Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/katoliki/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Magonjwa ya zinaa na dalili zake

Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image
Kuna magonjwa mengi tofauti ya zinaa, lakini yale ambayo yameenea sana ni kisonono, kaswende, klamdia, kankroidi, utando mweupe , Virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Shida kubwa ya magonjwa mengi ya zinaa ni kwamba dalili zake hazionekani kwa urahisi na kama yasipotibiwa kikamilifu yanaweza kuleta madhara makubwa. Maelezo kuhusu magonjwa ya zinaa yaliyoenea sana ni kama yafuatayo:

Kisonono:

Huchukua muda wa siku 1 hadi 14 tangu kuambukizwa mpaka kuonyesha dalili za kuumwa. Kwa wanawake dalili za kisonono ni maumivu chini ya tumbo ambayo yanaweza kuambatana na homa na kutokwa uchafu ukeni. Wapo wanawake wengine ambao hawaoni dalili zozote. Kwa wanaume dalili ni kutokwa na usaha uumeni na kupata maumivu wakati wa kukojoa. Athari yake kwa mwanamke ni kuziba mirija ya kupitisha mayai na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi, na vilevile ugumba. Kwa mtoto aliye tumboni mwa mama mjamzito kisonono cha mama yake kinaweza kusababisha upofu. Kwa mwanaume athari yake ni kuziba mirija ya kupitisha mkojo.
The ListPages module does not work recursively.

Kaswende:

Dalili ya kaswende kwa mwanamke ni vidonda sehemu za siri hasa kwenye mashavu ya uke na sehemu ya njia ya haja kubwa, pamoja na sundosundo sehemu ya siri. Kwa mwanaume dalili ni vidonda. Mara nyingi kimoja kwenye kichwa cha uume, kwenye kishina cha uume na kuzunguka njia ya haja kubwa. Pia mwanaume anaweza kupata sundosundo sehemu za siri. Ugonjwa huu husababisha matatizo ya moyo, na kuharibu ubongo na kuzaa watoto walemavu.

Klamdia:

Dalili yake kwa mwanamke mara nyingi siyo rahisi kuonekana. Kwa mwanaume dalili ni kupata maumivu wakati wa kukojoa, na kukojoa mara kwa mara. Athari kwa mwanamke ni kuziba kwa mirija ya kupitisha mayai na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi. Mimba hizi kuhatarisha maisha ya mama na kuleta ugumba vinaweza kutokea. Kwa mwanaume athari ni kuziba mirija ya kupitisha mbegu na utasa.
The ListPages module does not work recursively.

Kankroidi:

Dalili yake ni vidonda sehemu za siri vinavyokuwa na maumivu makali, maumivu wakati mkojo unapopita kwenye vidonda na kuvimba tezi sehemu za siri. Tezi huweza kupasuka na kutoa uchafu na maumivu makali.

Utando mweupe:

Dalili kwa mwanamke ni kutokwa na uchafu ukeni (kama maziwa yaliyoganda), kuwashwa na kuwa na michubuko sehemu za siri. Kwa mwanaume ni kuwashwa sehemu za siri na kusikia maumivu wakati wa kukojoa. Athari ni maumivu wakati wa kujamiiana.
The ListPages module does not work recursively.

Virusi vya UKIMWI:

Katika hatua ya mwanzo baada ya kuambukizwa hakuna dalili maalum. Hatua hii inaweza kuchukua mpaka miaka kumi. Lakini mara mtu anapoanza kuugua UKIMWI dalili zinakuwa nyingi. Pamoja na kupungua kinga ya mwili, kupungua uzito na kuumwa mara kwa mara. Matokeo ya kuugua UKIMWI baada ya muda fulani ni kifo.
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Je, inachukua muda gani tangu mtu aambukizwe na VVU hadi vionekane kwenye damu?

Je, inachukua muda gani tangu mtu aambukizwe na VVU hadi vionekane kwenye damu?

