Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA, MEI 21, 2023:<br>DOMINIKA YA 7 YA PASAKA<br>SHEREHE YA KUPAA BWANA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

MWANZO:
Mdo. 1:11

Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Atakuja vivyo hivyo mlivyomwona akienda zake mbinguni, Aleluya.

SOMO 1

Mdo. 1:1-11

Kitabu kile cha kwanza nalikiandika, Theofilo, katika habari ya mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha, hata siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua; wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu. Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu; ya kwamba Yohane alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache.

Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme? Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe. Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.

Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao. Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe, wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 47 : 1-2, 5-6, 7-8, (K) 5

(K) Mungu amepaa kwa kelele za shangwe, Bwana kwa sauti ya baragumu. au: Aleluya

Enyi watu wote, pigeni makofi,
Mpigieni Mungu kelele kwa sauti ya shangwe,
Kwa kuwa Bwana Aliye juu, mwenye kuogofya,
Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote. (K)

Mungu amepaa kwa kelele za shangwe,
Bwana kwa sauti ya baragumu.
Mwimbieni Mungu, naam, imbeni;
Mwimbieni mfalme wetu, naam, imbeni. (K)

Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote,
Imbeni kwa akili.
Mungu awamiliki mataifa,
Mungu ameketi katika kiti chake kitakatifu. (K)

SOMO 2

Efe 1 : 17-23

Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye; macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo; na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake; aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

SHANGILIO

Mt. 28:19-20

Aleluya, aleluya,
Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, na tazama, mimi nipo pamoja nanyi sikuzote.
Aleluya.

INJILI

Mt. 28:16-20

Wale wanafunzi kumi na mmoja walikwenda Galilaya mpaka mlima ule aliowaagiza Yesu. Nao walipomwona, walimsujudia; lakini baadhi yao waliona shaka. Yesu akaja kwao, akasema nao, akawambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi sikuzote, hata ukamilifu wa dahari.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Elizabeth Mtei Guest Apr 27, 2024
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest Oct 25, 2023
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ David Chacha Guest Apr 7, 2023
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Lydia Mahiga Guest Feb 27, 2023
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest Oct 25, 2022
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Vincent Mwangangi Guest Oct 22, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Grace Majaliwa Guest Dec 19, 2021
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Isaac Kiptoo Guest Dec 1, 2021
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ John Mushi Guest Nov 14, 2021
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Michael Onyango Guest Nov 7, 2021
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ John Malisa Guest Sep 27, 2021
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Joyce Aoko Guest May 18, 2021
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Grace Njuguna Guest Dec 10, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest Sep 11, 2020
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Wilson Ombati Guest Dec 16, 2019
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ George Tenga Guest Oct 23, 2019
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Anna Sumari Guest Jun 26, 2019
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Charles Mrope Guest Jun 4, 2019
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Anthony Kariuki Guest May 26, 2019
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Nancy Kawawa Guest Feb 24, 2019
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Frank Sokoine Guest Jan 26, 2019
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ James Malima Guest Jan 25, 2019
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Sarah Achieng Guest Jan 7, 2019
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Catherine Naliaka Guest Dec 6, 2018
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest Aug 28, 2018
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ James Kawawa Guest Aug 20, 2018
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest Aug 13, 2018
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Andrew Mchome Guest Jun 11, 2018
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ James Kimani Guest Jan 6, 2018
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Margaret Anyango Guest Nov 28, 2017
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Sarah Karani Guest Oct 3, 2017
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Elizabeth Mtei Guest Aug 16, 2017
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest May 23, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Patrick Akech Guest Apr 26, 2017
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Lucy Mahiga Guest Apr 10, 2017
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Grace Minja Guest Mar 20, 2017
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Janet Mwikali Guest Jan 22, 2017
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ James Malima Guest Aug 2, 2016
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Peter Otieno Guest Jul 17, 2016
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Victor Kamau Guest Mar 31, 2016
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Betty Akinyi Guest Feb 4, 2016
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ David Ochieng Guest Feb 2, 2016
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Alice Wanjiru Guest Jan 20, 2016
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Victor Sokoine Guest Jan 6, 2016
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Dec 31, 2015
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ John Mushi Guest Dec 24, 2015
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Joyce Aoko Guest Nov 23, 2015
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Agnes Sumaye Guest Jul 26, 2015
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ David Sokoine Guest Jun 16, 2015
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Andrew Odhiambo Guest Apr 21, 2015
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About