Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA, JULAI 24, 2021: JUMAMOSI, JUMA LA 16 LA MWAKA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1

Kut. 24:3-8

Musa aliwambia watu maneno yote ya Bwana, na hukumu zake zote; watu wote wakajibu kwa sauti moja, wakasema, Maneno yote aliyoyanena Bwana tutayatenda. Basi Musa akayaandika maneno yote ya Bwana, akaondoka asubuhi na mapema, akajenga madhabahu chini ya mlima, na nguzo kumi na mbili, kwa hesabu ya kabila kumi na mbili za Israeli, akapeleka vijana wa wana wa Israeli, waliotoa sadaka za kuteketezwa, wakamchinjia Bwana sadaka za amani za ng’ombe. Musa akatwaa nusu ya ile damu, akaitia katika mabakuli; na nusu ya ile damu akainyunyiza juu ya madhabahu. Kisha akakitwaa kitabu cha agano akakisoma masikioni mwa watu; wakasema, Hayo yote aliyoyanena Bwana tutayatenda, nasi tutatii. Musa akaitwaa ile damu, akawanyunyizia watu, akasema, Hii ndiyo damu ya agano alilolifanya Bwana pamoja nanyi katika maneno haya yote.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI

Zab. 50:1-2, 5-6, 14-15 (K) 14 (K)

Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru. Mungu, Mungu Bwana, amenena, ameiita nchi, Toka maawio ya jua hata machweo yake. Tokea Sayuni,, ukamilifu wa uzuri, Mungu amemulika. (K)

Nikusanyieni wacha Mungu wangu, Waliofanya agano nami kwa dhabihu. Na mbingu zitatangaza haki yake, Kwa maana Mungu ndiye aliye hakimu. (K)

Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; Mtimizie Aliye juu nadhiri zako. Ukaniite siku ya mateso; Nitakuokoa, na wewe utanitukuza. (K)

SHANGILIO

Zab. 8:15

Aleluya, aleluya,

Wanabarikiwa wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao, hulisikia neno la Mungu na kulishika.

Aleluya.

INJILI

Mt. 13:24 – 30

Yesu aliwatolea makutano mfano akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake; lakini watu walipolala akaja adui yake akapanda magugu katikati ya agano, akaenda zake. Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu. Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu? Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye? Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo. Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Edwin Ndambuki Guest Feb 12, 2024
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Lucy Wangui Guest Jan 29, 2024
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Margaret Mahiga Guest Jan 2, 2024
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Betty Akinyi Guest Dec 5, 2023
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ James Malima Guest Dec 4, 2023
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Hellen Nduta Guest Sep 17, 2023
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Jul 24, 2023
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Jackson Makori Guest Jun 24, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Andrew Mchome Guest Jan 22, 2023
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Peter Mugendi Guest Jan 20, 2023
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Lydia Mahiga Guest Jan 7, 2023
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ George Tenga Guest Nov 19, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Grace Majaliwa Guest Aug 30, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Janet Sumaye Guest Aug 5, 2022
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ John Mushi Guest May 18, 2022
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Nancy Akumu Guest Feb 20, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Josephine Nekesa Guest Feb 19, 2022
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Simon Kiprono Guest Jan 28, 2022
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Jackson Makori Guest Jan 3, 2022
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Dec 25, 2021
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Ruth Wanjiku Guest Aug 27, 2021
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ George Ndungu Guest Dec 4, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Andrew Odhiambo Guest Sep 6, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Vincent Mwangangi Guest Jul 5, 2020
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Rose Lowassa Guest May 11, 2020
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Esther Cheruiyot Guest Jan 15, 2020
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Rose Mwinuka Guest Jan 10, 2020
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Esther Nyambura Guest Jun 23, 2019
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Moses Kipkemboi Guest Jun 15, 2019
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Andrew Mchome Guest Jun 11, 2019
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ James Malima Guest Jun 9, 2019
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Monica Lissu Guest May 7, 2019
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ George Ndungu Guest Jan 28, 2019
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Grace Mushi Guest Oct 26, 2018
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Samson Mahiga Guest Oct 15, 2018
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Joseph Kiwanga Guest Sep 9, 2018
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Dorothy Nkya Guest Jun 19, 2018
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Ann Awino Guest Dec 11, 2017
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Charles Mrope Guest Dec 5, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ John Kamande Guest Jun 23, 2017
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Betty Akinyi Guest Feb 18, 2017
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Lydia Wanyama Guest Aug 15, 2016
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Philip Nyaga Guest Jul 16, 2016
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Anthony Kariuki Guest Apr 11, 2016
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Raphael Okoth Guest Mar 1, 2016
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Victor Kamau Guest Dec 14, 2015
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Diana Mallya Guest Dec 2, 2015
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Elizabeth Malima Guest Sep 4, 2015
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Thomas Mwakalindile Guest Jun 8, 2015
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Andrew Mchome Guest Apr 9, 2015
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About