Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA, JUNI 18, 2023: JUMAPILI, JUMA LA 11 LA MWAKA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

SOMO 1Β 

Kut. 19 :2-6

Waisraeli walipokuwa wameondoka Refidimu na kufika jangwa la Sinai, wakatua katika lile jangwa; wakapiga kambi huko wakiukabili mlima. Musa akapanda kwa Mungu, na Bwana akamwita toka mlima ule, akisema, Utawaambia nyumba ya Yakobo, na kuwaarifu wana wa Israeli, maneno haya: Mmeona jinsi nilivyowatendea Wamisri, na jinsi nilivyowachukua ninyi juu ya mbawa za tai, nikawaleta ninyi kwangu mimi. Sasa basi ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na kulishika agano langu, hapo ndipo mtakapokuwa tunu kwangu kuliko makabila yote ya watu; maana dunia yote pia ni mali yangu, nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATIΒ 

Zab. 100 :2-3, 5 (K) 3

(K) Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.

Mtumikieni Bwana kwa furaha;

Njoni mbele zake kwa kuimba. (K)

Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu;

Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake;

Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake. (K)

Kwa kuwa Bwana ndiye mwema;

Rehema zake ni za milele;

Na uaminifu wake vizazi na vizazi. (K)

SOMO 2Β 

Rum. 5 : 6-11

Wapendwa, hapo tulipokuwa hatuna nguvu, wakati ulipotimia, Kristo alikufa kwa ajili ya waovu. Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki; lakini yawezekana mtu kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu aliye mwema. Bali Mungu aonyesha pendo lake veye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi. Basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki katika damu yake, tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye. Kwa maana ikiwa tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kwa mauti ya Mwana wake, zaidi sana baada ya kupatanishwa tutaokolewa katika uzima wake. Wala si hivyo tu, ila pia twajifurahisha katika Mungu kwa Bwana wetu Yesu Kristo, am have kwa yeye sasa tumeupokea huo upatanisho.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

SHANG1LIOΒ 

Yn. 15 :15

Aleluya, aleluya, Ninyi nimewaita rafiki, kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.

Aleluya.

INJILIΒ 

Mt. 9:36-10:8

Yesu alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji. Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake. Akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu, wawatoe, na kupoza

magonjwa yote na udhaifu wa kila aina. Na majina ya hao mitume kumi na wawili ni haya; Wa kwanza Simoni aliyeitwa Petro, na Andrea nduguye; Yakobo wa Zebedayo, na Yohane nduguye; Filipo, na Bartholomayo; Tomaso, na Mathayo mtoza ushuru; Yakobo wa Alfayo, na Thadayo; Simoni Mkananayo, na Yuda Iskariote, naye ndiye mwenye kumsaliti. Hao Thenashara Yesu aliwatuma, akawaagiza, akisema, Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie. Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia. Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.

Neno la Bwana... Sifa kwako Ee Kristo.

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Elizabeth Mrema Guest Jun 28, 2024
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Irene Makena Guest Jul 1, 2023
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ David Kawawa Guest Jan 10, 2023
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Mary Sokoine Guest Dec 24, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Grace Majaliwa Guest Sep 11, 2022
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest Sep 4, 2022
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ Josephine Nekesa Guest Jul 27, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Mercy Atieno Guest Jun 13, 2022
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ John Mwangi Guest Apr 9, 2022
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Victor Sokoine Guest Mar 9, 2022
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Ruth Wanjiku Guest Jan 13, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Andrew Mchome Guest Dec 6, 2021
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Esther Cheruiyot Guest Dec 4, 2021
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest Nov 21, 2021
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Paul Kamau Guest Nov 1, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ Nicholas Wanjohi Guest Sep 14, 2021
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Sarah Karani Guest Apr 1, 2021
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ Monica Nyalandu Guest Mar 16, 2021
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Esther Cheruiyot Guest Feb 2, 2021
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Ruth Kibona Guest Dec 27, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ David Musyoka Guest Nov 9, 2020
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Samuel Were Guest Feb 2, 2020
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Samson Tibaijuka Guest Jan 5, 2020
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Peter Mbise Guest Jul 11, 2019
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest Jun 29, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Wilson Ombati Guest Jun 28, 2019
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Michael Mboya Guest Jun 11, 2019
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ Sharon Kibiru Guest Jun 5, 2019
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Charles Mchome Guest Apr 20, 2019
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ Paul Ndomba Guest Jan 24, 2019
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Catherine Mkumbo Guest Dec 5, 2018
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Nora Lowassa Guest Oct 20, 2018
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ Charles Mrope Guest Sep 9, 2018
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ John Lissu Guest Aug 25, 2018
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Nicholas Wanjohi Guest Jul 3, 2018
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ Nancy Kabura Guest Jun 28, 2018
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Isaac Kiptoo Guest Feb 27, 2018
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Victor Malima Guest Dec 28, 2017
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Bernard Oduor Guest Aug 28, 2017
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Lydia Mutheu Guest Mar 6, 2017
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Anna Malela Guest Feb 27, 2017
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Janet Wambura Guest Dec 20, 2016
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Chris Okello Guest Aug 21, 2016
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Agnes Njeri Guest Aug 8, 2016
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Jane Muthoni Guest Mar 27, 2016
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Josephine Nekesa Guest Jan 10, 2016
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Joseph Kitine Guest Nov 9, 2015
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Moses Kipkemboi Guest Aug 30, 2015
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Janet Mwikali Guest Jul 23, 2015
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Victor Sokoine Guest Apr 27, 2015
Neema ya Mungu inatosha kwako

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About