Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

Sala ya Usiku kabla ya kulala

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

SALA YA KUSHUKURU

Tunakushukuru, ee Mungu, kwa mapaji uliyotujalia leo. Amina.

Baba yetu …

Salamu Maria …

SALA YA IMANI

Mungu wangu, nasadiki maneno yote. Linayosadiki na linayofundisha Kanisa Katoliki la Roma. Kwani ndiwe uliyetufumbulia hayo. Wala hudanganyiki, wala hudanganyi. Amina.

SALA YA MATUMAINI

Mungu wangu, natumaini kwako, nitapewa kwa njia ya Yesu Kristo. Neema zako hapa duniani, na utukufu mbinguni. Kwani ndiwe uliye agana hayo nasi, nawe mwamini. Amina.

SALA YA MAPENDO

Mungu wangu, nakupenda zaidi ya chochote. Kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza. Nampenda na jirani yangu, kama nafsi yangu, kwa ajili yako. Amina.

KUTUBU DHAMBI

Tuwaze katika moyo wetu makosa ya leo tuliyomkosea Mungu kwa mawazo, kwa maneno, kwa vitendo na kwa kutotimiza wajibu. (Husubiri kidogo ).

Nakuungamia Mungu Mwenyezi, nanyi ndugu zangu, kwani nimekosa mno, kwa mawazo, kwa maneno, kwa vitendo, na kwa kutotimiza wajibu.
Nimekosa mimi, nimekosa mimi, nimekosa sana. Ndiyo maana nakuomba Maria mwenye heri, Bikira daima, Malaika na Watakatifu wote, nanyi ndugu zangu, niombeeni kwa Bwana Mungu wetu.
Mungu Mwenyezi atuhurumie, atusamehe dhambi zetu, atufikishe kwenye uzima wa milele. Amina.

SALA YA KUWAOMBEA WATU

Ee Mungu, nawaombea watu wa nchi hii, wapate kusikia maneno yako na kukupenda wewe Bwana Mungu wetu.

SALA KWA MALAIKA MLINZI

Malaika mlinzi wangu, unilinde katika hatari zote za roho na za mwili. Amina.

MALAIKA WA BWANA

(kipindi kisicho cha Pasaka)
Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria.
Naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
Salamu, Maria,…..
Ndimi mtumishi wa Bwana.
Nitendewe ulivyonena.
Salamu, Maria….
Neno la Mungu akatwaa mwili.
Akakaa kwetu.
Salamu, Maria….
Utuombee, Mzazi mtakatifu wa Mungu.
Tujaliwe ahadi za Kristu.
Tuombe:
Tunakuomba, Ee Bwana, utie neema yako mioyoni mwetu, ili sisi tuliojua kwa maelezo ya Malaika kwamba Mwanao amejifanya Mtu kwa mateso na msalaba wake tufikishwe kwenye utukufu wa ufufuko. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. AMINA.

AU;

MALKIA WA MBINGU (kipindi cha Pasaka)

Malkia wa mbingu, furahi, aleluya.
Kwani uliyestahili kumchukua, Aleluya.
Amefufuka alivyosema, Aleluya.
Utuombee kwa Mungu, Aleluya.
Furahi shangilia, ee Bikira Maria, Alaluya.
Kwani hakika Bwana amefufuka Aleluya.
Tuombe.
Ee Mungu, uliyependa kuifurahisha dunia kwa kufufuka kwake Bwana wetu Yesu Kristu, Mwanao, fanyiza, twakuomba, kwa ajili ya Bikira Maria, tupate nasi furaha za uzima wa milele. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. Amina.

ATUKUZWE (mara tatu)
Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu. Kama mwanzo na sasa na siku zote na milele. Amina.

KUJIKABIDHI

Enyi Yesu, Maria na Yosefu nawatolea moyo na roho na uzima wangu!
Enyi Yesu, Maria na Yosefu mnijilie saa ya kufa kwangu!
Enyi Yesu, Maria na Yosefu mnijalie nife mikononi mwenu!

(Rehema ya siku 300).

WIMBO:

Kwa heri Yesu mpenzi mwema,
Naenda usiudhike mno.
Nakushukuru, nakupenda,
Kwa hizo nyimbo za mwisho.
Asubuhi nitarudi.
Yesu kwa heri.

Kwa heri Mama mtakatifu,
Sasa napita pumzika.
Asante kwa moyo na nguvu,
Leo umeniombea.
Asubuhi nitarudi.
Mama kwa heri.

