Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/katoliki/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Maswali na Majibu kuhusu Liturujia

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

Misa Takatifu ina sehemu kuu ngapi?

Misa Takatifu ina sehemu kuu mbili
1. Litrujia ya Neno
2. Liturujia ya Ekaristi

Litrujia ya Ekaristi ina sehemu kuu ngapi?

Litrujia ya Ekaristi ina sehemu kuu tatu
1. Matayarisho ya vipaji
2. Sala ya Ekaristi
3. Ibada ya Komunyo

Liturujia ni nini?

Liturujia ni tendo la Kristo mwenyewe na Kanisa la kumtukuza na kumwabudu Mungu Baba; na hivyo kutekeleza fumbo la Wokovu kwa kuwatakasa watu

Liturujia ina nafasi gani katika Kanisa?

Liturujia ambayo ni tendo takatifu kuliko yote ndiyo chemichemi ambayo nguvu ya uhai wa Kanisa inabubujika na Kristo anaendeleza Kazi ya Ukombozi wetu

Katika liturujia waamini wanafanya nini?

Katika Liturujia waamini wanashiriki kwa matendo na kwa Ibada adhimisho lote yaani sala, nyimbo na matendo yote ya Ibada; na asiposhiriki matendo hayo kikamilifu, anakosa mafao kamili ya neema ipatikanayo katika Ibada hiyo.

Kilele cha Liturujia ni nini?

Kilele cha liturujia ni Sadaka Takatifu ya Misa

Kwa namna gani Mungu Baba ndiye asili na lengo la Liturujia?

Mungu Baba ndiye asili na lengo la Liturujia kwa sababu katika liturujia anatujaza Baraka zake katika Mwanae Yesu Kristo, naye anatumiminia Roho Mtakatifu mioyoni mwetu

Katika Liturujia Roho Mtakatifu anatenda nini kuhusiana na Kanisa?

Katika Liturujia Roho Mtakatifu analiandaa Kanisa likutane na Bwana wake

Ni nani hupanga Taratibu za Liturujia?

Mama Kanisa ndiye mwenye kupanga taratibu zote za Liturujia Katika mwaka mzima.
Huu mpango huitwa mwaka wa kanisa

Katika mwaka wa kanisa tunakumbuka nini?

Katika Mwaka wa Kanisa tunakumbuka natunaadhimisha matukio na mafumbo yote ya ukombozi wetu na hivyo twapata neema zake

Adhimisho la Liturujia Hutumia Ishara na Alama zipi?

Adhimisho la Liturujia Hutumia Ishara na Alama zinazohusiana na uumbaji, maisha ya binadamu na historia ya wokovu; nazo ni;
  1. mwanga,
  2. maji,
  3. moto,
  4. kuosha mikono/kupaka mafuta
  5. kumega mkate,
  6. kuwekea mikono n.k

Nani huadhimisha Liturujia?

Liturujia iliyo kazi ya Kristo Kuhani Mkuu na kichwa cha Kanisa huadhimishwa na kusanyiko lote, kila mmoja kulingana na kazi yake.

Liturujia inaadhimishwa wapi?

Liturujia inaadhimishwa pale waamini walipokusanyika kwa lengo hilo; kwa sababu Ibada katika Roho na Kweli ya Agano Jipya haifungwi na mahali fulani tuu, kwani dunia yote ni Takatifu

Liturujia Ifanyike mahali pa namna gani?

Liturujia ifanyike mahali palipoandaliwa vizuri iwezekanavyo kwa kuwa katika tendo la Ibada tunakutana na Mungu

Mwaka wa Kanisa una vipindi vikubwa vingapi?

Mwaka wa Kanisa una vipindi vikubwa vitano ambavyo ni;
1. Majilio = Majuma manne
2. Noeli = Kuzaliwa hadi Epifania
3. Kwaresma = Majuma sita na Juma Kuu
4. Pasaka = Siku ya Pasaka hadi Pentekoste
5. Kipindi cha mwaka majuma 34

Majilio ni nini?

