Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰

MASOMO YA MISA,Β JUMAPILI, JULAI 2, 2023: DOMINIKA LA 13 LA MWAKA

β€’
Author/Editor: Melkisedeck Leon Shine, 2015-2017: AckySHINE.com
Featured Image

MWANZO

Zab. 47:2

Enyi watu wote, pigeni makofi, mpigieni Mungu kelele kwa sauti ya shangwe.

SOMO 1Β 

2 Fal 4:8-11,14-16

Ilikuwa siku moja, Elisha alikwenda Shunemu; na huko kulikuwa na mwanamke mmoja mwenye cheo; nave akamshurutisha aje ale chakula. Ikawa kila alipopita njia ile, huingia kula chakula.

Yule mwanamke akamwambia mumewe, Tazama, mimi naona ya kuwa mtu huyu apitaye kwetu mara kwa mara ni mtu mtakatifu w’a Mungu. Nakuomba, tumfanyie chumba kidogo ukutani; na ndani yake tumwekee kitanda, na meza, na kiti, na kinara cha taa na itakuwa, atujiapo, ataingia humo.

Ikawa siku moja akafikia huko, akaingia katika chumba kile akalala. Akasema, Basi, atendewe nini? Gehazi akajibu, Hakika hana mwana, na mumewe ni mzee. Akamwambia, Kamwite. Naye alipokwisha kuitwa, akasimama mlangoni. Akasema, Panapo wakati huu mwakani, utamkumbatia mwana.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATIΒ 

Zab. 89 : 1-2, 15-18 (K) 1(K)

Fadhili za Bwana nitaziimba milele. Fadhili za Bwana nitaziimba milele; Kwa kinywa changu nitavijulisha vizazi vyote uaminifu wako. Maana nimesema, Fadhili zitajengwa milele;Katika mbingu utauthibitisha uaminifu wako. (K)

Heri watu wale waijuao sauti ya shangwe, Ee Bwana, kuenenda katika nuru ya uso wako. Kwa jina lako hufurahi mchana kutwa,Na kwa haki yako hutukuzwa. (K)

Maana fahari ya nguvu zao ni Wewe, Na kwa radhi yako pern be yetu itatukuka.

Maana ngao yetu ina Bwana,Na mfalme wetu ni wake Mtakatifu wa Israeli. (K)

SOMO 2Β 

Rum. 6:3-4,8-11

Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katikawafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.

Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye; tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena. Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; lakini kwa kule kuishi kwake, amwishia Mungu. Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi, na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.

Neno la Bwana... Tumshukuru Mungu.

SHANGILIOΒ 

Mt. 11:25

Aleluya, aleluya,Β 
Nakushukuru, Baba, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga.Β 
Aleluya.


INJILIΒ 

Mt. 10:37-42


Yesu aliwafundisha mitume wake hivi: Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili. Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili. Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona.

Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma. Ampokeave nabii kwa kuwa ni nabii, atapata thawabu ya nabii; naye ampokeaye mwenye haki kwa kuwa ni mwenye haki, atapata thawabu ya mwenye haki.

Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa ngaa kikombe cha maji ya baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia. haitampotea kamwe thawabu yake.

Neno la Bwana........Sifa kwako Ee Kristo

AckySHINE Solutions
✨ Join AckySHINE for more features! ✨

Comments 50

Please log in or register to comment or reply.
πŸ‘₯ Robert Ndunguru Guest Jul 17, 2024
Nguvu hutoka kwa Bwana
πŸ‘₯ Andrew Mahiga Guest May 9, 2024
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ David Sokoine Guest May 8, 2024
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πŸ‘₯ Betty Kimaro Guest Apr 19, 2024
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πŸ‘₯ John Kamande Guest Apr 6, 2024
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πŸ‘₯ Nancy Kabura Guest Mar 24, 2024
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πŸ‘₯ Rose Waithera Guest Mar 22, 2024
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πŸ‘₯ Michael Onyango Guest Jan 28, 2024
Rehema zake hudumu milele
πŸ‘₯ Edward Chepkoech Guest Dec 17, 2023
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
πŸ‘₯ Monica Lissu Guest Oct 20, 2023
Katika imani, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Tabitha Okumu Guest Dec 12, 2022
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πŸ‘₯ John Lissu Guest Oct 12, 2022
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πŸ‘₯ John Malisa Guest Apr 2, 2022
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πŸ‘₯ Josephine Nekesa Guest Mar 19, 2022
Nakuombea πŸ™
πŸ‘₯ Andrew Odhiambo Guest Mar 16, 2022
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πŸ‘₯ Victor Kimario Guest Feb 24, 2022
Neema ya Mungu inatosha kwako
πŸ‘₯ Bernard Oduor Guest Sep 24, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πŸ‘₯ Elizabeth Mrope Guest Mar 1, 2021
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πŸ‘₯ John Mwangi Guest Jan 27, 2021
Dumu katika Bwana.
πŸ‘₯ Benjamin Masanja Guest Jan 12, 2021
Tembea kwa imani, si kwa kuona
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest Oct 9, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πŸ‘₯ Joseph Njoroge Guest Apr 6, 2020
Mwamini Bwana; anajua njia
πŸ‘₯ Alex Nakitare Guest Oct 8, 2019
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πŸ‘₯ Miriam Mchome Guest Sep 16, 2019
Rehema hushinda hukumu
πŸ‘₯ Alice Mrema Guest Sep 14, 2019
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πŸ‘₯ Charles Mboje Guest Jun 20, 2019
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
πŸ‘₯ Thomas Mwakalindile Guest May 5, 2019
Imani inaweza kusogeza milima
πŸ‘₯ Josephine Nduta Guest Mar 21, 2019
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πŸ‘₯ Nancy Komba Guest Jan 23, 2019
Sifa kwa Bwana!
πŸ‘₯ Peter Mugendi Guest Dec 21, 2018
Endelea kuwa na imani!
πŸ‘₯ Alice Wanjiru Guest May 31, 2018
Mungu ni mwema, wakati wote!
πŸ‘₯ Sarah Mbise Guest Dec 12, 2017
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πŸ‘₯ Joyce Nkya Guest Nov 11, 2017
Baraka kwako na familia yako.
πŸ‘₯ Chris Okello Guest Oct 22, 2017
Tumaini ni nanga ya roho
πŸ‘₯ Jackson Makori Guest Oct 16, 2017
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πŸ‘₯ Daniel Obura Guest Jul 9, 2017
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πŸ‘₯ Francis Mrope Guest Jun 18, 2017
Neema na amani iwe nawe.
πŸ‘₯ George Tenga Guest May 31, 2017
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πŸ‘₯ Alice Mwikali Guest Feb 20, 2017
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πŸ‘₯ Monica Nyalandu Guest Feb 11, 2017
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πŸ‘₯ John Malisa Guest Dec 9, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πŸ‘₯ Ruth Mtangi Guest Dec 7, 2016
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πŸ‘₯ Janet Wambura Guest Dec 4, 2016
Mungu akubariki!
πŸ‘₯ Grace Njuguna Guest Oct 16, 2016
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πŸ‘₯ Sarah Karani Guest Sep 26, 2016
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πŸ‘₯ John Kamande Guest May 28, 2016
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πŸ‘₯ Joy Wacera Guest Apr 23, 2016
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
πŸ‘₯ George Tenga Guest Feb 9, 2016
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πŸ‘₯ Joy Wacera Guest Aug 22, 2015
Mwamini katika mpango wake.
πŸ‘₯ Moses Kipkemboi Guest May 13, 2015
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

πŸ”— Related Posts

🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About