Kwa heri Yosefu mnyenyekevu,
Kazi zatimilizika.
Kama mchana, leo usiku,
Nisimamie salama.
Asubuhi nitarudi.
Yosefu kwa heri.

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

KUOMBA ULINZI WA USIKU

Mungu wangu naenda kulala naomba malaika 14, waende nami, wawili juu, wawili chini, wawili upande wa kuume, wawili upande wa kushoto, wawili wanifunike, wawili waniamshe, wawili wanipeleke juu mbinguni. Mimi mtoto mdogo, roho yangu ni ndogo, haina nafasi kwa mtu yoyote ila kwa Yesu pekee. Amina.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 83

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Anthony Kariuki Guest Apr 25, 2024
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Benjamin Kibicho Guest Apr 22, 2024
πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
πŸ‘₯ Thomas Mwakalindile Guest Apr 9, 2024
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Mar 21, 2024
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Lucy Wangui Guest Mar 7, 2024
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Irene Makena Guest Feb 22, 2024
πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu
πŸ‘₯ Michael Onyango Guest Feb 7, 2024
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Janet Sumaye Guest Jan 5, 2024
πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
πŸ‘₯ Samuel Were Guest Dec 21, 2023
πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie
πŸ‘₯ David Nyerere Guest Nov 9, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ James Mduma Guest Oct 12, 2023
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Christopher Oloo Guest Oct 10, 2023
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Jacob Kiplangat Guest Jun 15, 2023
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Dorothy Mwakalindile Guest May 14, 2023
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Peter Mugendi Guest Dec 23, 2022
πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
πŸ‘₯ Mary Kidata Guest Nov 24, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ David Chacha Guest Nov 6, 2022
πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu
πŸ‘₯ Betty Kimaro Guest Nov 5, 2022
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ James Kimani Guest Oct 10, 2022
πŸ™β€οΈ Mungu akubariki
πŸ‘₯ Joy Wacera Guest Sep 9, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Lydia Mutheu Guest Jun 1, 2022
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Henry Sokoine Guest Jun 1, 2022
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Carol Nyakio Guest Apr 27, 2022
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Samson Tibaijuka Guest Dec 10, 2021
πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha
πŸ‘₯ Dorothy Majaliwa Guest Oct 11, 2021
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Violet Mumo Guest Oct 1, 2021
πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu
πŸ‘₯ Sarah Karani Guest Jul 21, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest Jul 16, 2021
πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose
πŸ‘₯ Betty Kimaro Guest Jun 21, 2021
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Elizabeth Mrema Guest Apr 24, 2021
πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua
πŸ‘₯ David Kawawa Guest Apr 22, 2021
πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani
πŸ‘₯ Mariam Kawawa Guest Apr 21, 2021
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Linda Karimi Guest Jan 17, 2021
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Moses Kipkemboi Guest Dec 31, 2020
πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka
πŸ‘₯ Peter Mbise Guest Dec 3, 2020
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest Sep 5, 2020
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Dorothy Majaliwa Guest May 20, 2020
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ Rose Mwinuka Guest Mar 28, 2020
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Kevin Maina Guest Mar 28, 2020
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ John Kamande Guest Dec 18, 2019
πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
πŸ‘₯ Edward Lowassa Guest Dec 3, 2019
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Linda Karimi Guest Nov 13, 2019
πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Oct 11, 2019
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Christopher Oloo Guest Sep 25, 2019
πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana
πŸ‘₯ Kevin Maina Guest Aug 20, 2019
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Betty Cheruiyot Guest Aug 18, 2019
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Anna Kibwana Guest Jul 30, 2019
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Grace Njuguna Guest May 10, 2019
πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi
πŸ‘₯ Ruth Kibona Guest Apr 29, 2019
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Apr 26, 2019
πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Feb 22, 2019
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Catherine Mkumbo Guest Feb 9, 2019
πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu
πŸ‘₯ Francis Mrope Guest Jan 9, 2019
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Thomas Mtaki Guest Nov 8, 2018
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Charles Mboje Guest Jul 30, 2018
πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe
πŸ‘₯ Michael Mboya Guest Jul 24, 2018
πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha
πŸ‘₯ Thomas Mwakalindile Guest May 9, 2018
πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
πŸ‘₯ Charles Wafula Guest May 8, 2018
πŸ™πŸ™πŸ™
πŸ‘₯ Agnes Sumaye Guest Apr 15, 2018
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Carol Nyakio Guest Apr 14, 2018
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About