Majilio ni kipindi cha Dominika nne cha kujiandaa na Sherehe ya Kuzaliwa Bwana wetu Yesu Kristo, yaani NOELI.
Kinawakilisha karne zote za Agano la Kale

Kwaresma ni nini?

Kwaresma ni kipindi cha siku 40 cha kujiandaa kuadhimisha Sherehe kuu ya PASAKA yaani kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
Tunajiandaa kwa Kufunga Kusali, Kutubu, na Matendo Mema.

Wakati wa kwaresma yawapasa waamini kufanya nini?

Waamini wanapaswa kujitakasa zaidi kwa;
  1. kusali,
  2. kufunga,
  3. toba na
  4. matendo mema

Kipindi cha Pasaka hudumu kwa siku ngapi?

Kipindi cha Pasaka hudumu kwa siku 50;
Yaani kuanzia Sherehe ya Pasaka hadi Sherehe ya Pentekoste

Siku za Dominika Kanisa huadhimisha nini?

Kila Dominika Kanisa Huadhimisha kumbukumbu ya Fumbo la Pasaka; Yaani;
Mateso, Kifo na Ufufuko wa wa Bwana, katika hali ya kutomwagika damu tena.

Kwa nini Jumapili inapaswa kuitwa siku ya Bwana au Dominika?

Jumapili inapaswa kuitwa Siku ya Bwana au Dominika kwa sababu ndiyo siku Bwana amefufuka Mshindi wa Dhambi na Mauti

Kipindi cha Mwaka ni nini?

Kipindi cha Mwaka ni kipindi cha kufurahi kuishi matunda ya ukombozi wetu

Sikukuu Kubwa Kupita zote Katika Kanisa ni ipi?

Sikukuu Kubwa Kupita zote Katika Kanisa ni PASAKA
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Violet Mumo (Guest) on July 12, 2024

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

David Chacha (Guest) on January 7, 2024

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Anthony Kariuki (Guest) on November 30, 2023

Mwamini Bwana; anajua njia

Grace Mushi (Guest) on October 2, 2023

Mungu ni mwema, wakati wote!

Alex Nakitare (Guest) on June 29, 2023

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Paul Kamau (Guest) on April 19, 2023

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Margaret Anyango (Guest) on April 3, 2023

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Lucy Kimotho (Guest) on December 17, 2022

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Mercy Atieno (Guest) on December 11, 2022

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Jane Malecela (Guest) on August 26, 2022

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Alex Nakitare (Guest) on April 25, 2022

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Lucy Wangui (Guest) on December 31, 2021

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

David Ochieng (Guest) on October 30, 2021

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Joseph Mallya (Guest) on August 23, 2021

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Edward Chepkoech (Guest) on July 12, 2021

Neema ya Mungu inatosha kwako

Stephen Malecela (Guest) on April 26, 2021

Mungu akubariki!

Francis Mrope (Guest) on March 27, 2021

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Mariam Hassan (Guest) on March 9, 2021

Neema na amani iwe nawe.

Nora Lowassa (Guest) on November 27, 2020

Katika imani, yote yanawezekana

Sarah Mbise (Guest) on October 23, 2020

Imani inaweza kusogeza milima

George Tenga (Guest) on September 25, 2020

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Elizabeth Mrema (Guest) on September 12, 2020

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Lucy Kimotho (Guest) on August 9, 2020

Nakuombea πŸ™

Moses Mwita (Guest) on August 2, 2020

Dumu katika Bwana.

