿ‘ฅ Stephen Malecela Guest Nov 24, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐Ÿ‘ฅ Robert Ndunguru Guest Oct 24, 2022
Mungu ni mwema, wakati wote!
๐Ÿ‘ฅ Rose Amukowa Guest Sep 30, 2022
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐Ÿ‘ฅ Victor Kamau Guest Jul 20, 2022
Tumaini ni nanga ya roho
๐Ÿ‘ฅ Emily Chepngeno Guest Jul 4, 2022
Kwa Mungu, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Jane Muthui Guest Jun 29, 2022
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
๐Ÿ‘ฅ Michael Mboya Guest Apr 19, 2022
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐Ÿ‘ฅ George Tenga Guest Jan 13, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
๐Ÿ‘ฅ Patrick Akech Guest Sep 17, 2021
Endelea kuwa na imani!
๐Ÿ‘ฅ Agnes Lowassa Guest Aug 26, 2021
Mwamini katika mpango wake.
๐Ÿ‘ฅ Ann Wambui Guest May 6, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Stephen Mushi Guest Apr 29, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
๐Ÿ‘ฅ Mariam Hassan Guest Jan 25, 2021
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
๐Ÿ‘ฅ Isaac Kiptoo Guest Jan 9, 2021
Katika imani, yote yanawezekana
๐Ÿ‘ฅ Joseph Kawawa Guest Oct 6, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
๐Ÿ‘ฅ Miriam Mchome Guest Aug 1, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
๐Ÿ‘ฅ Stephen Mushi Guest Jul 16, 2020
Neema na amani iwe nawe.
๐Ÿ‘ฅ Edith Cherotich Guest Mar 19, 2020
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐Ÿ‘ฅ Peter Otieno Guest Feb 14, 2020
Mwamini Bwana; anajua njia
๐Ÿ‘ฅ Betty Kimaro Guest Feb 6, 2020
Nakuombea ๐Ÿ™
๐Ÿ‘ฅ Charles Mrope Guest Nov 25, 2019
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
๐Ÿ‘ฅ Joyce Mussa Guest Jul 6, 2019
Wakati wa Mungu ni kamilifu
๐Ÿ‘ฅ Tabitha Okumu Guest May 17, 2019
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐Ÿ‘ฅ Jacob Kiplangat Guest Feb 22, 2019
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
๐Ÿ‘ฅ Esther Cheruiyot Guest May 25, 2018
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐Ÿ‘ฅ Paul Ndomba Guest May 4, 2018
Mungu akubariki!
๐Ÿ‘ฅ Anna Kibwana Guest Jan 26, 2018
Rehema hushinda hukumu
๐Ÿ‘ฅ Carol Nyakio Guest Jan 9, 2018
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
๐Ÿ‘ฅ Thomas Mwakalindile Guest Jan 5, 2018
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐Ÿ‘ฅ Brian Karanja Guest Dec 19, 2017
Dumu katika Bwana.
๐Ÿ‘ฅ Christopher Oloo Guest Oct 24, 2017
Sifa kwa Bwana!
๐Ÿ‘ฅ Alex Nakitare Guest Sep 1, 2017
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
๐Ÿ‘ฅ Patrick Mutua Guest Aug 21, 2017
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Majaliwa Guest Jan 4, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
๐Ÿ‘ฅ Alice Wanjiru Guest Nov 23, 2016
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
๐Ÿ‘ฅ Betty Cheruiyot Guest Jul 24, 2016
Baraka kwako na familia yako.
๐Ÿ‘ฅ Diana Mumbua Guest Jul 8, 2016
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
๐Ÿ‘ฅ Nancy Kabura Guest Apr 28, 2016
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
๐Ÿ‘ฅ Paul Ndomba Guest Mar 1, 2016
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐Ÿ‘ฅ Andrew Mchome Guest Oct 28, 2015
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
๐Ÿ‘ฅ Joseph Kiwanga Guest Oct 19, 2015
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐Ÿ‘ฅ Michael Onyango Guest Sep 13, 2015
Nguvu hutoka kwa Bwana
๐Ÿ‘ฅ Dorothy Nkya Guest Aug 22, 2015
Imani inaweza kusogeza milima
๐Ÿ‘ฅ Raphael Okoth Guest May 16, 2015
Rehema zake hudumu milele

๐Ÿ”— Related Posts

๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About