Inakadiriwa huchukua miezi mitatu tangu kuambukizwa na VVU hadi i virusi hivyo vionekane kwenye d... Read More

Je, Ni Vipi naweza Kukabiliana na Hisia za Kutokuwa Tayari kwa Ngono?

Je, Ni Vipi naweza Kukabiliana na Hisia za Kutokuwa Tayari kwa Ngono?

Je, Ni Vipi naweza Kukabiliana na Hisia za Kutokuwa Tayari kwa Ngono? 😊

  1. Kwanz... Read More

Jinsi ya Kujikinga na Maambukizi ya Kisonono na Kaswende

Jinsi ya Kujikinga na Maambukizi ya Kisonono na Kaswende

Jinsi ya Kujikinga na Maambukizi ya Kisonono na Kaswende 🌟

Karibu sana kwenye makala hi... Read More

Vidokezo vya Kuepuka Mazungumzo ya Kuchosha na Msichana

Vidokezo vya Kuepuka Mazungumzo ya Kuchosha na Msichana

Mazungumzo ni sehemu muhimu katika uhusiano wowote wa kimapenzi. Lakini kuna wakati mazungumzo ya... Read More

Kwa nini nao watu wanaishi kwenye ndoa wanapata maambukizi ya virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Kwa nini nao watu wanaishi kwenye ndoa wanapata maambukizi ya virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Kuna sababu kuu mbili i kwa wana ndoa kupata maambukizi i ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI.
Kw... Read More

Inakuaje mwanaume anaonyesha dalili za magonjwa ya zinaa zaidi kuliko mwanamke?

Inakuaje mwanaume anaonyesha dalili za magonjwa ya zinaa zaidi kuliko mwanamke?

Wanaume mara nyingi huambukizwa sehemu za mrija wa mkojo. Katika sehemu hizi ni rahisi kusikia mw... Read More

Je, mwanamke ambaye ana hedhi kila mwezi, inawezekana kuwa mgumba?

Je, mwanamke ambaye ana hedhi kila mwezi, inawezekana kuwa mgumba?

Ndiyo, i inawezekana kwamba mwanamke anayepata hedhi yake kila mwezi akawa mgumba. Na vilevile i ... Read More

Ndoa ya kulazimishwa

Ndoa ya kulazimishwa

Ndoa ya kulazimishwa ni ile ambayo mwanamume au mwanamke
anaozwa bila yeye mwenyewe kukubali... Read More

Je, watu wanapendelea kutumia muda mwingi katika mchezo wa hatua wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Je, watu wanapendelea kutumia muda mwingi katika mchezo wa hatua wakati wa ngono/kufanya mapenzi?

Habari yako rafiki, leo tutajadili kuhusu swali linaloulizwa sana kuhusu watu kwa nini wanapendel... Read More

Je, mtu anaweza kuambukizwa virusi vya UKIMWI na UKIMWI iwapo atavaliana nguo na mtu mwenye Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Je, mtu anaweza kuambukizwa virusi vya UKIMWI na UKIMWI iwapo atavaliana nguo na mtu mwenye Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Hapana, Virusi vya UKIMWI na UKIMWI hauambukizwi kwa kuvaliana nguo na mgonjwa, kwa sababu vijidu... Read More

Nifanye nini ili kujua kama nina au sina maambukizi ya Virusi vya UKIMWI?

Nifanye nini ili kujua kama nina au sina maambukizi ya Virusi vya UKIMWI?

Ipo njia moja ya kuhakikisha kama umeambukizwa Virusi vya UKIMWI na UKIMWI au hapana. Njia hii ni... Read More

Nifanyeje kujiepusha na vishawishi vya mpenzi wangu vinavyoweza kunifanya nisitumie kondomu?

Nifanyeje kujiepusha na vishawishi vya mpenzi wangu vinavyoweza kunifanya nisitumie kondomu?

Mara nyingine siyo rahisi kujiepusha na vishawishi vya kujamiiana bila kutumia kondomu kutokana n... Read More

πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About