John Lissu (Guest) on April 19, 2020

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Charles Mchome (Guest) on April 10, 2020

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Agnes Njeri (Guest) on April 8, 2020

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Susan Wangari (Guest) on March 20, 2020

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Daniel Obura (Guest) on March 9, 2020

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Kenneth Murithi (Guest) on February 19, 2020

Rehema hushinda hukumu

Thomas Mtaki (Guest) on October 25, 2019

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Francis Mrope (Guest) on September 23, 2019

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Fredrick Mutiso (Guest) on September 19, 2019

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Lydia Wanyama (Guest) on September 16, 2019

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Miriam Mchome (Guest) on September 14, 2019

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Anthony Kariuki (Guest) on August 29, 2019

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Francis Njeru (Guest) on August 24, 2019

Baraka kwako na familia yako.

Ann Wambui (Guest) on October 13, 2018

Nguvu hutoka kwa Bwana

Margaret Anyango (Guest) on April 29, 2018

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Edward Chepkoech (Guest) on January 9, 2018

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Henry Mollel (Guest) on May 5, 2017

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Esther Nyambura (Guest) on April 25, 2017

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Alex Nakitare (Guest) on October 8, 2016

Endelea kuwa na imani!

Catherine Naliaka (Guest) on April 4, 2016

Sifa kwa Bwana!

Alice Mrema (Guest) on March 16, 2016

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Edwin Ndambuki (Guest) on March 7, 2016

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Thomas Mtaki (Guest) on February 16, 2016

Mwamini katika mpango wake.

Peter Tibaijuka (Guest) on October 21, 2015

Tumaini ni nanga ya roho

Nancy Kabura (Guest) on September 3, 2015

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Mercy Atieno (Guest) on August 22, 2015

Rehema zake hudumu milele

Related Posts

Amri ya Sita ya Mungu: Kutunza usafi wa moyo na kuwa waaminifu

Amri ya Sita ya Mungu: Kutunza usafi wa moyo na kuwa waaminifu

Katika Amri ya Sita na Tisa Mungu ametuamuru nini?Read More

Maswali na Majibu kuhusu Malaika

Maswali na Majibu kuhusu Malaika

Read More

Mambo ya muhimu kujua kuhusu Sakramenti ya Kipaimara

Mambo ya muhimu kujua kuhusu Sakramenti ya Kipaimara

Read More
Amri ya Kwanza ya Mungu: Mambo Muhimu ya Kuzingatia

Amri ya Kwanza ya Mungu: Mambo Muhimu ya Kuzingatia

Katika amri ya kwanza ya Mungu tumeamriwa nini?... Read More

Maswali yanayoulizwa sana kuhusu Ibada ya Kanisa Katoliki

Maswali yanayoulizwa sana kuhusu Ibada ya Kanisa Katoliki

Read More

Mafundisho kuhusu Binadamu, Mtu na Utu

Mafundisho kuhusu Binadamu, Mtu na Utu

Read More

Mambo ya Muhimu kufahamu kuhusu Mungu

Mambo ya Muhimu kufahamu kuhusu Mungu

Read More

Je, Kanisa Katoliki linatambua na kufundisha Maandiko Matakatifu kuwa Neno la Mungu?

Je, Kanisa Katoliki linatambua na kufundisha Maandiko Matakatifu kuwa Neno la Mungu?

Je, Kanisa Katoliki linatambua na kufundisha Maandiko Matakatifu kuwa Neno la Mungu? Ndio! Kanisa... Read More

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha Ndoa kama sakramenti ya agano la upendo na uaminifu?

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha Ndoa kama sakramenti ya agano la upendo na uaminifu?

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha Ndoa kama sakramenti ya agano la upendo na uaminifu?... Read More

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu msamaha na rehema?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu msamaha na rehema?

Leo tutajadili kuhusu imani ya Kanisa Katoliki kuhusu msamaha na rehema. Kwa Wakatoliki, msamaha ... Read More

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa kutubu na kumgeukia Mungu katika wongofu wa moyo?

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa kutubu na kumgeukia Mungu katika wongofu wa moyo?

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa kutubu na kumgeukia Mungu katika wongofu ... Read More

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa sala katika maisha ya Kikristo?

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa sala katika maisha ya Kikristo?

Sala ni sehemu muhimu katika maisha ya Kikristo. Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa... Read More